Tcu na heslb wanawatakia nini watanzania.

taffu69

JF-Expert Member
Feb 26, 2007
2,094
538
Nimekuwa nikifuatilia utaratibu unaotumiwa na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) katika kudahili wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo vya elimu ya juu na pia utaratibu unaotumiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwa wanaoomba mikopo kwa ajili ya masomo kwa ngazi ya elimu ya juu ambao unatia shaka kwa kiasi kikubwa.

Nakubaliana na ukweli kuwa kutokana na mabadiliko ya mifumo pamoja na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, ni vyema mambo mengi yakafanywa kwa kutumia teknolojia ya kisasa kama vile kudahili wanafunzi kwa kutumia mtandao wa internet na pia kutumia mfumo huo katika kuomba mikopo. Jambo linalotatiza ni kwa jinsi gani mfumo huo wa mawasiliano ulivyosambaa nchini na namna wale wanaotaka kudahiliwa wanaweza kupata huduma hiyo kwa muda unaotakiwa. Mathalani kijana ambaye yuko Nkasi, Ngara, Nanyumbu, Kibondo, Mugumu, Loliondo na kwingineko atakavyoweza kupata huduma ya mtandao wa internet akiwa kwenye maeneo hayo pasipo kulazimika kusafiri umbali mrefu kama sio kwenda Dar Es Salaam kufuata huduma hiyo tena kwa gharama kubwa.

Mbali na hilo, hata mfumo wa kulipia ada stahili kwa ajili ya kupata fomu zinazotakiwa unatia mashaka na unaleta usumbufu mkubwa pia. Mfano, TCU wanataka kabla ya kufanya jambo lolote ulipe ada ya udahili kiasi cha shilingi 30,000 lakini ili uweze kulipa ada hiyo unalazimika kwenda kwenye tawi la benki ya NBC ili uweze kununua kadi itakayokuwezesha kujisajili kwenye mtandao wa taasisi hiyo. Nao HESLB wanataka kabla ya kupata fursa ya kuingia kwenye mtandao wao kwa ajili ya kupata fomu za mkopo ulipe ada ya shilingi 30,000 kupitia M-PESA.

Hoja ninayotaka kutoa hapa ni kwa nini taasisi hizi zimekuwa na ufinyu wa kufikiri katika kupanga namna ya kushughulikia mambo haya kwa upana zaidi ikizingatiwa kuwa zinaendeshwa na watu wasomi na wanaojua mazingira halisi wanayoishi Watanzania. Mfano badala ya kulazimisha kufanya udahili kwa kupitia mtandao wa internet pekee wangetoa fursa kwa wale ambao hawana nafasi ya kupata mtandao wa internet kupata fomu hizo kwa ajili ya kuzijaza kama ilivyokuwa inafanyika awali. Aidha, mfumo wa kulipia ada stahili nao ungehuishwa kwa kutoa fursa ya kulipia kupitia mfumo ama taasisi nyingine badala ya kutegemea taasisi moja pekee. Mfano, benki ya NBC matawi yake yako mijini zaidi ukilinganisha na benki ya NMB ambayo matawi yake yamesambaa hadi vijijini hivyo ingekuwepo benki mbadala kwa ajili ya ya kufanya malipo ya ada husika. Hivyo hivyo kwa upande wa malipo yanayofanywa kupitia M-PESA ni wazi kuwa sio watu wote wamejisajili kupitia mfumo huo kwani kuna ambao wamejisajili kwenye TIGO PESA ama Airtel.

Mbali na hayo, hata utaratibu wa urejeshaji wa fomu za mikopo unaleta usumbufu mkubwa kwani unalazimisha mwombaji kurejesha fomu kwa njia ya EMS pekee bila kujali mhusika yuko eneo gani. Mfano, kwa mwombaji ambaye yuko Dar Es Salaam angeweza kurejesha fomu hizo moja kwa moja kwenye ofisi za HESLB pasipo kuzituma kwa njia ya EMS ama kwa wale ambao wako mikoani na hawawezi kupata huduma hiyo kwa urahisi wangeweza pia kutumia njia ya posta.

Ni vyema taasisi hizi zikaondokana na ukiritimba zinaoufanya kwa sasa kwani inaonesha wazi kuwa zinachangia katika kudumaza kasi ya ukuaji wa elimu na kupunguza ari ya vijana wetu katika kutafuta elimu. Aidha, ukiritimba huu unazifanya taasisi hizi kuonekana kufanya kazi kama mawakala wa makampuni/taasisi fulani kitu ambacho hakitoi picha nzuri kwa jamii ambayo kwayo taasisi hizi (TCU na HESLB) zinajiendesha kwa kutumia kodi ya Watanzania wote. Utaratibu unaotumiwa na taasisi hizi pia unaonekana kuwa unaleta ubaguzi kwani hauoneshi kuwajali watanzania wote kwa ujumla wao.
 
