Tatizo la UTI

KIGHERA

Member
Nov 19, 2010
84
27
Habari wadau,
Nilipata tatizo la kukojoa mara kwa mara na mkojo ukawa unauma kiasi ya kwamba nashidwa hata kuuzuia( yaani hata kama niko barabarani ni lazima nitafute sehemu nijisitiri vinginevyo ntaharibu).

Ikabidi niende hospital,docta akaniambia nina UTI ila aliangalia kisukari akaniambia sina hivyo akanipa dawa za siku 5 nikatumia zikaisha ila sikupata nafuu, nikawa nimesafiri ikanilazimu niende hospital nyingine na kumhadithia docta picha nzima na kwa bahati makasha ya zile dawa nilikuwa nazo nikamuonyesha, akaniambia nipime mkojo na akanifanyia kipimo kingine akaniambia ni kweli nina UTI na imekaa muda hiyo hata ngozi ya kibovu inaonekana ina uvimbe hivyo nae akanipa dawa.

Nikatumia zile dawa zikaisha,bado nikawa naskia tena ile hela hivyo nikarudi kwake akaniamba kuna maendeleao mazuri ila uvimbe haujaisha,akanipa dawa zingine na kunipiga sindano moja nazo nimemaliza last week ila ile hali naiskia bado hivyo napanga nikamuone tena.
Naomba ushauri wenu au kama m2 alipitia tatizo kama langu alifanyaje likaisha, maana linanisumbua kwa nn natumia dawa bado naendelea kulisikia.
 
Duuuh! Pole sana mkuu kwa tatzo hilo, subili wadau waje humu kuna watu wana matatzo yanayofanana.
 
UTI yako ilikua sugu hivyo itachukua muda kutoka,
kunywa maji mengi sana,

Kula matunda kama matango na matikiti kwa wingi sana.

Pole sana.
 
Habari wadau,
Nilipata tatizo la kukojoa mara kwa mara na mkojo ukawa unauma kiasi ya kwamba nashidwa hata kuuzuia( yaani hata kama niko barabarani ni lazima nitafute sehemu nijisitiri vinginevyo ntaharibu).

Ikabidi niende hospital,docta akaniambia nina UTI ila aliangalia kisukari akaniambia sina hivyo akanipa dawa za siku 5 nikatumia zikaisha ila sikupata nafuu, nikawa nimesafiri ikanilazimu niende hospital nyingine na kumhadithia docta picha nzima na kwa bahati makasha ya zile dawa nilikuwa nazo nikamuonyesha, akaniambia nipime mkojo na akanifanyia kipimo kingine akaniambia ni kweli nina UTI na imekaa muda hiyo hata ngozi ya kibovu inaonekana ina uvimbe hivyo nae akanipa dawa.

Nikatumia zile dawa zikaisha,bado nikawa naskia tena ile hela hivyo nikarudi kwake akaniamba kuna maendeleao mazuri ila uvimbe haujaisha,akanipa dawa zingine na kunipiga sindano moja nazo nimemaliza last week ila ile hali naiskia bado hivyo napanga nikamuone tena.
Naomba ushauri wenu au kama m2 alipitia tatizo kama langu alifanyaje likaisha, maana linanisumbua kwa nn natumia dawa bado naendelea kulisikia.
Mimi ninaweza kukutibia huo ugonjwa wako UTI na ukapona nitakupa dawa ya kutumia siku 30 na utapona kabisa. Ukihitaji tiba na matibabu toka kwangu Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu.
 
Hakikisha unakunywa maji Lita 4 mpaka 5 kwa siku punguza vilev soda na vitu zingine zisizo na tija kwa dawa njoo pm
 
nimeenda tena hospital kumuona docta,amenifanyia ultrasound na kuniambia naedelea vzr ila sijapona kabisa,so alinichoma sindano moja na kunipa vidonge vya TIDAZOL na ACELOFENCE (ZeRodol) samahani mm sio docta ila nilikuwa navisoma vilivyoandikwa ambavyo naendelea kuvitumia ntawajuza matokeo yake.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom