tatizo la ku change gear kwenye alteza gitta

tatizo la ku change gear kwenye alteza gitta

elmagnifico

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2011
Posts
8,260
Reaction score
9,747
Jumapili ya iliyopita nilipata ajali gari langu liligongwa kwa nyuma likabonyea na bamba likapinda, bahati nzuri halikupasuka kioo wala taa.
Siku hiyo hiyo nililipeleka kwa fundi alinyooshe lilikaa siku tatu kaliniletea jana.
Sasa tatizo ni kwamba nilipoliendesha nikagundua linaunguruma sana na linachelewa badili gear toka namba moja kwenda mbili na mbili kwenda tatu.
Kwenye mlima ndo kabisa linabaki namba moja.
Kuna jamaa flani aliniambia tatizo litakuwa mafla na kuitengeneza milion 2 ila akaonekana mbabaishaji na hakuwa na uhakika wa alisemalo na bei ilinitisha kama ki alteza tu bei hiyo prado si ataniambia milioni kumi.
Wanajamvi nani anamfahamu fundi mzuri anayeweza nisaidia tatizo hili.
 
Mambo ya Gear kuchange ni GearBox (ni kutoka Engine-Gearbox-Diff /Driving shaft)
lakini anakuambia Mafla hiyo ni tofauti kabisa huko ni katika uchomaji wa mafuta mainfold - Exhaust
Mimi naendeshaga tu lakini kwa Idea huenda Gear box ilishtuka ndio maana gear za automatic hazipokeani
 
Mambo ya Gear kuchange ni GearBox (ni kutoka Engine-Gearbox-Diff /Driving shaft)
lakini anakuambia Mafla hiyo ni tofauti kabisa huko ni katika uchomaji wa mafuta mainfold - Exhaust
Mimi naendeshaga tu lakini kwa Idea huenda Gear box ilishtuka ndio maana gear za automatic hazipokeani

Asante kaka kwa mchango wako
 
Nenda garage, kabadili hydraulic na kusafisha sample ya g/box na filter yake ndani.

Inawezekana ikawa ndo tatizo kweli maana inabd nkaifanyie marekebsho ikifikia km 78000 nw iko 77000
 
Nenda garage, kabadili hydraulic na kusafisha sample ya g/box na filter yake ndani.

Kwel akanunue hydraulic abadil ila km bado tafuta fund wire ring wa magar aliye na ujuz na magar ya kisasa mimi ki proffesional ni fund wa engine lakin hyo jamaa aliye kwambia tatzo exhaust unge mchapa bakora hyo ni yahaya
 
Niko dar mkuu

Mkuu nenda Msasani, kuna garage wanaiita General Tyre, ile barabara ya kutoka Namanga, Msasni hadi Masaki. Kabla hujafika CCBRT uliza General tyre, watatatua tatizo la gari yako. Au nenda kwa Wachina wa pale Kijitonyama maeneo ya Sayansi nyuma ya kituo cha mafuta cha OILCOM.
 
Mkuu nenda Msasani, kuna garage wanaiita General Tyre, ile barabara ya kutoka Namanga, Msasni hadi Masaki. Kabla hujafika CCBRT uliza General tyre, watatatua tatizo la gari yako. Au nenda kwa Wachina wa pale Kijitonyama maeneo ya Sayansi nyuma ya kituo cha mafuta cha OILCOM.

Asante sana mkuu ntafka hapo
 
Inawezekana ikawa ndo tatizo kweli maana inabd nkaifanyie marekebsho ikifikia km 78000 nw iko 77000

Sio inawezakana,hapo ndio kwenye tatizo fanya ulivyoshauriwa. Tatizo kama hilo nilipata kwenye gx100.
 
Asante kaka kwa mchango wako
ELMANifico unaniita mkaka mbona sikuelewi au kukuelezea muundo wa ufanyaji kazi wa gari? mbona elimu hii hutolewa kwingi tena mm ni ya zamani sana Arusha Tech miaka ya 90' na nianaendesha magari makubwa zaidi'
ILA NIPE JIBU BASI UMESHAITENGENEZA?
km bado tafuta gereji zozote za Wachina watalitatua mara moja kaka yangu
 
Last edited by a moderator:
ELMANifico unaniita mkaka mbona sikuelewi au kukuelezea muundo wa ufanyaji kazi wa gari? mbona elimu hii hutolewa kwingi tena mm ni ya zamani sana Arusha Tech miaka ya 90' na nianaendesha magari makubwa zaidi'
ILA NIPE JIBU BASI UMESHAITENGENEZA?
km bado tafuta gereji zozote za Wachina watalitatua mara moja kaka yangu

Sorry mwanamama, nilipitiwa tu, nashukuru nimefaniki lilikuwa tatizo la kubadili mafuta ya gear box and everything ikarudi kuwa sawa.
Halafu wajua wewe ni kati ya wanawake wachache wengi wanajua kuendesha hata spare tyre hawajui inapohifadhiwa kwenye gari zao
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom