Habari, Wateja Wetu.
Tunapenda kutoa mrejesho kuhusu changamoto ya umeme kuwa mdogo (low voltage) inayowakabili baadhi ya wateja wetu katika Wilaya ya Chunya na wilaya ya Mkwajuni.
Tafadhali fahamu kuwa Serikali kupitia TANESCO inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto hii. Leo Septemba 11, 2026, mkataba wa ujenzi wa miundombinu muhimu ya umeme umesainiwa Wilayani Mkwajuni, hatua ambayo inalenga kuongeza upatikanaji wa umeme kwenye wilaya hizo.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 220 (220kV) kutoka Iganjo, Mbeya hadi Saza, Wilaya ya Mkwajuni, yenye urefu wa takribani kilomita 122, kwa thamani ya TSh bilioni 109. Aidha, mradi unahusisha ujenzi wa kituo cha kupozea umeme chenye uwezo wa 100MVA, sawa na takribani MW 80.
Mradi huu unatarajiwa kuleta kutatua changamoto yote ya upatikanaji wa umeme kwa wateja wote.
Hivyo, tunaomba muendelee kuwa na uvumilivu wakati utekelezaji wake unaendelea.
Tunawashukuru kwa ushirikiano na uvumilivu wenu.
Asante! ^HN