taffu69
JF-Expert Member
- Feb 26, 2007
- 2,094
- 538
Nimekuwa nikifuatilia utaratibu unaotumiwa na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) katika kudahili wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo vya elimu ya juu na pia utaratibu unaotumiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwa wanaoomba mikopo kwa ajili ya masomo kwa ngazi ya elimu ya juu ambao unatia shaka kwa kiasi kikubwa.
Nakubaliana na ukweli kuwa kutokana na mabadiliko ya mifumo pamoja na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, ni vyema mambo mengi yakafanywa kwa kutumia teknolojia ya kisasa kama vile kudahili wanafunzi kwa kutumia mtandao wa internet na pia kutumia mfumo huo katika kuomba mikopo. Jambo linalotatiza ni kwa jinsi gani mfumo huo wa mawasiliano ulivyosambaa nchini na namna wale wanaotaka kudahiliwa wanaweza kupata huduma hiyo kwa muda unaotakiwa. Mathalani kijana ambaye yuko Nkasi, Ngara, Nanyumbu, Kibondo, Mugumu, Loliondo na kwingineko atakavyoweza kupata huduma ya mtandao wa internet akiwa kwenye maeneo hayo pasipo kulazimika kusafiri umbali mrefu kama sio kwenda Dar Es Salaam kufuata huduma hiyo tena kwa gharama kubwa.
Mbali na hilo, hata mfumo wa kulipia ada stahili kwa ajili ya kupata fomu zinazotakiwa unatia mashaka na unaleta usumbufu mkubwa pia. Mfano, TCU wanataka kabla ya kufanya jambo lolote ulipe ada ya udahili kiasi cha shilingi 30,000 lakini ili uweze kulipa ada hiyo unalazimika kwenda kwenye tawi la benki ya NBC ili uweze kununua kadi itakayokuwezesha kujisajili kwenye mtandao wa taasisi hiyo. Nao HESLB wanataka kabla ya kupata fursa ya kuingia kwenye mtandao wao kwa ajili ya kupata fomu za mkopo ulipe ada ya shilingi 30,000 kupitia M-PESA.
Hoja ninayotaka kutoa hapa ni kwa nini taasisi hizi zimekuwa na ufinyu wa kufikiri katika kupanga namna ya kushughulikia mambo haya kwa upana zaidi ikizingatiwa kuwa zinaendeshwa na watu wasomi na wanaojua mazingira halisi wanayoishi Watanzania. Mfano badala ya kulazimisha kufanya udahili kwa kupitia mtandao wa internet pekee wangetoa fursa kwa wale ambao hawana nafasi ya kupata mtandao wa internet kupata fomu hizo kwa ajili ya kuzijaza kama ilivyokuwa inafanyika awali. Aidha, mfumo wa kulipia ada stahili nao ungehuishwa kwa kutoa fursa ya kulipia kupitia mfumo ama taasisi nyingine badala ya kutegemea taasisi moja pekee. Mfano, benki ya NBC matawi yake yako mijini zaidi ukilinganisha na benki ya NMB ambayo matawi yake yamesambaa hadi vijijini hivyo ingekuwepo benki mbadala kwa ajili ya ya kufanya malipo ya ada husika. Hivyo hivyo kwa upande wa malipo yanayofanywa kupitia M-PESA ni wazi kuwa sio watu wote wamejisajili kupitia mfumo huo kwani kuna ambao wamejisajili kwenye TIGO PESA ama Airtel.
Mbali na hayo, hata utaratibu wa urejeshaji wa fomu za mikopo unaleta usumbufu mkubwa kwani unalazimisha mwombaji kurejesha fomu kwa njia ya EMS pekee bila kujali mhusika yuko eneo gani. Mfano, kwa mwombaji ambaye yuko Dar Es Salaam angeweza kurejesha fomu hizo moja kwa moja kwenye ofisi za HESLB pasipo kuzituma kwa njia ya EMS ama kwa wale ambao wako mikoani na hawawezi kupata huduma hiyo kwa urahisi wangeweza pia kutumia njia ya posta.
Ni vyema taasisi hizi zikaondokana na ukiritimba zinaoufanya kwa sasa kwani inaonesha wazi kuwa zinachangia katika kudumaza kasi ya ukuaji wa elimu na kupunguza ari ya vijana wetu katika kutafuta elimu. Aidha, ukiritimba huu unazifanya taasisi hizi kuonekana kufanya kazi kama mawakala wa makampuni/taasisi fulani kitu ambacho hakitoi picha nzuri kwa jamii ambayo kwayo taasisi hizi (TCU na HESLB) zinajiendesha kwa kutumia kodi ya Watanzania wote. Utaratibu unaotumiwa na taasisi hizi pia unaonekana kuwa unaleta ubaguzi kwani hauoneshi kuwajali watanzania wote kwa ujumla wao.
