Paspii0
JF-Expert Member
- Apr 10, 2020
- 638
- 1,038
Napenda kuchukua dakika chache, kabla hamjaruka tena kwenda "self-care vacation" Zanzibar, kuwaeleza maneno machache yenye uzito wa mawe ya Mbudya kisiwani na utani wa nyanya wa Tandale.
Tumejua mnaendelea kukataa ndoa kwa visingizio vya;
Ndoa ni agano, si deal la Netflix la mwezi mmoja. Kuingia kwenye ndoa ukiwa na mtazamo wa "Try & Error" ni kama kuingia baharini ukiwa umevaa slippers.
Efeso 5:25 inasema “Enyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa...”
Je wewe unaweza kufa kwa mtu unayemfollow Instagram au tik-tok tu?,Kama huwezi, usioe bado.
Kutoa mahari si kununua mke bali ni kuonyesha thamani.
Kama unaona mahari ni gharama, tafakari,Kwa nini unanunua iPhone 16 pro kwa milioni tatu lakini unasema mwanamke hapaswi kupewa ng'ombe wawili?
Thamani haipimwi kwa bei , lakini bei inaonyesha uamuzi wa moyo.
Kama huwezi toa ng’ombe, toa moyo wa kweli ,lakini usitoe ahadi kama siasa za uchaguzi.
Enyi Wake, watiini waume zenu ,lakini si kama mpo katika kambi ya Jeshi.
Kutii ni tunda la upendo , si kiapo cha mateka. Mungu hajasema mke awe remote controlled, bali awe msaidizi na si kama remote ya king’amuzi cha tv.
Mke si ‘second-class citizen,’ ni mshirika wa kwanza katika agano.
Itaedelea…………………….
Tumejua mnaendelea kukataa ndoa kwa visingizio vya;
- Wanaume wote ni mbwa 🙄
- Wanawake wa siku hizi wanapenda pochi sana kuliko mapenzi.
- Mimi ni single ila mingle.
- Nataka nipate PhD kwanza.
- Ndoa ni kifungo cha maisha.
- Mimi ni feminist,alpha lone wolf. A.K.A msimbe
Ndoa ni agano, si deal la Netflix la mwezi mmoja. Kuingia kwenye ndoa ukiwa na mtazamo wa "Try & Error" ni kama kuingia baharini ukiwa umevaa slippers.
Efeso 5:25 inasema “Enyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa...”
Je wewe unaweza kufa kwa mtu unayemfollow Instagram au tik-tok tu?,Kama huwezi, usioe bado.
Kutoa mahari si kununua mke bali ni kuonyesha thamani.
Kama unaona mahari ni gharama, tafakari,Kwa nini unanunua iPhone 16 pro kwa milioni tatu lakini unasema mwanamke hapaswi kupewa ng'ombe wawili?
Thamani haipimwi kwa bei , lakini bei inaonyesha uamuzi wa moyo.
Kama huwezi toa ng’ombe, toa moyo wa kweli ,lakini usitoe ahadi kama siasa za uchaguzi.
Enyi Wake, watiini waume zenu ,lakini si kama mpo katika kambi ya Jeshi.
Kutii ni tunda la upendo , si kiapo cha mateka. Mungu hajasema mke awe remote controlled, bali awe msaidizi na si kama remote ya king’amuzi cha tv.
Mke si ‘second-class citizen,’ ni mshirika wa kwanza katika agano.
Itaedelea…………………….