mimi kitu ambacho sijawahi kuelewa ni kwamba hawa USA wanazuia watu wasitengeneze siraha za NUCLEAR kwa madai kwamba watazitumia vibaya sasa swali langu ni kwamba wao wanaozitengeneza watazitumia wapi maana kazi ya siraha ni kujiahami au kudhuru na wanadai hairuhusiwi kutumia hizi siraha sasa kama hairuhusiwi kwanini zitengenezwe.
Well said mkuu, labda niongezee kwamba Taifa hili hili linalo wanyoshea vidole Mataifa mengine ndilo taifa pekee lililowahi kuripua mabomu ya nuclear na kungamiza binadamu wenzao huko Japan, hakuna Taifa lingine Duniani lililowahi kufanya unyama kama huo duniani licha ya kuwa na mabomu ya nuclear!
Wanasayansi walio husika na utengenezaji/hudwaji wa bomu la nuclear walikasilishwa sana na uhamuzi wa Rais Truman (U.S.A) kuangusha bomu Japan wakati hapakuwepo na ulazima wowote wa kufanya hivyo kwa kuwa USA ilisha pata taarifa kwamba wajapan walikuwa mbioni kusitisha vita. Baadae ikaja gundulika kwamba Merikani ilihamua kuangusha Bomu Japan ili kuwa wahi Warusi ambao walikuwa na mpango wa kuivamia Japan baada ya kufanikiwa kumaliza vita Ulaya, vile vile bomu hilo walitaka kuwatisha Warusi ambao walionekana kuwa juu kijeshi wakati wa mapigano huko Ulaya kwa kufanikiwa kuteka makao makuu ya Hitler na kukomboa nchi nyingi za Ulaya ya mashariki na Baltic kutoka mikononi mwa NAZI.
Baada ya baadhi ya wanasayansi wa Merikani kutafakali mwenendo wa Merikani kwa kina wakaona Merikani ikiwa ni nchi pekee yenye mabomu ya Nuclear Dunia hatakuwa salama, ndio maana baadhi ya wana sayansi
(wengine walikuwa ni ma-spy) walifikia uhamuzi wa kuipatia Urusi kwa siri mbinu za kuhunda/tengeneza mabomu ya nuclear, hii ilisaidia sana Urusi kupunguza muda wa utafiti na kufanikiwa kulipua bomu la nuclear within 3/4 years kama sikosei - kitendo hicho kiliwatia wendawazimu Merikani, wakahanza kutafuta mchawi baadhi ya wanasayansi walinyongwa kwa eti usaliti na wengine kufungwa.
Kwa kufupi Merikani huwa aitaki Mataifa mengine yawe na silaha hizo si kwa kuofia kuvamiwa au nini - mawazo yao yako kutaka ku-control mataifa mengine na kufanya wapendavyo ni hilo tu, wanajua fika kwamba taifa lolote likisha kuwa na mabomu ya nuclear si rahisi kukubali kuendeshwa kama puta na Merikani.