Chamoto
JF-Expert Member
- Dec 7, 2007
- 8,328
- 17,537
Mi nilienda Mango kwa Twanga pepeta. Nikawa najichezea zangu pale mbele pamoja na wadau wengine. Mnapafahamu Mango siku ya Jmosi usiku. Katika kucheza wakawepo mabinti wawili wazuri tu nadhani wanatoka chuo fulani. Wakatoka huko nyuma na kuja mbele yangu na mmoja (beautiful) akawa anacheza nami na mara ananipa mgongo n.k. Zikawa kama zinatembea ishara fulani kati yao. Mwisho wa siku mziki uliisha tukaenda kukaa. Inawezeka ni njia ya kutongoza? Unfortunately sikuchukua hatua yoyote maana walikuwa ni wageni kwangu ila roho ilinisuta. Niambieni ili next time nisifanye tena blunders
Rule Of Thumb (just do it)
Unapoona dada kajitokeza tuu ghafla karibu
yako huku akijidai kama yuko bize na shughuli
zake (mfano kucheza mziki) ujue kwamba mambo
poa. Wewe kazi yako ni kumtokea sasa akikataa
au akikubali hiyo si juu yako.
Kwahiyo ndugu yangu siku nyingine usiogope
kukataliwa, usiweke umuhimu wowote katika hilo
tukio (kutongoza) kwasababu hata kama
akikukataa huwezi kudhalilika kwasababu bado
hamfahamiani. Chukulia kama ni kitendo cha
kishujaa na amini nakuambia utajisikia raha
kutoa dukuduku lako na utazidi kujiamini.
Next time just give it a shot, you never know.