TFF:acheni kuwabeba wachezaji wa Kitanzania

Turnkey

JF-Expert Member
Jul 9, 2013
7,359
5,831
Baada ya mechi ya Mc Alger na Yanga kumalizika ,nimejiuliza maswali mengi sana.Kweli kwa aina ya wachezaji wa Kitanzania hata karne tatu zijazo hatuwezi kuchukua kombe lolote la Afrika.Cha kufanya TFF kuruhusu timu kusajili idadi yoyote ya wachezaji wa kigeni..hii itafanya wachezaji wetu kugombania namba na wageni hivyo kufanya viwango vyao viwe juu..mfano TP mazembe wakati wa Samatta ni wachezaji watatu tu wa kicongo walikuwa wanaanza .
 
hii ni kweli mpira sio halmashauri au manispaa useme tulinde ajira zetu wakati hatuuwezi..

hni ngumu sana kushindana kimataifa kwa wachezaji wetu wavivu na wasio na skills za level za juu..

hata mamelod sundown ametwaa ubingwa caf msimu uliopita kwa kutumia wachezaji wageni..
 
Tatizo letu tanzania hakuna kiongozi wa michezo mwenye moyo wa dhati kuendeleza michezo, tunaona nchi za wenzetu wanavyoaandaa pragram mbali mbali za kukuza michezo na kuzismamia. Ila hapa bongo tunataka kuvuna bila kupanda. Mh Kikwete aliwahi kusema ukitaka kula lazima uliwe, TFF hawataki kuliwa. Uongozi wa michezo unang'aniwa hadi mahakamani, mchezaji anaendelea kucheza hata kama ana kadi 30 za njano na TFF hawana habari, wachezaji wanataka mazoezi wanayoyataka wao, ushindi na ubingwa kwa kuhonga timu ndogo ndogo ndio matekeo yake hayo kwa timu zote za Tanzania.
 
Back
Top Bottom