TEMESA, kazi ya vivuko Kigamboni imewashinda?

mkadiriajimajenzi

JF-Expert Member
Dec 31, 2015
549
608
Katika hali isiyo ya kawaida, majira haya ya saa tatu na nusu usiku huu kivuko cha magari na abiria cha MV Magogoni kimeshindwa kuanza safari kutoka upande wa Magogoni kwenda Kigamboni na kusababisha taharuki kubwa kwa abiria waliokua tayari wameshaingia kwa ajili ya kuanza safari.

Ikumbukwe kwamba vivuko hivi vibovu vya TEMESA vimekua vikilalalamikiwa sana na wasafiri kwa miaka mingi sasa bila mafanikio yoyote.

Nachukua fursa hii kuiomba Serikali itazame upya suala la uendeshaji wa vivuko hivi kwa maana TEMESA maji yameshawafika shingoni.

IMG_0283.jpg

IMG_0282.jpg
 
Hivyo vivuko ni vya umma sio kipaumbele,kipaumbele ni posho na vieite za watawala.
 
Alokuruhusu upige picha kivuko ni Nani? Jisalimishe b4 hatujakukamata
 
Wanawatesa wananchi wa Kigamboni.
Mbona hapo wanaweza kuwekeza tu hata hivyo vivuko vingine vikiwepo?
Walete vivuko vingine vizuri Nauli wafanye hata 1000 wananchi watavuka tu.
Kuliko Nauli iwe 200, pamoja na Shida ya kusubiri hapo Saa zima.
Tatizo limeendelea kwa Muda mrefu haieleweki nia yao ni nini.
 
Sehemu zote za kukaa dar mtu anaenda kukaa kigamboni wengine wanajiona kama wapo Dubai na zanzibar vile wanavyoringa sehemu nyingine ni za utalii sio za makazi siku nyingine upite na tuangoma ili usijaze server za jf
 
kama unakaa kigamboni jitahidi uwe na gari na ukitoka mishe zako usiwe na haraka kula poz sehem mpka sa moja kamata njia ya darajan vuka nenda kwako maisha simple tu
 
Back
Top Bottom