TCRA tufafanulieni maana ya FTA

TCRA tufafanulieni maana ya FTA

ntamaholo

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
12,950
Reaction score
6,981
Hawa jamaa siwaelewi kabisa. Mimi nina ving'amuzi viwili, na vyote vimeunganishwa kwenye tv yangu.

Kinachoamua nilipie kipi, ni huduma nayohitaji kwa muda huo.

Nikihitaji mipira ya ndani, nalipia Azam.

Nikihitaji habari mbalimbali, nalipia startime.

Sasa swali langu ni FTA services. Hawa wanaojiita pay tv, yaani azam, wamegoma kuziingiA channel za itv, eatv, chanel 10, clouds, wasafi kwa kuwa zina leseni ya FTA. Channel pekee iliyopo huko ni ua matangazo channel 100, na tbc1 pekee. Na hapa sijalipia mwezi sasa, lkn tbc1 wapo hewani.

Ugomvi wangu leo ni startime, shirika.la serikali kwa asilimoa fulani. Leo nimaliza furushi lao, lkn cha kushangaza, channel pekee iliyobak, ni channel 099, ambayo ni matangazo yao tu.

Hata tbc1 ambayo ni FTA, haipo na wala zile FTA channel nazo hazipo, hivyo ni kama tumepigwa chenga.

Sasa FTA ni nini hasa?
 
Hawa jamaa siwaelewi kabisa. Mimi nina ving'amuzi viwili, na vyote vimeunganishwa kwenye tv yangu.

Kinachoamua nilipie kipi, ni huduma nayohitaji kwa muda huo.

Nikihitaji mipira ya ndani, nalipia Azam.

Nikihitaji habari mbalimbali, nalipia startime.

Sasa swali langu ni FTA services. Hawa wanaojiita pay tv, yaani azam, wamegoma kuziingiA channel za itv, eatv, chanel 10, clouds, wasafi kwa kuwa zina leseni ya FTA. Channel pekee iliyopo huko ni ua matangazo channel 100, na tbc1 pekee. Na hapa sijalipia mwezi sasa, lkn tbc1 wapo hewani.

Ugomvi wangu leo ni startime, shirika.la serikali kwa asilimoa fulani. Leo nimaliza furushi lao, lkn cha kushangaza, channel pekee iliyobak, ni channel 099, ambayo ni matangazo yao tu.

Hata tbc1 ambayo ni FTA, haipo na wala zile FTA channel nazo hazipo, hivyo ni kama tumepigwa chenga.

Sasa FTA ni nini hasa?
Mkuu Mtama, kwanza pole kwa yote, pili mimi japo sio TCRA, lakini nina ka mwanga kidogo.

Kuna aina tatu za Matangazo ya TV,
1. FTA ni Free on Air, TV zote za bure ndizo zinaonekana bure. Kwa Tanzania, TBC, ITV, Star TV, Channel Ten, ZBC, Capital TV, EA TV, Clouds TV, Etc ni za bure.
2. Cable TV or Pay TV, hizi ni TV za kulipia, Kwa Tanzania ni Azam TV, DSTV, Zuku, Sibuka, na TV kibao za Dini.
3. Online TV na VOD, hizi ni TV zinazo rusha contents on line nazo ni bure.

Kwa mujibu wa leseni zao, cable TV zote zinawajibu wa kurusha bure national wide FTA, ambayo ni TBC. Na haziruhusiwi kurusha FTA nyingine.

Kilichokuwa kinafanyika ni cable TV kama Azam, Zuku na DSTV wote walikuwa wanarusha FTA kwa kulipia.

TCRA, walipiga maarufuku Cable kuonyesha FTA, hivyo hata news ya Azam TV sasa ni online na VOD.

Ili kuendelea kupata FTA zote bure, ni lazima utumie
1. Kingamuzi cha Star Times ambacho kinarusha bure FTA zote za Tanzania.
2. Utumie satellite dish na receiver utaziona channels zote za bure na mi bure.
3. Utumie Smart TV ambayo inashika FTA zote na ni bure.

Tangu hili zoezi lianze, kiukweli kuna mikanganyiko mingi, ambapo TCRA inapaswa kutoa elimu zaidi.

P
 
Pole sana mkuu, mimi kingamuzi changu cha Startimes sijalipia muda mrefu kweli naangalia bure hizo channel wanazoziita FTA zinaonekana ITV, Startv, Channel 10 na EATV Ila wasafi na Clouds haziomeshi
 
Back
Top Bottom