Tatizo la mifupa kusagika

Tatizo la mifupa kusagika

daudycharles

Member
Joined
Feb 19, 2014
Posts
50
Reaction score
16
Habari za leo wapendwa,

Jamani naombeni msaada wa mawazo kwamba mie nasumbuliwa na kusagika kwa viungo vyangu yaani ule uteute wa ktk magoti,mabega,viwiko,nyonga pamoja na pingili za mgongo nahisi umepungua,pia napatwa na maumivu hivyo siwezi fanya kazi ngumu sasa nakuwa naumia,je nitumie dawa gani ili kuweza kutibu tatizo hili?
 
Mkuu muuliza swali, natumaini we ni me. Naomba kuuliza swali moja la msingi kabla wadau hawajaja. Una umri gani na uzito wako ukoje?
Jibu la swali hilo linahusika katika kupelekea kupata Jibu na suluhuhisho kwako
 
Pole kwa yanayokusibu ndugu...

Kwa namna ulivyojieleza ni dhahiri kuwa una matatizo katika maungio ya mifupa.

Lakini ni ngumu kutambua moja kwa moja kwa kiasi gani umeathirika au ni aina ipi haswa ya matatizo ya joints uliyonayo.

Watu wengi wenye matatizo ya maungio ya mifupa hukumbwa na tatizo ambalo kitaalamu hujulikana kama Osteoarthritis.

Aina hii ya arthrits hutokea kutokana na kulika kwa layer laini 'articular cartilage' inayofunika mfupa kwenye maungio.

Ukiacha aina hii ya arthrits zipo aina nyinginezo hivyo ni vyema ukawatafuta wataalamu wa mifupa wakusaidie.

Ni vyema ukafanya hima sasa usichelewe kabla tatizo halijawa critical.
 
habari za leo wapendwa,

jamani naombeni msaada wa mawazo kwamba mie nasumbuliwa na kusagika kwa viungo vyangu yaani ule uteute wa ktk magoti,mabega,viwiko,nyonga pamoja na pingili za mgongo nahisi umepungua,pia napatwa na maumivu hivyo siwezi fanya kazi ngumu sasa nakuwa naumia,je nitumie dawa gani ili kuweza kutibu tatizo hili?

pole sana mimi ni mhanga wa hilo tatizo kwa zaidi ya miaka ishirini, nakumbuka miaka ya tisini nilipoanza kuumwa nilipatiwa dawa katika hospital ya kcmc moshi, nikapona lakini sio kivile, mpaka sasa natumia tiba mbadala ambazo zinanipa nafuu lakini sio kupona moja kwa moja, cha kukushauri wahi mapema muhimbili ukafanyiwe vipi au hospital yoyote kubwa halafu nakupa hii no. 0755360508 hiyo ni tiba mbadala wapo kinondoni natumia dawa zao napata nafuu
 
Mkuu muuliza swali, natumaini we ni me. Naomba kuuliza swali moja la msingi kabla wadau hawajaja. Una umri gani na uzito wako ukoje?
Jibu la swali hilo linahusika katika kupelekea kupata Jibu na suluhuhisho kwako
Kaka mim na miaka 24 alafu nimepima juzi na kilo 55 na ni mrefu kama wa Mt1%naa yan nimeaz kupata shida ya kumwa na nyonga sana pale napo tembea na na mishipa kuvuta kama mifupa inasagana nilikuwa nataman kujua kama kilo n sababi
 
Back
Top Bottom