Team Lowassa - Ushauri

Team Lowassa - Ushauri

Captain-Chui

Member
Joined
Dec 11, 2014
Posts
80
Reaction score
49
TEAM Lowassa kweli mna nguvu kubwa kisiasa nchini, na mna wafuasi wengi. LAKINI msije mkajiachia hiyo nguvu yenu ikawalewesha mkafikiria mmeiweka CCM mfukoni. Pamoja na nguvu yake na marafiki zake na wafuasi wake mkumbuke LOWASSA sio CCM. Kwa sasa Team Lowassa bado mmelewa mnafikiri Lowassa ndio CCM. Walio nje ya Team Lowassa wameshaona dalili kwamba CCM haiwezi kumchagua Lowassa, na upinzani haitamkubali Lowassa.

USHAURI:
Team Lowassa fungueni macho muone dalili mpime mwelekeo wa upepo. Jiwekeni tayari kuweka mikakati ya kuhama CCM na kufungua chama kipya. Sasa hivi Team Lowassa mna nguvu ya kuleta mapinduzi ya kisiasa nchini kwa maana mna wafuasi wa kutosha. Jaribu kutafakari ushindani wa kisiasa utakavyokuwa mkali nchini kama kukiwa na Chama cha CCM, CHADEMA, na Chama cha TEAM LOWASSA, na vyama vingine. Huu ndio utakuwa mwanzo wa demokrasia ya kweli.
 
Yaan Lowasa ahame CCM?! Si watafilisika hao watu!
 
Kuna mtu ambaye yuko Team Lowasa anasema wao tatizo lililobaki ni kizingiti pekee ni kamati kuu ya CCM.Lakini anasema wamejiandaa vema kuruka hicho kiuzi.
Hivi kamati kuu wajumbe ni:
JK - Mwenyekiti
Kinana - Katibu
Mangula - Mjumbe
Pinda - ;
Makinda ;

Naomba tusaidiane ili tujue nani anaweza kununulika na-nani hawezi.
 
it sound rubbish lakini ipo siku itatokea mkuu tena inaweza kuwa mwezi wa tisa 2015
 
Ushauri wako mzuri sana na, tunashukuru. Ila tutabaki CCM na tutaingia kwenye kinyang'anyiro na CCM. Tunashukuru kwa ushauri.
 
Ccm ngoma bado mbichi, ukizubaa umeachwa feri! Mtoto hatumwi dukani. Yaani kwenye huu mchakato wa kumpitisha mgombea wakipita salama basi kweli watakuwa ni manyang'au yaliyo kubuhu
 
Mleta Uzi uko sahihi,ILA kama mwenyekiti wao wa chama kaamuwa chama kimfie mikononi sasa,ye mwenyewe apime upepo angalie Ni lipi afadhali kwake,lowassa Ni manowari ya kivita
 
TEAM Lowassa kweli mna nguvu kubwa kisiasa nchini, na mna wafuasi wengi. LAKINI msije mkajiachia hiyo nguvu yenu ikawalewesha mkafikiria mmeiweka CCM mfukoni. Pamoja na nguvu yake na marafiki zake na wafuasi wake mkumbuke LOWASSA sio CCM. Kwa sasa Team Lowassa bado mmelewa mnafikiri Lowassa ndio CCM. Walio nje ya Team Lowassa wameshaona dalili kwamba CCM haiwezi kumchagua Lowassa, na upinzani haitamkubali Lowassa.
.
Tanzania kuna watu wa ajabu ajabu wengi tu.
Wapo wanaojitokeza na kung'ang'ania mambo huku wakielewa kabisa hakuna mafanikio mwishoni.
Mwaka 2005, Mzee Malecela aling'ang'ania kugombea Urais mpaka akajiita "embe bivu' huku CCM WENYEWE wakijua yeye ni "embe bovu" na matokeo yake mliyaona.
Ushauri wangu kwa Team EL: Endeleeni kula bata kwa mfuko wake huyo kamanda wenu, kwani akiukosa huo Urais, hatakuwa tayari kuwafadhi na kuwahisani tena. Imbeni sana sifa zake usiku na mchana na mwisho wa siku, endeleeni na atakayeteuliwa rasmi! Mjini hapa!
 
Tushajipanga tayari kwa lolote. CCM ni sawa tu na baba na mama ambapo ukifikia hatua ya kujitegemea unakaa pembeni na mambo yanaendelea kama kawaida. Hatuwezi kuruhusu kikundi tulichokipa dhamana kutuandalia raisi dhaifu kama membe huku tukishuhudia kijana mdogo mwenye malezi ya "baba chovya ugali usisahau na kuchukua nyama" (ndanda kojanga osola nenyama) kama Makonda kumtukana mtu mwenye umri wa baba yake. Lowassa kinachosumbua ni nguvu na kuwa na wafuasi wengi kote Tanzania hali iliyosababisha wapinzani wake kumulika tochi zao zote kwa Lowassa. Mimi nashangaa sana kwani hivi karibuni wana CCM wengi tu wametangaza nia lakini wala hatujasikia wakikemewa! Mie nasema awamu hii hatuangilii uzuri wa bendera isipokuwa mtu.
 
tushajipanga tayari kwa lolote. Ccm ni sawa tu na baba na mama ambapo ukifikia hatua ya kujitegemea unakaa pembeni na mambo yanaendelea kama kawaida. Hatuwezi kuruhusu kikundi tulichokipa dhamana kutuandalia raisi dhaifu kama membe huku tukishuhudia kijana mdogo mwenye malezi ya "baba chovya ugali usisahau na kuchukua nyama" (ndanda kojanga osola nenyama) kama makonda kumtukana mtu mwenye umri wa baba yake. Lowassa kinachosumbua ni nguvu na kuwa na wafuasi wengi kote tanzania hali iliyosababisha wapinzani wake kumulika tochi zao zote kwa lowassa. Mimi nashangaa sana kwani hivi karibuni wana ccm wengi tu wametangaza nia lakini wala hatujasikia wakikemewa! Mie nasema awamu hii hatuangilii uzuri wa bendera isipokuwa mtu.
ngoma inogile
 
Ukoo wa panya tuu.. team buku sijui ngapi tokaka kwa jemedari fisadi
 
Mtajinyeaaa sana kabla ya kujambaaaaaaaaa
Lowassa oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.....
 
Back
Top Bottom