TFDA na TBS wanafanya kazi moja?

TFDA na TBS wanafanya kazi moja?

ng'adi lawi

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2014
Posts
2,956
Reaction score
1,115
Kwa muda mrefu kumekuwa na sintofahamu kati ya TFDA na TBS hasa ktk kutoa vyeti vya ubora na usalama wa vyakula na madawa. Kila shirika lina viwango vyake na vyote ni gharama kwa mfanyabiashara. Ni vema TFDA wawe pekee katika kuthibiti vyakula na madawa na TBS wahusike na viwango vya bidhaa nyingine au wadau mwaonaje? Tunaoagiza bidhaa hizi kutoka nje ya nchi na wenye viwanda tunalipa gharama za kupima ubora mara mbili kwa mini?
 
Ni kweli TFDA na TBS wanafanya kazi moja na siyo hao tu kuna taasisi zaidi ya saba zinafanya kazi moja. Kwa wenye viwanda ongeza OSHA, WMA, FIRE, NEMC, COUNCILS na nyinginezo. Ukizichunguza hizi taasisi zote zinarudia kile ambacho wengine wanafanya. Ukiwauliza wote wanasema wameanzishwa kwa sheria mbalimbali na wanatekeleza sheria. Hii imetokana na kucopy na kupaste sheria mbalimbali kutoka nchi tofauti kwa mfano tunacopy South Africa then tunaenda Ghana kumbe sheria ya South Africa imetake care hiyo sheria ya Ghana, Pia taasisi hizi hulipwa na wafanyabiashara kwahiyo serikalini hawaoni huo mzigo, ndiyo maana bidhaa za Tanzania zinakuwa ghali sana. Maoni yangu ni hizi taasisi zijiendeshe na fedha kutoka serikali kuu na siyo kwa fee au tuwe na taasisi moja au mbali kama mdau anavyoshauri hapo juu. Tanzania haiwezi kuwa nchi ya viwanda wakati kuna taasisi zaidi ya saba ambazo bila wao huwezi fungua kiwanda. NB TBS ndiyo sherika pekee lenye kutengeneza viwango na wote TFDA N.K Hutumia viwango vya TBS bidhaa inapimwa na TBS then TFDA parameter ni zile zile, standard ni hiyo hiyo, hii siyo tu gharama kwafanyabiashara bali pia matumizi mabaya ya wafanyakazi, vifaa na kemikali ambazo mara nyingi tunazinunua kwa fedha za kigeni.
 
Ni kweli TFDA na TBS wanafanya kazi moja na siyo hao tu kuna taasisi zaidi ya saba zinafanya kazi moja. Kwa wenye viwanda ongeza OSHA, WMA, FIRE, NEMC, COUNCILS na nyinginezo. Ukizichunguza hizi taasisi zote zinarudia kile ambacho wengine wanafanya. Ukiwauliza wote wanasema wameanzishwa kwa sheria mbalimbali na wanatekeleza sheria. Hii imetokana na kucopy na kupaste sheria mbalimbali kutoka nchi tofauti kwa mfano tunacopy South Africa then tunaenda Ghana kumbe sheria ya South Africa imetake care hiyo sheria ya Ghana, Pia taasisi hizi hulipwa na wafanyabiashara kwahiyo serikalini hawaoni huo mzigo, ndiyo maana bidhaa za Tanzania zinakuwa ghali sana. Maoni yangu ni hizi taasisi zijiendeshe na fedha kutoka serikali kuu na siyo kwa fee au tuwe na taasisi moja au mbali kama mdau anavyoshauri hapo juu. Tanzania haiwezi kuwa nchi ya viwanda wakati kuna taasisi zaidi ya saba ambazo bila wao huwezi fungua kiwanda. NB TBS ndiyo sherika pekee lenye kutengeneza viwango na wote TFDA N.K Hutumia viwango vya TBS bidhaa inapimwa na TBS then TFDA parameter ni zile zile, standard ni hiyo hiyo, hii siyo tu gharama kwafanyabiashara bali pia matumizi mabaya ya wafanyakazi, vifaa na kemikali ambazo mara nyingi tunazinunua kwa fedha za kigeni.
KUONDOA MKANGANYIKO WOTE TFDA LINGEKUWA TAWI LA SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA TBS
 
Kweli kabisa! hawa jamaa wanasumbua! mi nimegundua kadawa kangu ka kutibu kuku. nikaamua nikajali, nikaenda kwa TFDA wakasema lete milion moja. bado kitoka hapo niende TBS. nilipo enda tbs wakasema lete laki nne. mi niko Matombo huku Moro nitapatawapi hio hela jamani! libaki shirika moja tu.
 
Wanafanya kazi nzuri ila wanashindwa kukagua ubora wa vyeti hasa vitokeavyo koromije
 
Jamani tuvumilieni tu maana tunaongozwa na mataahira hayawezi kuliona hilo! Hivi kuna ugumu gani kuzifanya TFDA, WMA kuwa idara ndani ya TBS? Huu ni wizi wa mchana kweupe! Mibunge yetu pumbavvv nayo iko kimya tu!!
 
Back
Top Bottom