Acha Uvivu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 525
- 131
Jamaa ana matatizo ya akili. Juzi tar. 24 akawa amechanganyikiwa na akawa mkorofi vibaya sana. Basi alivopelekwa hospital kwa nguvu akapewa dawa za usingizi, kwa kitaalamu 'sedatives'. Bahati mbaya kumbe zilikuwa na nguvu kupita kiasi. Jamaa kapiga mbonji mpaka leo asubuhi tar.26, kapata fahamu . Anaamka anauliza "vipi leo tunaenda kutembelea wapi?" Rafiki yake anastuka, "kutembelea wakati leo siku ya kazi? J3 leo." Jamaa anafoka "acha utani leo siku kuu ya krismas." Rafiki yake ikabidi awe mpole. Samahani jana ndo ilikuwa krismas, bahati mbaya juzi ulipatwa na tatizo la akili ukapewa dawa za usingizi. Ukweli mpaka sasa wanajf mahali hapa bado hapajaeleweka. Jamaa anadai krismas yake. Bahati mbaya siku haziwezi kurudishwa nyuma. Nadhani ushauri hapa unahitajika, vurugu tupu jamaa hakubali. Picha ninazo kwenye simu lakini bahati mbaya siwezi ku-upload.