Tatizo la Wireless Internet

benja

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
331
Reaction score
230
Wadau nna tatizo. Ofisini internet ni ya Wireless lakini laptop yangu (sony) haishiki hiyo wireless. Cha ajabu nikiconnect na local area network inashika na nikiconect wireless ya simu (hotspot) inashika. Laptop yangu ina Operating Sytem ya Windows 10. naombeni msaada
 
Inawezekana ikawa access au routers hazipo compatible na wifi ya adapter ya pc yako

Nikuulize jina la network ya offisi yenu linaonekana kwenye computer?
 
possibility nyengine hio wifi inaweza kuwa band tofauti na uwezo wa laptop yako, una simu ya kisasa? simu inashika wifi ya ofisi?
 
Inawezekana ikawa access au routers hazipo compatible na wifi ya adapter ya pc yako

Nikuulize jina la network ya offisi yenu linaonekana kwenye computer?

Yes jina la Network naliona na naweza hata type password but in the process of connecting ndio inakata na kuandika 'cant connect to this network'
 
possibility nyengine hio wifi inaweza kuwa band tofauti na uwezo wa laptop yako, una simu ya kisasa? simu inashika wifi ya ofisi?

Yes nna simu ya kisasa na inashika wi-fi ya offisi
 
Wifi zipo na chanell 1-13 .

Ipo hivii. Nilinunua laptoo dell latitude e6230. Na simu tecno wx3lte ila laptop yangu ikawa haikamati kwenye hotspot ya simu.

Ila wifi nyingine zinashika freesh. Nilichokuja kugundua ni kuwa simu ilikua inabroadcast wifi chanell 13 ila laptop yangu haikamati chanell 13.

Nikabadilisja wifi adapter ya laptop , tatizo likaisha mpaka leo.

Kuna software (ngoja niicheki jina.) ukiiweka kwenye pc inayoshika hiyo wifi ita analyze na kukupa taarifa zote za hiyo wifi (channel+band) baada ya hapo sasa pitIa online ujue uwezo wa adapter yako.

Hi inatokea sana na pc used
 


asante mkuu
 

kifaa cha wireless kina uwezo gani,kiwango gani mfano 108a/b/g/n na uwezo mawimbi yake yakoje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…