vamda
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 919
- 598
Salam wana JF. Huwa natumia dishi la futi 6 kupata matangazo ya televisheni. Siku za nyuma nilikuwa napata matangazo mbalimbali ikiwemo TBC1 lakini sasa ni zaidi ya mwezi sipati matangazo yao. Kila nikiwasha TBC1 inaandika 'WEAK SIGNAL' Je ni kweli TBC1 wamepunguza masafa ya matangazo (signal)? Kama jibu ni ndio basi TBC1 haina faida kwa wananchi tulio wengi tunaoishi vijijini ambao hatuna huduma ya ving'amuzi. Madishi ndiyo yanayotuokoa. TBC1 watufikirie sisi wananchi tunaoishi vijijini maana hiyo ni telelvisheni ya Taifa, tuna haki ya kupata matangazo yao. Au kwa sababu wanataka kurusha kombe la dunia, wameamua kutubania sisi wanyonge tunaotumia madishi ili wafanye biashara yao ya ving'amuzi!