Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,277
- 8,840
KWA miaka mingi iliyopita palisikika kilio cha kutaka vyombo vya habari vya serikali vibadilike na kuacha kuwa vya propaganda za serikali, chama tawala au taasisi yoyote nyingine.
Watu wengi waliipongeza hatua ya serikali ya kuifanya Radio Tanzania na kituo cha serikali cha televisheni kuwa shirika na kuwa vya umma.
Hapo mwanzoni vituo vya redio na televisheni vya TBC, vilitoa mwanga wa kuwa kweli vya umma.
Lakini pole pole tokea TBC kupata uongozi mpya tunaona ukereketwa wa CCM na kujikita zaidi katika siasa kuliko kuheshimu maadili ya taaluma ya habari, ikiwa pamoja na ya watu kupata habari za kila upande.
Hii sasa Watanzania wengi unawasikia wakisema masikini TBC imepotea njia na hakuna wa kuiongoza njia sahihi.
TBC ya leo imejitokeza wazi kuonyesha ukereketwa wa CCM na kuegemea kupita kiasi upande wa serikali na kujisahau kuwa ni mali ya walipa kodi wote wa Tanzania.
Kwa kweli na hii sio siri TBC ya jana sio ya leo, na kama inataka kuendelea hivyo ni vizuri ikabadili jina na kujiita CCM Radio au CCM TV badala ya kutumia jina la Tanzania. Lakini ikifanya hivyo isitumie pesa za walipa kodi.
Mara nyingi nimesikia kwa uthibitisho juu ya namna ambavyo uongozi wa TBC ulivyowahi kulalamikia baadhi ya vipindi vilivyopita ambapo zilisikika sauti za kuikosoa serikali, kama vile ni haramu kufanya hivyo.
Watu wengi waliipongeza hatua ya serikali ya kuifanya Radio Tanzania na kituo cha serikali cha televisheni kuwa shirika na kuwa vya umma.
Hapo mwanzoni vituo vya redio na televisheni vya TBC, vilitoa mwanga wa kuwa kweli vya umma.
Lakini pole pole tokea TBC kupata uongozi mpya tunaona ukereketwa wa CCM na kujikita zaidi katika siasa kuliko kuheshimu maadili ya taaluma ya habari, ikiwa pamoja na ya watu kupata habari za kila upande.
Hii sasa Watanzania wengi unawasikia wakisema masikini TBC imepotea njia na hakuna wa kuiongoza njia sahihi.
TBC ya leo imejitokeza wazi kuonyesha ukereketwa wa CCM na kuegemea kupita kiasi upande wa serikali na kujisahau kuwa ni mali ya walipa kodi wote wa Tanzania.
Kwa kweli na hii sio siri TBC ya jana sio ya leo, na kama inataka kuendelea hivyo ni vizuri ikabadili jina na kujiita CCM Radio au CCM TV badala ya kutumia jina la Tanzania. Lakini ikifanya hivyo isitumie pesa za walipa kodi.
Mara nyingi nimesikia kwa uthibitisho juu ya namna ambavyo uongozi wa TBC ulivyowahi kulalamikia baadhi ya vipindi vilivyopita ambapo zilisikika sauti za kuikosoa serikali, kama vile ni haramu kufanya hivyo.