The best smartphone 2017... Samsung galaxy S8

Hivi Mkuu Lusungo Ukiacha S8, kuna hii Simu nyingine toka kampuni ya Samsung ambayo ni Galaxy A5(2017) ninayoona kama ni nzuri hasa Ukizingatia pia na suala la gharama....... vipi Unaweza Kunikomentia vipi Kuhusu hii Simu?

Maoni yako tafadhali Mkuu!
 
Mkuu kuna watu walikazana IPhone na number 1 nimewaletea hyo mada wajisomee.... nimepitia specs za hzo simu yaani IPhone X ana haki ya kuwa namba 4
 
A5 2017 ni nzuri but price yake ni far better ukachukua flagship za samsung kama S5..S6 edge au 7 maana hizo zipo juu kupita hyo A5 2017 na price zinalingana
 
Ingawa naamini brand fulani ya simu ni mapenzi ya mtu..bila kusahau uchumi wake...

Ila samsung ni chaguo langu..
1. Camera zake
2. Screen
3. Size.. ya simu nyingi za S Samsung ni moderate ila iphones za nyuma ni ndogo ndogo... zimenilevya..

lusungo huo mtandao ndiyo walisema Samsung and Iphone are the Pepsi and coke.
 
Yeah ni nzuri.
 
Nimenunua A7 ya 2017, so far naona ipo poa tu.
Battery life inakaa zaidi ya masaa 18 hadi 20 ambayo sio mbaya.
Japo iphone siiachi.
Mi naonaga price ya A series ni bora zaidi ukajiongeza kwenye S series....

A7 ya 2017 ni nzuri pia japo sio flagship
 
kwa mtazamo wangu my top 3 ingekuwa hiv
1. LG V30
2. samsung s8
3. Google pxl 2 xl

ila for the best budget phone ONE PLUS 5T is the best.
Mkuu umetumia vigezo vipii
 
A5 2017 ni nzuri but price yake ni far better ukachukua flagship za samsung kama S5..S6 edge au 7 maana hizo zipo juu kupita hyo A5 2017 na price zinalingana
Ok Asante Mkuu kwa Mawazo yako.... S5/6 naona kama zimeanza kupitwa hivi

Nadhani A5 yenyewe inapo shawishi ni ile Internal Memory Capacity yake 32gb.Ram 3gb n. k. nk.....

Nadhani S5/6 ni 16gn kama nitakuwa ryt!

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu umetumia vigezo vipii
hizo zote tatu ni high end phones na zote ziko vizuri kwa upande wa specs...ila kilichonifanya kuiweka lg v30 kuwa ya kwanza ni jinsi walivyoweza kuoptimize matumizi yake ya battery...ukichunguza video nyingi zinazo onesha battery drainage comparisons kati ya hizo simu hapo juu lg v30 imekuwa ikishika no 1...

S8 nimeiweka ya pili kwasababu ya designing yake plus specs ,ijapokuwa kwa specs hawajaachana na v30..designing iliyonivutia ni jinsi walivyoweza kuzipunguza zile bezels bila kualter performance yake.

google pixel 2 XL nimeiweka ya tatu kwa ajili ya camera , S8 iko poa kwenye camera ila kwa selfie hamgusi huyu jamaa. (waweza fuatilia comparisons zilizoko mtandaoni ujionee hizo picha zilizopigwa na hizi simu)...

ONE plus 5T nimeikubali cuz haiko kwenye makundi ya price ya hizo simu tatu nilizozitaja hapo juu ila inakupa specs na performance karibia na hizo hapo juu naweza sema kwa asilimia 88% - 94% ....hata pia nashangaa kwanini mtu anachanganyikiwa na iphone X wakati hata huyu ONE PLUS 5T anaweza kupa performance nzuri kuliko iphone X ....

binafsi naona ni kejeli kufananisha (S8 , google pixel 2 au lg v30) na iphone X

mtazamo tu , sio sheria.
 
Asante mkuu umefafanua vyema leo baada ya kuupitia huo mtandao ndo nimejua mengi ambayo humu tunawekaga ushabiki mbele....

Yaani leo ndio nimegundua hii s8 niliyonayo ni bonge la kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…