GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
TCRA pale Mawasiliano tower mmekodoa macho mnatazama tu na ninyi mnachekelea, nini athari za segment hii kauzu kuliko dagaa na matusi haya wanayoyaporomosha wasanii hawa wa ZE COMEDY wanaonekana kukosa kabisa ubunifu kwa sasa na kuamua kuwafundisha watoto matusi kwa nguvu.
Hili si la kusubiri mpaka wanasiasa waongee Bungeni, chukueni hatua mapema, meno na kucha mmepewa mpaka watu walalamike ndo mjue kuwa ni kosa, tumieni vema basi weledi wenu kunusuru kizazi cha watanzania hawa wasiokuwa na uchaguzi wa mambo wanaojifunza lugha hizi zilizopitiliza mipaka na maadili ya makuzi mema.
Hili si la kusubiri mpaka wanasiasa waongee Bungeni, chukueni hatua mapema, meno na kucha mmepewa mpaka watu walalamike ndo mjue kuwa ni kosa, tumieni vema basi weledi wenu kunusuru kizazi cha watanzania hawa wasiokuwa na uchaguzi wa mambo wanaojifunza lugha hizi zilizopitiliza mipaka na maadili ya makuzi mema.