TCRA CCC Mkowapi Tunaibiwa Bando za Internet?

TCRA CCC Mkowapi Tunaibiwa Bando za Internet?

Masulupwete

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
2,366
Reaction score
2,435
Unanunua bando la wiki nzima la kifurushi cha internet labda bando la shilingi 3,000 unapewa 400MB (kwa mtandao naotumia mimi).

1. Mosi, hilo bando uliloambiwa ni la wiki litadumu kwa siku 6 kamili, badala ya kudumu kwa siku 7. Wenzetu hawa sijui wiki ina siku 6, au hizi siku wao wanazihesabu kwa staili gani, sielewi.

2. Pili, ukishanunua hilo bando sasa, ndo mziki unaanza sasa. Wanazikatakata/gawanya hizo bando; kuna MB wanazipeleka watsap (bila kujali kama wewe unatumia hiyo watsap au hutumii), zingine fesibuku (hivohivo hawajali upo huko fesibuku au haupo), zinazobaki ndio unaingiziwa bando la kawaida la kutumia kwenye internet.

Matokeo yake unapata mb chache sana kwa ajili ya internet na unatumia kwa siku hizo 6 badala ya 7.

Huu ni uzulumati wa mchana kweupe. Hivi TCRA mnayaona haya au hadi tuje huko maofisini kwenu kupanga foleni kuwaelezea haya?

Nyinyi sio watumiaji wa huduma hizi hamuoni upuuzi huu unaofanywa kwa watumiaji au mnasubiri jpm awatumbue?
 
wanajua na wao ndo wanawapangia vifurushi huoni ww wote vifurushi vinafanana akianza voda kupunguza anafuata halo tigo airtel
 
Nchi zingine, internet ni bidhaa ya msingi na haki ya kila mwananchi!

Huku Tanganyika, internet ni kama anasa!

Mafisadi yananyakua fedha za walalahoi kama manyang'au!

Anyway, ndio nchi yetu hii, shithole!
 
Siku zinakuja kuendesha gharama za Simu itakuwa ni gharama kuliko kula broiler na chips

Siku zenyewe ndio hizi boss... mie hili ndio bundle langu la mwisho kutumia, baada ya hapa simu itakaa tu ndani, mwenye shida anioigie ... nimejikuta kwa wiki natumia zaidi ya 20,000... kuja kushtuka nikajionea huruma kabisaa
 
Halotel wana ile 1GB kwa 1000 wiki kwenye Halopesa lakini kinaisha siku 3 tu. Halotel nimeshaiogopa. Ni wezi balaa
Hapa kwa halotel utakuwa umedanganya,mm sijawahi kuona hiki,labda useme speed imepungua
 
Aisee
Screenshot_2019-08-05-09-13-41.jpeg
 
Hizo bundle unazonunua, ndio hizo hizo wanatumia kudukua mawasiliano yako, ndio maana unaona zinaisha haraka
 
Asante Sana mtoa mada! Kwakweli hali ni ngumu. Mitandao km voda na halotel ni hatari. Voda unaambia sh. 1000 unapata units 100 ukiongea nusu saa tu unaambiwa dk zimeisha!!! Halotel hiyo hata cha chuo lazima uwe na 3000 ndo unapata Cha siku7 GB1.3😟😟😟
Unanunua bando la wiki nzima la kifurushi cha internet labda bando la shilingi 3,000 unapewa 400MB (kwa mtandao naotumia mimi).

1. Mosi, hilo bando uliloambiwa ni la wiki litadumu kwa siku 6 kamili, badala ya kudumu kwa siku 7. Wenzetu hawa sijui wiki ina siku 6, au hizi siku wao wanazihesabu kwa staili gani, sielewi.

2. Pili, ukishanunua hilo bando sasa, ndo mziki unaanza sasa. Wanazikatakata/gawanya hizo bando; kuna MB wanazipeleka watsap (bila kujali kama wewe unatumia hiyo watsap au hutumii), zingine fesibuku (hivohivo hawajali upo huko fesibuku au haupo), zinazobaki ndio unaingiziwa bando la kawaida la kutumia kwenye internet.

Matokeo yake unapata mb chache sana kwa ajili ya internet na unatumia kwa siku hizo 6 badala ya 7.

Huu ni uzulumati wa mchana kweupe. Hivi TCRA mnayaona haya au hadi tuje huko maofisini kwenu kupanga foleni kuwaelezea haya?

Nyinyi sio watumiaji wa huduma hizi hamuoni upuuzi huu unaofanywa kwa watumiaji au mnasubiri jpm awatumbue?
 
Back
Top Bottom