BabuK
JF-Expert Member
- Jul 30, 2008
- 1,845
- 329
SERIKALI imeshauriwa kuongeza juhudi katika kutoa mafunzo, kwa walimu maalumu wa kufundisha watu wenye ulemavu.
Rai hiyo ilitolea juzi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sinza Maalum,jijini Dar es Salaam, Charles Katage, alipokuwa akipokea msaada wa basi la wanafunzi wa shule hiyo, lilitolewa na Kampuni ya Simu za mikononi ya Tigo.
"Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, inapaswa kuongeza nguvu katika kutoa mafunzo kwa walimu ambao ni maalumu katika kufundisha watoto wenye mahitaji maalum (walemavu)," alisema Katage.
Alisema hatua hiyo ni ya muhimu hasa kwa kuzingatia kuwa bila ubunifu wa kufundisha watoto hawa, kazi itakuwa ngumu zaidi.
Akipokea basi hilo lenye thamani ya Sh106 milioni, Katage alisema kwa muda mrefu sasa, shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na tatizo la usafiri, jambo lililosababisha watoto wengi kushindwa kuhudhuria shuleni.
Alisema tatizo hilo pia lilisababisha wanafunzi kushindwa kufanya ziara za kimasomo na kwamba kitendo cha Tigo kutoa basi hilo, kimesaidia mno kupunguza ukubwa wa tatizo.
"Tumekuwa tukishindwa kwenda katika ziara mbalimbali za kielimu kwa sababu ya kukosa usafiri, naona sasa tumepata mkombozi na watoto wetu wamefurahi sana,"alisema Katage.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Benjamini Kulwa, alisema serikali iko katika mchakato wa kuongeza mishahara kwa walimu wanaofundisha watoto walemavu.
"Kwa sasa tuko kwenye mchakato wa kuwaongezea mshahara walimu wanaofundisha elimu maalumu kwani wana kazi kubwa sana,"alisema Kulwa.
Ofias Rasilimali Watu wa Tigo, Bennet Kakorozya,alisema msaada huo kwa shule hiyo, unalenga katika kukuza kiwango cha elimu kwa watoto wenye ulemavu.
Chanzo: Mwananchi
Rai hiyo ilitolea juzi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sinza Maalum,jijini Dar es Salaam, Charles Katage, alipokuwa akipokea msaada wa basi la wanafunzi wa shule hiyo, lilitolewa na Kampuni ya Simu za mikononi ya Tigo.
"Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, inapaswa kuongeza nguvu katika kutoa mafunzo kwa walimu ambao ni maalumu katika kufundisha watoto wenye mahitaji maalum (walemavu)," alisema Katage.
Alisema hatua hiyo ni ya muhimu hasa kwa kuzingatia kuwa bila ubunifu wa kufundisha watoto hawa, kazi itakuwa ngumu zaidi.
Akipokea basi hilo lenye thamani ya Sh106 milioni, Katage alisema kwa muda mrefu sasa, shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na tatizo la usafiri, jambo lililosababisha watoto wengi kushindwa kuhudhuria shuleni.
Alisema tatizo hilo pia lilisababisha wanafunzi kushindwa kufanya ziara za kimasomo na kwamba kitendo cha Tigo kutoa basi hilo, kimesaidia mno kupunguza ukubwa wa tatizo.
"Tumekuwa tukishindwa kwenda katika ziara mbalimbali za kielimu kwa sababu ya kukosa usafiri, naona sasa tumepata mkombozi na watoto wetu wamefurahi sana,"alisema Katage.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Benjamini Kulwa, alisema serikali iko katika mchakato wa kuongeza mishahara kwa walimu wanaofundisha watoto walemavu.
"Kwa sasa tuko kwenye mchakato wa kuwaongezea mshahara walimu wanaofundisha elimu maalumu kwani wana kazi kubwa sana,"alisema Kulwa.
Ofias Rasilimali Watu wa Tigo, Bennet Kakorozya,alisema msaada huo kwa shule hiyo, unalenga katika kukuza kiwango cha elimu kwa watoto wenye ulemavu.
Chanzo: Mwananchi