Mie nilitegemea bunge liitume kamati yake kuchunguza ufirahuni huu unaofanywa na tcu na heslb mpaka kupelekea maenezi ya vvu kwa ndugu zetu hawa,wakishaugua ni nani atawatibia ama itakuwa hasara ya nani?
 
Nimekuwa nikifuatilia utaratibu unaotumiwa na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) katika kudahili wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo vya elimu ya juu na pia utaratibu unaotumiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwa wanaoomba mikopo kwa ajili ya masomo kwa ngazi ya elimu ya juu ambao unatia shaka kwa kiasi kikubwa.

Nakubaliana na ukweli kuwa kutokana na mabadiliko ya mifumo pamoja na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, ni vyema mambo mengi yakafanywa kwa kutumia teknolojia ya kisasa kama vile kudahili wanafunzi kwa kutumia mtandao wa internet na pia kutumia mfumo huo katika kuomba mikopo. Jambo linalotatiza ni kwa jinsi gani mfumo huo wa mawasiliano ulivyosambaa nchini na namna wale wanaotaka kudahiliwa wanaweza kupata huduma hiyo kwa muda unaotakiwa. Mathalani kijana ambaye yuko Nkasi, Ngara, Nanyumbu, Kibondo, Mugumu, Loliondo na kwingineko atakavyoweza kupata huduma ya mtandao wa internet akiwa kwenye maeneo hayo pasipo kulazimika kusafiri umbali mrefu kama sio kwenda Dar Es Salaam kufuata huduma hiyo tena kwa gharama kubwa.

Mbali na hilo, hata mfumo wa kulipia ada stahili kwa ajili ya kupata fomu zinazotakiwa unatia mashaka na unaleta usumbufu mkubwa pia. Mfano, TCU wanataka kabla ya kufanya jambo lolote ulipe ada ya udahili kiasi cha shilingi 30,000 lakini ili uweze kulipa ada hiyo unalazimika kwenda kwenye tawi la benki ya NBC ili uweze kununua kadi itakayokuwezesha kujisajili kwenye mtandao wa taasisi hiyo. Nao HESLB wanataka kabla ya kupata fursa ya kuingia kwenye mtandao wao kwa ajili ya kupata fomu za mkopo ulipe ada ya shilingi 30,000 kupitia M-PESA.

Hoja ninayotaka kutoa hapa ni kwa nini taasisi hizi zimekuwa na ufinyu wa kufikiri katika kupanga namna ya kushughulikia mambo haya kwa upana zaidi ikizingatiwa kuwa zinaendeshwa na watu wasomi na wanaojua mazingira halisi wanayoishi Watanzania. Mfano badala ya kulazimisha kufanya udahili kwa kupitia mtandao wa internet pekee wangetoa fursa kwa wale ambao hawana nafasi ya kupata mtandao wa internet kupata fomu hizo kwa ajili ya kuzijaza kama ilivyokuwa inafanyika awali. Aidha, mfumo wa kulipia ada stahili nao ungehuishwa kwa kutoa fursa ya kulipia kupitia mfumo ama taasisi nyingine badala ya kutegemea taasisi moja pekee. Mfano, benki ya NBC matawi yake yako mijini zaidi ukilinganisha na benki ya NMB ambayo matawi yake yamesambaa hadi vijijini hivyo ingekuwepo benki mbadala kwa ajili ya ya kufanya malipo ya ada husika. Hivyo hivyo kwa upande wa malipo yanayofanywa kupitia M-PESA ni wazi kuwa sio watu wote wamejisajili kupitia mfumo huo kwani kuna ambao wamejisajili kwenye TIGO PESA ama Airtel.

Mbali na hayo, hata utaratibu wa urejeshaji wa fomu za mikopo unaleta usumbufu mkubwa kwani unalazimisha mwombaji kurejesha fomu kwa njia ya EMS pekee bila kujali mhusika yuko eneo gani. Mfano, kwa mwombaji ambaye yuko Dar Es Salaam angeweza kurejesha fomu hizo moja kwa moja kwenye ofisi za HESLB pasipo kuzituma kwa njia ya EMS ama kwa wale ambao wako mikoani na hawawezi kupata huduma hiyo kwa urahisi wangeweza pia kutumia njia ya posta.

