TCU yaanza kuwatoza ada ya Sh. 20,000 wanafunzi

KaziIendelee

JF-Expert Member
Oct 30, 2013
327
229
Kuhusu kuanzisha tozo la Tsh 20,000/= kwa kila Mwanafunzi wa Chuo Kikuu.

Serikali inapaswa kuingilia kati suala la tozo iliyoanzishwa na Tume ya vyuo vikuu nchini, kiasi cha Tsh 20,000/= kwa kila mwanafunzi nchini.

TCU imeanzisha tozo hili kwa wanafunzi Wa vyuo vikuu kinyume na regulation ya 14 (1) (d) ya "Universities (General) Regulations, G.N.No.226" ya mwaka 2013 ambayo inakitaka chuo kilipie "prescribed annual commission fee" kwa kila mwanafunzi aliyedahiliwa kwenye chuo husika. Jambo hili limepelekea wanafunzi kutoendelea kujisajili katika vyuo vikuu vingi nchini kwasababu tozo la TCU Tsh 20,000/= kwa kila mwanafunzi limeanzishwa bila kufuata utaratibu Wa kisheria.

Pia sheria ambayo TCU wameitumia, wameitafsiri vibaya kwa kuwataka wanafunzi walipe tozo hilo na isiwe chuo kama utaratibu ulivyokuwa kipindi cha nyuma.


Pia wanasheria tuwasaidie wanafunzi wanaoonewa nchini kwa kulazimishwa kulipa tozo hilo. Tusome "Regulation" ambayo TCU wameitumia katika Public Notice yao kupitia website yao Home - Tanzania Commission for Universities ili tuwasaidie wanafunzi na hata baadhi ya uongozi wa vyuo kupata tafsiri sahihi ya nani anapaswa kulipia hiyo pesa.

Pia Mhe. Rais JPM, suala hili linagusa tabaka ambalo ulikuwa unalilia sana liweze kutimiza ndoto zao za kielimu lakini usajili umeshasimama katika vyuo vingi nchini kwasababu wanafunzi wamekataa kulipa tozo hilo; ni wakati sasa, baada ya kulijua hili, pamoja na viongozi wengine MULITOLEE MAAMUZI, VIJANA TULIOWATUMA WAKASOME WANATESEKA MNO NA HILI SUALA. Kwani kwa namna nyingine lilipaswa kufahamiawa na bodi ya mikopo ili kiasi kitoke board halafu wanafunzi walipie, unfortunately haipo hivyo.


Serikali iingilie kati jambo hili ili lisije likasababisha mgogoro kati ya wanafunzi na uongozi Wa vyuo kuwa mkubwa nchini
 
Umesikika. Binafsi nimekerwa sana na taarifa hii. Hawa TCU wanaibuka tu na kuwakandamiza wanafunzi. Hivi zile direct costs wanazolipa wanafunzi kwa vyuo zinafanya kazi gani? Kwa nini hiyo tozo isitokane na fedha hizo ambazo wanafunzi wanalipa na hawajui zinafanya kazi gani? Then mwanafunzi anapodahiliwa kupitia TCU, analipa kiasi cha shilingi 50,000. Tena mbaya zaidi kiwango hicho hakirejeshwi hata kama haujapata chuo. Huu ni uonevu wa hali ya juu sana. Ina maana elfu hamsini hazitoshi mpaka wanaanzisha gharama nyingine?
 
Nauliza hivi, je tozo hiyo ipo kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza tu ama wanafunzi wote? Kama ndo hivyo, ni kiasi gani TCU wanavuna na je fedha hizo zinafanya kazi gani?
 
Hakuna anayelia bali huu ni ufisadi uliopigiwa kelele na Mheshimiwa Rais Magufuli

Hiv ww una mtindio wa ubongo nn ??? Hiyo ni mipango ya serekali inayongozwa na Makufuli...na kwa makufuli kamalikuwa hamjui ..ameondoa ada ya shule ya msingi had sekondari tu wengine ......tutaisoma namba ..na namba ndiyo hiyooi....HAPA KAZI TU.. hutaki baki kwenu
 
Nauliza hivi, je tozo hiyo ipo kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza tu ama wanafunzi wote? Kama ndo hivyo, ni kiasi gani TCU wanavuna na je fedha hizo zinafanya kazi gani?

hapo KAZI TU ha ha ha mtaisoma namba na bado mlichagua wenyewea
 
Unalalamika nini! Hii si ni sera yetu ya Hapa Kazi tu. Kazi bila pesa wewe umeona wapi?
 
Asante tcu..karo tu wengine hawajalipa sembuse iyooo.. Shkamoo serikali
 
Hahaaa.....HAPA KAZI TU....mnalia nn...?? Mlikataa elimu ya bure

We ungekuwa ushawai hata kulipa ada ya chekechea kwa pesa yako hata usingesema hayo..... Pesa bila kujua inaenda kufanya kazi gani ya msingi kwa mtoaji inauma bwana, hata kama ni buku.
Suala la kutokea hizo gharama halina uhusiano na elimu bure..... Kwani ina uhusiano na ada iyo...
 
Back
Top Bottom