John Tendwa, msajili wa vyama vya siasa aliyeamua kujigeuza kuwa mwanasiasa twaomba kauli yako juu ya gharama za uchaguzi mdogo ujao wa jimbo la Arusha Mjini, NCCR Mageuzi kilipomvua uanachama mbunge wao David Kafulila na CUF kumvua uanachama Mh Hamad Rashid ulijitokeza katika vyombo vya habari ukilaumu maamuzi halali ya vikao vya kamati kuu na baraza kuu la utendaji la vyama husika kwa kuchukua maamuzi ya kuwavua uanachama wabunge wao mtazamo wako ukiwa kwenye gharama za chaguzi za marudio, uliongea ukionesha na kufafanua jinsi uchaguzi mmoja unavyogharimu billions of money, kam Taifa tumetoka kuteketeza hela nyingi kwenye uchaguzi wa Arumeru Mashariki na sasa mahakama kuu kanda ya Arusha imetengua ushindi wa aliyekuwa mbunge wa Jimbo hilo Mh Lema. Sasa yatupasa kuingia kwenye uchaguzi ambao matokeo yake hata kabla ya kura kupigwa yeshajulikana haihitaji hata kumlika kwa tochi ili kuona ukweli huu, Huoni kuwa suala hili latupeleka katika gharama zisizo za lazima na nchi inakabiliwa na ukata wa fedha? Au hili ni gumu kujitokeza tena hadharani kulizungumzia maana lina faida kwako? Wazee wa kimeru walikuagiza umwambie Lema asifike Arumeru , je katika uchaguzi mdogo wa Arusha Mjini unadhani wazee watakupa ujumbe gani wa kuufikisha kwa Bw Lema? Asiwe mgombea ama? Nasubiri kusikia toka kwako ili kuniprove me wrong kwamba weye hauko fair & free katika utendaji wako kama Msajili wa vyama vya siasa.