Nakubaliana na ukweli kuwa kutokana na mabadiliko ya mifumo pamoja na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, ni vyema mambo mengi yakafanywa kwa kutumia teknolojia ya kisasa kama vile kudahili wanafunzi kwa kutumia mtandao wa internet na pia kutumia mfumo huo katika kuomba mikopo. Jambo linalotatiza ni kwa jinsi gani mfumo huo wa mawasiliano ulivyosambaa nchini na namna wale wanaotaka kudahiliwa wanaweza kupata huduma hiyo kwa muda unaotakiwa. Mathalani kijana ambaye yuko Nkasi, Ngara, Nanyumbu, Kibondo, Mugumu, Loliondo na kwingineko atakavyoweza kupata huduma ya mtandao wa internet akiwa kwenye maeneo hayo pasipo kulazimika kusafiri umbali mrefu kama sio kwenda Dar Es Salaam kufuata huduma hiyo tena kwa gharama kubwa.
Mbali na hilo, hata mfumo wa kulipia ada stahili kwa ajili ya kupata fomu zinazotakiwa unatia mashaka na unaleta usumbufu mkubwa pia. Mfano, TCU wanataka kabla ya kufanya jambo lolote ulipe ada ya udahili kiasi cha shilingi 30,000 lakini ili uweze kulipa ada hiyo unalazimika kwenda kwenye tawi la benki ya NBC ili uweze kununua kadi itakayokuwezesha kujisajili kwenye mtandao wa taasisi hiyo. Nao HESLB wanataka kabla ya kupata fursa ya kuingia kwenye mtandao wao kwa ajili ya kupata fomu za mkopo ulipe ada ya shilingi 30,000 kupitia M-PESA.
Hoja ninayotaka kutoa hapa ni kwa nini taasisi hizi zimekuwa na ufinyu wa kufikiri katika kupanga namna ya kushughulikia mambo haya kwa upana zaidi ikizingatiwa kuwa zinaendeshwa na watu wasomi na wanaojua mazingira halisi wanayoishi Watanzania. Mfano badala ya kulazimisha kufanya udahili kwa kupitia mtandao wa internet pekee wangetoa fursa kwa wale ambao hawana nafasi ya kupata mtandao wa internet kupata fomu hizo kwa ajili ya kuzijaza kama ilivyokuwa inafanyika awali. Aidha, mfumo wa kulipia ada stahili nao ungehuishwa kwa kutoa fursa ya kulipia kupitia mfumo ama taasisi nyingine badala ya kutegemea taasisi moja pekee. Mfano, benki ya NBC matawi yake yako mijini zaidi ukilinganisha na benki ya NMB ambayo matawi yake yamesambaa hadi vijijini hivyo ingekuwepo benki mbadala kwa ajili ya ya kufanya malipo ya ada husika. Hivyo hivyo kwa upande wa malipo yanayofanywa kupitia M-PESA ni wazi kuwa sio watu wote wamejisajili kupitia mfumo huo kwani kuna ambao wamejisajili kwenye TIGO PESA ama Airtel.
Mbali na hayo, hata utaratibu wa urejeshaji wa fomu za mikopo unaleta usumbufu mkubwa kwani unalazimisha mwombaji kurejesha fomu kwa njia ya EMS pekee bila kujali mhusika yuko eneo gani. Mfano, kwa mwombaji ambaye yuko Dar Es Salaam angeweza kurejesha fomu hizo moja kwa moja kwenye ofisi za HESLB pasipo kuzituma kwa njia ya EMS ama kwa wale ambao wako mikoani na hawawezi kupata huduma hiyo kwa urahisi wangeweza pia kutumia njia ya posta.
Ni vyema taasisi hizi zikaondokana na ukiritimba zinaoufanya kwa sasa kwani inaonesha wazi kuwa zinachangia katika kudumaza kasi ya ukuaji wa elimu na kupunguza ari ya vijana wetu katika kutafuta elimu. Aidha, ukiritimba huu unazifanya taasisi hizi kuonekana kufanya kazi kama mawakala wa makampuni/taasisi fulani kitu ambacho hakitoi picha nzuri kwa jamii ambayo kwayo taasisi hizi (TCU na HESLB) zinajiendesha kwa kutumia kodi ya Watanzania wote. Utaratibu unaotumiwa na taasisi hizi pia unaonekana kuwa unaleta ubaguzi kwani hauoneshi kuwajali watanzania wote kwa ujumla wao.