Hio ndio stand bora kwa sasa afrika mashariki na kati.
Stand ya ubungo jijini Dsm ambayo ndiyo stand mama kwa Tanzania yenyewe imekuwa kama gofu lilopigwa bomu na mgambo wa Al qaeda katika vita ya Iraq kwa namna ilivyokuwa hovyo kwa kuwa na uchakavu wa kila namna na majengo yaliyochoka sana pale stand ya ubungo
Kwakweli Mara ya kwanza kupita pale Msamvu sikuamini kama ni Tz ,nikajisemea moyoni kumbe inawezekana kwakweli stendi ya Msamvu ndio Bora kushinda zote Tz ina mandhari nzuri ,imepangwa vzr na ina utaratibu mzuri wa kuingia na kutoa mabasi na huduma za kijamii zilizoboreshwa.
Hio ndio stand bora kwa sasa afrika mashariki na kati.
Stand ya ubungo jijini Dsm ambayo ndiyo stand mama kwa Tanzania yenyewe imekuwa kama gofu lilopigwa bomu na mgambo wa Al qaeda katika vita ya Iraq kwa namna ilivyokuwa hovyo kwa kuwa na uchakavu wa kila namna na majengo yaliyochoka sana pale stand ya ubungo
Unazungumzia Mwanza?Mikoa hii ya Mza na Shinyanga ni ya watu kuvuna na kuondoka.Wamevuna sana huku na kupaacha hovyo halafu unashangaa viongozi wala hawachukui hatua.Labda awamu hii tunaweza kushuhudia angalau mabadiliko kidogo.
Angalia stand ya Shinyanga,ni lami isiyo na kiwango kabisa lakini mamilioni yaliyotumika hapo ndo utachoka!Vyoo utadhani vya shule ya msingi ya porini kabisa!Vichafu utadhani maji hakuna!Huu mkoa nadhani viongozi ni wachawi sana kiasi kwamba hata akija Majaliwa sijui kama atawafanya lolote!