This Friday on Star TV: TCRA na Changamoto ya Digitali

This Friday on Star TV: TCRA na Changamoto ya Digitali

Kabla ya king'amuzi nilikuwa naangalia kipindi cha tuongee asubuhi bila tabu ila kwa sasa mpaka natamani nikawatupie hili li dekoda hao jamaa...nimekosa kipindi hiki kwa sababu ya wao kulamba ten percent. ndio tatizo la kukurupuka kwa kweli...yaani hapa mara yanakatika mara yanajiunga...tabu tupu!
 
Nimejaribu kufuatilia huu mjadala nimemshangaa huyo jamaa kadanganya amekosa nauli ya kwenda kwao moshi kidogo kasahau kuwa kasema hivyo akasema kama atapatikana mtu kutoka mwanza atamlipia nauli aje dar kufundishwa ushauri wangu mtu alipie kulinga na matumizi yake
 
TV hatuoni naona ving'amuzi navyo vimeng'amuka, hata redio nazo zilisha anza shida, eti radio nazo zinahitaji vig'amuzi? Pia washauri hao wakurugenzi wa TCRA wajiunge na JF na weka uzi hapa tutaongea mpaka lyamba. Powa nitajitahidi kuangalizia kwa jirani
 
Yahya tununue vingapi au kipi mana ni mkanganyo mi binafsi siwaelewi hawa TCRA.
 
Kwani local channels ni tbc,itv,eatv,chanel ten na star times tu? Vipi kuhusu clouds,dtv,agape tv,sibuka, na zingine zilizopo hapa nchini si local? Na kama ni local mbona hazioneshwi free kwenye startimes na ving'amuzi vingine?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Yahya Mohamed: kuna mkanganyiko ambao bado wengi wetu hatujauelewa, kuna wengine kutoka TCRA wanasema kua ukishakua na king'amuzi chako basi wenye king'amuzi wanapaswa kuonyesha chaneli za stations tano bure yaani hata kama hujalipia utaziona nazo ni ITV, chanel ten, Sta tv, eatv na TBC. Jana ama leo kama sikosei nikamsikia tena mtu kutoka TCRA akisema, wao wana mamlaka ya kushinikiza TBC ya taifa ndio ionekane kwenye king'amuzi chochote ila hizi nyingine inabidi makubaliano yafanyike kati ya TV na warusha matangazo sasa hapa naomba uulize lipi ni sa hihi.
Kama la kwanza ni sa hihi kwa nini kwenye king'amuzi cha Easy TV mtu usipolipia unaona TV mbili tu nazo ni TBC na Star TV , hizo nyingine tatu hazionekani mpaka ulipie.

Ufafanuzi kutoka kwa Innocent Mungi ni kuwa wana uwezo wa kusihinikiza DSTV kwa mikataba ya kimataifa kuwa na TV ya Taifa katika package yao bure, lakini channel zingine ni makubaliano kati ya msambaza huduma na kituo husika.
 
Kwani local channels ni tbc,itv,eatv,chanel ten na star times tu? Vipi kuhusu clouds,dtv,agape tv,sibuka, na zingine zilizopo hapa nchini si local? Na kama ni local mbona hazioneshwi free kwenye startimes na ving'amuzi vingine?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums


Ufafanuzi kutoka TCRA: ni kwamba channel zenye leseni ya Kitaifa ni tano na hizo ndio zitapatikana katika vingamuzi bure na zile zenye leseni ya kimkoa au kutoa huduma katika miji fulani zitaonekana katika eneo hilo tu kwa utaratibu ambao utawezeshwa na Multiplex operators
 
Ufafanuzi kutoka kwa Innocent Mungi ni kuwa wana uwezo wa kusihinikiza DSTV kwa mikataba ya kimataifa kuwa na TV ya Taifa katika package yao bure, lakini channel zingine ni makubaliano kati ya msambaza huduma na kituo husika.

Yahya vipi kuhusu hivi ving'amuzi vingine ukiacha DST kama vile Easy TV, hizo channel tano tutaziona bure? maana mpaka sasa kwa Easy TV ni chanel mbili tu tunazoziona bure
 
Yahya vipi kuhusu hivi ving'amuzi vingine ukiacha DST kama vile Easy TV, hizo channel tano tutaziona bure? maana mpaka sasa kwa Easy TV ni chanel mbili tu tunazoziona bure

Nikiendelea kunukuu Ufafanuzi wa Mungi katika Kipindi hicho Mkuu, Channel za Free to air kitaifa ni tano ni sheria kwa multiplex operators wote kuwa nazo katika package yao kwa hiyo hata kama mtumiaji hana uwezo wa kulipia premium services ataendelea kuziona regardless ashanunua king'amuzi.

Kwa hiyo ni suala la uzimamizi wa Sheria tu kufanikisha mchakato huo, Ila Easy TV hana leseni ya Multiplex Operator, So far wapo watatu ambao ni AGAPE Associates, Basic Transimission LTD BTL na Star TIMES.

Hakutoa Ufafanuzi kuhusu Easy TV ila kwa mantiki ya kawaida ni aidha apaewe huduma na moja kati ya hawa multiplex kwa channel zake au pia aombe leseni hiyo ambayo ni ghali kuitekeleza kuliko maelezo ya kawaida
 
Yahya Mohamed,
Naomba kukuuliza kwamba, swala la kuhamia digitali limetangazwa zaidi ya miaka miwili. Inakuaje baada ya analogia kuzimwa ndio mnaanza kutangaza kutuletea ving'amuzi tena itakuwa hivi karibuni? Mlikuwa mnasubiri nini? Naona kama vile mnafanya kazi kama ofisi ya zimamoto. Hadi moto utokee ndio mnatoka ofisini kukimbilia kuuzima!!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom