Wahenga walipata kunena kwamba KIMYA KINGI, HUWA KINA MSHINDO MKUU.....Watanzania makini hawapaswi kuhangaishwa na mtu mwenye uroho wa madaraka kiasi cha kutumia gharama kubwa kuyanunua madaraka bali tunatakiwa tutumie busara ndogo kujIuliza, je kwanini huyu mtu amekuwa na munkari na uongozi kiasi kwamba cha kuwa tayari kufanya lolote hata kama ni la kuvunja kanuni na taratibu za chama chake ili aupate uongozi..??,....Huruma hii kwa WATANZANIA wanaoshindia mlo mmoja ameitoa wapi....??...Kwanini anaonekana kuwa ni mwenye haraka na papara na uongozi....??....Nini kimejificha ndani ya dhamira yake juu ya taifa hili...??...WATANZANIA tuzifungue fikra zetu ili tuweze kuyachanganua mambo katika uhalisia wake....Tusizubaishwe na purukushani za wanasiasa walaghai...ule wakati tuliokuwa sote tukiusubiria kwa hamu na shauku hatimaye umewadia...tuliyavumilia mateso na manyanyaso kwa kipindi cha miaka mitano tukiamini kuwa siku moja yatakwisha...tukiamini kuwa hakuna marefu yasiyofika tamati...na hatimaye wakati umefika wa kufanya maamuzi sahihi ili yale mateso yaliyopita ya miaka mitano yawe historia...Hatupaswi kuyarudia makosa..Tukumbuke kuwa mustakabali wetu na watoto wetu kwa kipindi cha miaka mitano ijayo kinaanza na maamuzi ya leo.....Maamuzi yoyote mabovu yatapelekea majuto kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.....Tusisahau kuwa kiongozi makini hapimwi kwa sahani za pilau atakazo tugawia kipindi cha kampeni na wala si kwa vipande vya khanga wala fulana bali kwa sera zake makini na mipango inayotekelezeka....Tunapaswa kuchagua kiongozi ambaye hatatufanya tuyajutie maamuzi yetu huko mbele ya safari...tunapaswa kuchagua kiongozi au viongozi ambao tutajivunia kuwa nao kwenye safari yetu ya huko tunapopataka kwenda....Tunahitaji kiongozi au viongozi watakaotufanya tujutie kuwa ni kwanini hatukuwachagua mapema...Tunataka viongozi ambao watatusahaulisha mateso yaliopita na sio kutukumbusha mateso yaliyopita....Tunataka viongozi ambao hatutaona haya kuwakosoa pindi watakapo toka nje ya mstari....hatutaki viongozi waliojawa na viburi pindi waambiwapo ukweli au kukosolewa....Tunataka viongozi watakaolifanya taifa likimbie kimaendeleo na sio kuchechemea kimaendeleo.....Tunataka viongozi watakaotuunganisha WATANZANIA na sio kutugawa WATANZANIA.....Tunataka viongozi watakafanya maamuzi ya kitaifa kwa manufaa ya taifa na sio kwa manufaa ya familia zao na wapambe wao...Tunataka kiongozi mwenye uchungu na MATATIZO YETU na sio kiongozi atakayetumia matatizo yetu kama mtaji wa kujitajirisha yeye na vibaraka wake.....Tunahitaji kiongozi atakayetupa mikakati yenye kueleweka ya kulikwamua taifa letu.........lakini yote haya yanategemea sana maamuzi yetu ya leo........MUNGU IBARIKI TANZANIA