Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,183
Edward Lowassa, waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond bado anautaka Urais 2015 kwa bei yoyote ile, licha ya kuchafuka vibaya kimaadili, hii ni kwa mujibu wa vyanzo ndani ya CCM.
Akishindwa kuupata Urais, yuko radhi awe "kingmaker" aweke watu wake ili apate nafasi nyingine ya juu, kama ya Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.
Watu ambao Lowassa anapanga kuwaweka iwapo jina lake litakataliwa na Kamati Kuu ya CCM ni pamoja na Dr. Mohamed Gharib Bilal, Emmanuel Nchimbi na January Makamba.
Iwapo mtu wa Lowassa kutoka Zanzibar (Dr Billal) atapitishwa na CCM kuwa mgombea Urais wa 2015, basi Billal atamchagua Lowassa kama mgombea mwenza (running mate) wake na hivyo kumfanya Lowassa kuwa Makamu wa Rais iwapo watashinda uchaguzi.
Iwapo kati ya Emmanuel Nchimbi au January Makamba atachaguliwa kuwa mgombea Urais 2015 basi yeye Lowassa atateuliwa kuwa executive Prime Minister.
Malengo ya Lowassa kwa 2015 ni haya (in order of importance):
1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Rais wa Tanganyika (katiba mpya ikipita)
3. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
4. Waziri Mkuu wa Tanzania
Kwa kutumia pesa zake za kifisadi na pesa za Rostam Aziz, tajiri namba 1 Tanzania kwa mujibu wa gazeti la Forbes, Lowassa amenunua kuungwa mkono na asilimia 75 ya wabunge wa Tanzania kutoka CCM, CHADEMA na CUF. Lowassa pia amenunua asilimia 80 ya wajumbe wa NEC na asilimia 75 ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. Sasa anakamilisha kununua wajumbe wa Kamati Kuu.
Kamati Kuu ndio kizingiti pekee kwa Lowassa na kundi lake. Wameamua kuwa iwapo Kamati Kuu itatupa jina la Lowassa, basi NEC italazimisha jina la Lowassa lirudishwe ili achaguliwe kuwa mgombea.
Bila shaka CCM ikimuweka Lowassa kama mgombea Urais wa 2015, wapinzani watapata nafasi kubwa ya kushinda Urais kutokana na kiongozi huyu kuchafuka kwa ufisadi na kuleta mpasuko mkubwa ndani ya chama tawala iwapo atateuliwa.
MUNGU IBAIRIKI TANZANIA.... MUNGU TUEPUSHE NA RAIS FISADI 2015
wanaompa ubunge kwanza hawana uzalendo. mtu fisadi aliyekubuhu kama EL hapaswi hata kuwa sheha