Nina mtoto wa uncle wangu mwenye umri wa miaka takribani 18. Alikuwa na afya njema kabisa na alikuwa anafanya vyema kwenye masomo, yupo form three.
Lakini sasa hali yake si shwari kabisa kwani kapatwa na ugonjwa wa kuzimia kwa ghafla muda wa miezi miwili, tatu sasa, hasa mida kuanzia saa sita usiku akiwa kalala, na huwa inatokea kwa nguvu hasa.
Kisha anatapika; na mara chache amekuwa anaweweseka na kupiga makelele usiku kiasi cha hata kuamsha majirani.
Sasa wakuu kwa info nilizonazo, walimpleleka hospitali kwa doctor wa Moyo, akafanyiwa x-ray wakamwambia hawaoni tatizo lolote. Wakahangaika kwa tiba za jadi, waganga bado tatizo likawa palepale. Kinachohuzunisha ni kuwa huyu kijana amekata tamaa mpaka akafikia hatua ya kutaka kujiua na kusema kuwa anapoteza hela za wazazi tu, bora afe kama haponi. Watu wamejaribu kumsihi na kumshauri na yeye mwenyewe akaamua kumpokea Yesu, kwani ndio anaona suluhisho la mwisho.
Lakini jana hali ile ya kuzimia imetokea tena baada ya kutulia siku chache baada ya kumpokea Yesu. Sasa ninachouliza, Je kuna mtu mwenye idea haya ni majonjwa ya aina gani kama ni ya kibinadamu? au ndio mambo ya kiswahili?
Na kama kuna mtu anayefahamu Mchungaji anayeweza kumuombea kijana wetu aweze kufurahia maisha kama watu wengine tunaomba ushauri. Inauma kuona kijana mtiifu, hard working, maisha yake yanakwenda mrama namna hii.
Asanteni kwa michango yenu.
Lakini sasa hali yake si shwari kabisa kwani kapatwa na ugonjwa wa kuzimia kwa ghafla muda wa miezi miwili, tatu sasa, hasa mida kuanzia saa sita usiku akiwa kalala, na huwa inatokea kwa nguvu hasa.
Kisha anatapika; na mara chache amekuwa anaweweseka na kupiga makelele usiku kiasi cha hata kuamsha majirani.
Sasa wakuu kwa info nilizonazo, walimpleleka hospitali kwa doctor wa Moyo, akafanyiwa x-ray wakamwambia hawaoni tatizo lolote. Wakahangaika kwa tiba za jadi, waganga bado tatizo likawa palepale. Kinachohuzunisha ni kuwa huyu kijana amekata tamaa mpaka akafikia hatua ya kutaka kujiua na kusema kuwa anapoteza hela za wazazi tu, bora afe kama haponi. Watu wamejaribu kumsihi na kumshauri na yeye mwenyewe akaamua kumpokea Yesu, kwani ndio anaona suluhisho la mwisho.
Lakini jana hali ile ya kuzimia imetokea tena baada ya kutulia siku chache baada ya kumpokea Yesu. Sasa ninachouliza, Je kuna mtu mwenye idea haya ni majonjwa ya aina gani kama ni ya kibinadamu? au ndio mambo ya kiswahili?
Na kama kuna mtu anayefahamu Mchungaji anayeweza kumuombea kijana wetu aweze kufurahia maisha kama watu wengine tunaomba ushauri. Inauma kuona kijana mtiifu, hard working, maisha yake yanakwenda mrama namna hii.
Asanteni kwa michango yenu.