TCRA, Mimi nina ombi moja tuu kwenu

TCRA, Mimi nina ombi moja tuu kwenu

Hazchem plate

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2011
Posts
11,059
Reaction score
15,532
Sisi watazamaji wa TV tunaomba local channels zirudishwe kwenye Ving'amuzi vyote. Kama tumeweza kununua Ving'amuzi hata kulipia Local channels tunaweza.

Sio kwa mateso haya.
 
Wasirudishe tu Mimi sijaona cha maana kwenye hizo local Chanel.

Bora walivyoondoa.😁
 
Hii nchi sasa hivi inaenda kama gari lililokatika senta bolti , LENGO LA YOTE HAYA NI KULAZIMISHA WANANCHI KUANGALIA TV ILIYOSHINDWA YA TBC , HATA HIVYO MPANGO WAO UMESHINDWA KABLA HAUJAANZA .
 
Uko sahihi mkuu maana hatujaacha kulipia ving'amuzi vyetu japo local channels hazimo. Wanaopinga hoja hii ni watangaza nia 2019/2020 kama sio wapambe.
 
Huwa nalipia Azam kifurushi cha elfu 23 kwa miezi mi3 mi3, juzi nimelipia tena. Wakae nazo loko chaneli zao! Hapa Naangalia Yanga v African Lyon! Jana nimeangalia Taifa Stars, pia SIMBA!
Elfu 23 kwa miezi 3??? Unalipiaje mkuu?
 
Huwa nalipia Azam kifurushi cha elfu 23 kwa miezi mi3 mi3, juzi nimelipia tena. Wakae nazo loko chaneli zao! Hapa Naangalia Yanga v African Lyon! Jana nimeangalia Taifa Stars, pia SIMBA!
Ngapi ngapi?
 
Back
Top Bottom