Ni vyema taasisi hizi zikaondokana na ukiritimba zinaoufanya kwa sasa kwani inaonesha wazi kuwa zinachangia katika kudumaza kasi ya ukuaji wa elimu na kupunguza ari ya vijana wetu katika kutafuta elimu. Aidha, ukiritimba huu unazifanya taasisi hizi kuonekana kufanya kazi kama mawakala wa makampuni/taasisi fulani kitu ambacho hakitoi picha nzuri kwa jamii ambayo kwayo taasisi hizi (TCU na HESLB) zinajiendesha kwa kutumia kodi ya Watanzania wote. Utaratibu unaotumiwa na taasisi hizi pia unaonekana kuwa unaleta ubaguzi kwani hauoneshi kuwajali watanzania wote kwa ujumla wao.

Hakuna huduma itolewayo bure duniani hata kama inatolewa na serikali, maana kwa kulipa kodi peke yake inatosha kudai kuwa umelipia huduma husika ila kwa ishu ya TCU wazee fikirieni ikiwezekana mfumo huu wa kulipia 30,000 na unapewa nafasi ya kuomba kozi nane ufe ili kila mwombaji akanunue fomu chuoni ajaze kivyake na chuo husika ndio kimdahili, hapo hujahesabu nauli chakula na malazi bado photocopi za vyeti na ujinga mwingine mwiingi tulioupitia sisi tuliojidahili kwa njia ya fomu. Mfumo wa CAS umeweza kudahili watu kwa usawa kwani hata mwenye 30,000 tuu ataapply vyuo vingi hivyo kuongeza uwezekano wa kupata chuo tofauti na angenunua fomu moja kwa 30,000 chuo kimoja tuu kama ilivyokuwa hapo awali.

Gazeti la Majira la leo tareh 24 linailaumu TCU kwa kudahili wanafunzi wengi wakati serikali inauwezo mdogo wa kuwalipia wote mkopo, hivyo wanashauri ni bora TCU ingedahili wachache ambao serikali inauwezo wa kuwapa mikopo woote, hamuoni kuwa huu ndio utakuwa ni UBAGIZI WA HALI YA JUU?
 
Kama kuna ambae anaona huu mfumo wa tcu wa kudahili wanafunzi haufai,bac ahame nchi.over
 
Hakuna huduma itolewayo bure duniani hata kama inatolewa na serikali, maana kwa kulipa kodi peke yake inatosha kudai kuwa umelipia huduma husika ila kwa ishu ya TCU wazee fikirieni ikiwezekana mfumo huu wa kulipia 30,000 na unapewa nafasi ya kuomba kozi nane ufe ili kila mwombaji akanunue fomu chuoni ajaze kivyake na chuo husika ndio kimdahili, hapo hujahesabu nauli chakula na malazi bado photocopi za vyeti na ujinga mwingine mwiingi tulioupitia sisi tuliojidahili kwa njia ya fomu. Mfumo wa CAS umeweza kudahili watu kwa usawa kwani hata mwenye 30,000 tuu ataapply vyuo vingi hivyo kuongeza uwezekano wa kupata chuo tofauti na angenunua fomu moja kwa 30,000 chuo kimoja tuu kama ilivyokuwa hapo awali.

Gazeti la Majira la leo tareh 24 linailaumu TCU kwa kudahili wanafunzi wengi wakati serikali inauwezo mdogo wa kuwalipia wote mkopo, hivyo wanashauri ni bora TCU ingedahili wachache ambao serikali inauwezo wa kuwapa mikopo woote, hamuoni kuwa huu ndio utakuwa ni UBAGIZI WA HALI YA JUU?

Hapa sijaghusia suala la gharama ila utaratibu unaotumika na mazingira ya jumla ya nchi yetu.
 
watu wanaweza kuchangia 10m arusi moja...ila kuchagia elimu ya juu.. eti kila siku ni serikali tu!!!!
 
Sidhani kama ni mbayaa sana sema. Waalioko mbali na teknolojia hii nda wanapata tabu mfumo wa kulipia ilipaswa iwe Nmb then M-pesa,Tigo pesa,Airtel money na hata Easy pesa coz. Kila binadamu anaushabiki wake wao kama Tcu wangeweka mfumo wa kukubalianaa na malipo ya Makampuni yote haya note kama inatumika moja M-pesa means kuna ushabiki wa kibiashara ndani yake THANKS
 
Back
Top Bottom