Tatizo ana tattoo, nimuulize?

Tatizo ana tattoo, nimuulize?

MTINGIJOLI

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2014
Posts
1,460
Reaction score
1,476
Habari za asubuhi wanajukwaa, hongereni na majukumu ya kujenga taifa ketu.


Turudi kwenye mada yetu, katika pitapita zangu nimekutana na binti mrembo, nilifahamiana nae baada ya kwenda kwenye ofisi zao na yeye ndie alienitatulia shida yangu, bssi hapo ndipo urafiki wetu ulipoanzia hadi kufikia kwenye mapenzi, kipindi chote hicho hatukuwahi kukutana kimwili hadi wiki mbili zilizopita ndio tulipanga kukutana, basi tukiwa faragha na mahaba ya hapa na pale, hamadi namsauka nguo, namkuta ana tattoo pajani, kwa kweli nilishtuka mnoo,

Ila nilijitahidi nisimuonyeshe kama kuna chochote cha tufauti, basi tunafanya yetu ila mi nikiwa na lundo la mawazo kichwani, nilichokuja kugundua hata yeye hakua anataka niwe naiangalia ile tattoo, maana nikitupa jicho huwa anaificha kinamna flani, kwa upande wangu mimi, mtu mwenye tattoo huwa namfikiria kinamna nyengine kabisa ( samahani kwa wote wenye tattoo, sina lengo baya) sasa nashindwa nimuulize anijibu ili moyo wangu uwe na amani?

Au nimuache tu kimya kimya, ( ila ataumia mno, maana penzi limekolea sana, hasa kipindi hiki)

Hebu nishaurini wadau, maana naamini humu kuna wabobezi wa mambo mbali mbali, napokea aina zote za ushauri na maoni yote.

Natanguliza shukrani.
 
Demu mwenye tattoo zaidi ya moja au kutoboa ulimi na kitovu huwa nnawafikiria tofauti sana
 
мωαмвιє ѕιρєη∂ι нιуσ αкαιƒυтє, ℓαв∂α αтαвα∂ιℓι мƒυмσ ωα мαιѕнα уαкє кωα αјιℓι уαкσ
 
Tatoo ni urembo jaman kama kupaka powder, wanja lipstic sijui piko m sioni tatizo labda awe na tabia chafu ndo utaogopa tabia ila tatoo hapana kwa kweli
 
Unataka umuulize nini? Na tattoo umeshaiona
 
tattoo kwenye paja?urembo huu auone nani!
swali gumu, ila mimi sikubaliani na hiyo tattoo yake,
si unajua akili ya wasichana aliona akichora hiyo tattoo Kama akikutana na mwanaume atamuona yupo romantic sana yaani ataongezeka mvuto.
 
Tatizo umeshaingia uwanja mwingine busara yako ikuongoze, ila kuna ugumu hapo
 
Kiukweli mimi pia hua naona tatoo kama uchafu flani mwilini.. yaani naona kama kovu hivi! Eti unakuta binti ana paja lake jororo kabisa rangi ya mtume halafu analichafua kwa matatoo. Kwangu hapana kwakweli.
 
Back
Top Bottom