Tetemeko Kagera: Mashirika ya nje hayawezi kuwa mbadala wa Serikali

Rweye

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
16,958
7,512
Kwanza niwapongeze sana wenzetu wa FAO kwa kuamua kusaidia kurejesha hari ya chakula na kilimo kwa maeneo yaliyoathirika na tetemeko mkoani Kagera. Tunasema asante kwasababu kusema kweli ni kitambo hawa watu walihitaji msaada na hasa kutoka kwa Serikali lakini hawakuwahi kusaidiwa. Wananchi walilia njaa kwa kukosa chakula na bado Serikali haikuja na mkakati wowote wa dharura. Wananchi walilia wasaidiwe vifaa vya ujenzi kama saruji, mabati na nondo kwa bei nafuu lakini serikali ikawaambia wajenge viwanda vyao. Waliomba wasaidiwe wapatiwe michango ya rambi rambi lakini serikali ikawaambia michango ile haikuwa ya kwao, bali ni kwa ajiri ya kujengea miundombinu. Kiujumla hawa wananchi walitelekezwa na Serikali yao.

Sasa leo Mungu kawaona watu wake, shirika la FAO limewaona na limeamua kuwabeba. Kwa huo msaada uliotolewa wa miaka miwili katika kusaidia shughuri za kilimo na upatikanaji wa chakula si tu itawafuta machozi wahanga, bali pia itawapunguzia unyonge na upweke walioachiwa na Serikali yao. Na naelewa haya hayajaja ghafla tu, naomba tutambue kazi kubwa iliyofanywa na Mama Tibaijuka na Wanakagera wa ndani na nje kwa ujumla katika kutafuta msaada kutoka nje kwa ajiri ya kutatua athari za tetemeko. Tunawashukuru pia kikundi cha Face Bukoba kwa juhudi zao walizozionesha mpaka sasa. Mungu awatie nguvu na awaongoze.

Mwisho nimalizie kwa kusema, Serikali ipo kikatiba na kusaidia watu wake ni wajibu kikatiba. Ifahamike hata ikipita miaka mingapi, bado Serikali itabaki na hili deni kwa wana Kagera. Mashirika na makundi watafanya yao lakini deni la Serikali kwa huu mkoa halitaisha kamwe. Ni jukumu la wananchi kuona ni namna gani wanailazimisha Serikali kuwajibika kwao, kwa njia za kisheria ama kwa misingi ya kisiasa.
 
Nakuunga mkono kwenye uliyoyaandika lakini swali langu kwako ni hili. Kwanini huwa unaikosoa Serikali hii ambayo imejaa madudu chungu nzima inapokuja kwenye issues za Kagera tu na hasa hili la tetemeko la ardhi lakini madudu chungu nzima mengine nchini yanayoathiri kila kona ya nchi yetu huwa hutii neno!? KULIKONI!?

Kwanza niwapongeze sana wenzetu wa FAO kwa kuamua kusaidia kurejesha hari ya chakula na kilimo kwa maeneo yaliyoathirika na tetemeko mkoani Kagera. Tunasema asante kwasababu kusema kweli ni kitambo hawa watu walihitaji msaada na hasa kutoka kwa Serikali lakini hawakuwahi kusaidiwa. Wananchi walilia njaa kwa kukosa chakula na bado Serikali haikuja na mkakati wowote wa dharura. Wananchi walilia wasaidiwe vifaa vya ujenzi kama saruji, mabati na nondo kwa bei nafuu lakini serikali ikawaambia wajenge viwanda vyao. Waliomba wasaidiwe wapatiwe michango ya rambi rambi lakini serikali ikawaambia michango ile haikuwa ya kwao, bali ni kwa ajiri ya kujengea miundombinu. Kiujumla hawa wananchi walitelekezwa na Serikali yao.

Sasa leo Mungu kawaona watu wake, shirika la FAO limewaona na limeamua kuwabeba. Kwa huo msaada uliotolewa wa miaka miwili katika kusaidia shughuri za kilimo na upatikanaji wa chakula si tu itawafuta machozi wahanga, bali pia itawapunguzia unyonge na upweke walioachiwa na Serikali yao. Na naelewa haya hayajaja ghafla tu, naomba tutambue kazi kubwa iliyofanywa na Mama Tibaijuka na Wanakagera wa ndani na nje kwa ujumla katika kutafuta msaada kutoka nje kwa ajiri ya kutatua athari za tetemeko. Tunawashukuru pia kikundi cha Face Bukoba kwa juhudi zao walizozionesha mpaka sasa. Mungu awatie nguvu na awaongoze.

Mwisho nimalizie kwa kusema, Serikali ipo kikatiba na kusaidia watu wake ni wajibu kikatiba. Ifahamike hata ikipita miaka mingapi, bado Serikali itabaki na hili deni kwa wana Kagera. Mashirika na makundi watafanya yao lakini deni la Serikali kwa huu mkoa halitaisha kamwe. Ni jukumu la wananchi kuona ni namna gani wanailazimisha Serikali kuwajibika kwao, kwa njia za kisheria ama kwa misingi ya kisiasa.
 
Nakuunga mkono kwenye uliyoyaandika lakini swali langu kwako ni hili. Kwanini huwa unaikosoa Serikali hii ambayo imejaa madudu chungu nzima inapokuja kwenye issues za Kagera tu na hasa hili la tetemeko la ardhi lakini madudu chungu nzima mengine nchini yanayoathiri kila kona ya nchi yetu huwa hutii neno!? KULIKONI!?
Sidhani mkuu, toa mfano wa unachokisema na mie ntakwambia maeneo mengine ninakokosoa bila kuangalia sura
 
Madudu chungu nzima kama ya Bajeti ya 29 trillion lakini pesa zilizotolewa ni 34%, issue ya vyeti vya Bashite na uvamizi wake na kwanini hafutwi kazi wakati Nape ambaye hakuwa na kosa lolote lile ndiye aliyefutwa kazi. Kudharau katiba na Bunge hata siku moja sijakusoma humu ukiandika kuhusu madudu haya. Na haya ni machache tu. Mbona humu pamoja na kuwa wengi wetu si wa kutoka Kagera tulipiga kelele sana kuanzia alipotaka kuondoka nchini kwenda Zambia kwenye sherehe za kuapishwa Rais mpya na ukwapuaji wa bilioni 16 za wahanga wa tetemeko.

Ushauri wangu kwako usiilamu Serikali pale inapohusiana na mambo ya Kagera tu bali mambo yote yale ambayo yanawaathiri Watanzania wote bila kujali wanatokea mkoa upi nchini.

Sidhani mkuu, toa mfano wa unachokisema na mie ntakwambia maeneo mengine ninakokosoa bila kuangalia sura
 
Madudu chungu nzima kama ya Bajeti ya 29 trillion lakini pesa zilizotolewa ni 34%, issue ya vyeti vya Bashite na uvamizi wake na kwanini hafutwi kazi wakati Nape ambaye hakuwa na kosa lolote lile ndiye aliyefutwa kazi. Kudharau katiba na Bunge hata siku moja sijakusoma humu ukiandika kuhusu madudu haya. Na haya ni machache tu. Mbona humu pamoja na kuwa wengi wetu si wa kutoka Kagera tulipiga kelele sana kuanzia alipotaka kuondoka nchini kwenda Zambia kwenye sherehe za kuapishwa Rais mpya na ukwapuaji wa bilioni 16 za wahanga wa tetemeko.

Ushauri wangu kwako usiilamu Serikali pale inapohusiana na mambo ya Kagera tu bali mambo yote yale ambayo yanawaathiri Watanzania wote bila kujali wanatokea mkoa upi nchini.
Watanzania tuko wengi mkuu na kila mtu ana utashi wake. Na si lazima kila mtu alete post hapa, kwanza tambua kila mtu ana kitu kinachomuuma. Pili kila stori ina ukweli wake, janga haliwezi kulinganishwa na mambo ya kipuuzi ya kisiasa za hovyo. Siasa eti za akina uliowataja ama kwa ujumla wa siasa ni unafiki, uongo, ulaghai na kutafuta sifa. Sasa nikiamua kutoyaongelea hayo yawezekana sioni impact yake kwasababu siasa si 'hasa'. Tunasave mda wetu kwa kutoongelea mambo ya hivi kila siku. Ishu ya janga si ya siasa na ulipima uzito wa kinachosemwa ndo utaona na wewe uchangie ama uache. Nne, ni historia ya wahusika ya mkoa huu pia inaleta hisia zake tofauti na hasa linapokuja suala la majanga naichukulia kama special zone, kitu special ni exceptional kwa kila kitu. Ninazo sababu nyingi sana ninapoamua kufanya jambo lakini kikubwa zaidi huwa sifati mkumbo na ushabaki, umri wa kufanya hayo ushanipita mbali. Samahani kama ntakuwa nimekukwaza
 
Sijasema umenikwaza. Kwa hiyo utashi wako wewe ni kufumbia macho madudu mengine yote nchini ila yale ya Kagera tu ndiyo ambayo utaikoromea Serikali?

Huoni impact ya madudu mengi ndani ya Serikali hii kwa Watanzania wote kwa mfano bajeti ya 29 trilioni lakini zilizotolewa ni less than 50% lakini unaona impact pale ambapo Serikali haisadii hata senti moja kwa wahanga wa tetemeko. Sawa nimekuelewa Mkuu.

Watanzania tuko wengi mkuu na kila mtu ana utashi wake. Na si lazima kila mtu alete post hapa, kwanza tambua kila mtu ana kitu kinachomuuma. Pili kila stori ina ukweli wake, janga haliwezi kulinganishwa na mambo ya kipuuzi ya kisiasa za hovyo. Siasa eti za akina uliowataja ama kwa ujumla wa siasa ni unafiki, uongo, ulaghai na kutafuta sifa. Sasa nikiamua kutoyaongelea hayo yawezekana sioni impact yake kwasababu siasa si 'hasa'. Tunasave mda wetu kwa kutoongelea mambo ya hivi kila siku. Ishu ya janga si ya siasa na ulipima uzito wa kinachosemwa ndo utaona na wewe uchangie ama uache. Nne, ni historia ya wahusika ya mkoa huu pia inaleta hisia zake tofauti na hasa linapokuja suala la majanga naichukulia kama special zone, kitu special ni exceptional kwa kila kitu. Ninazo sababu nyingi sana ninapoamua kufanya jambo lakini kikubwa zaidi huwa sifati mkumbo na ushabaki, umri wa kufanya hayo ushanipita mbali. Samahani kama ntakuwa nimekukwaza
 
Serikali ya ccm haikuleta earthquake, ,,jichangeni wahaya msaidie ndugu zenu,,,,na Kura zenu 2020 mtupe kwa lazima Rweye
 
Back
Top Bottom