Tathmini: Dhamira ya "maandamano ya Mange" imefanikiwa

Tathmini: Dhamira ya "maandamano ya Mange" imefanikiwa

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2007
Posts
1,116
Reaction score
4,773
Maandamano yaliyopangwa kufanyika jana April 26, 2018 hayakutokea. Hilo halina mjadala.Na wala si la kushangaza. Kwa nguvu kubwa iliyoonyeshwa na vyombo vya dola juzi, ilihitaji zaidi ya ujasiri kwa mtu kujitokeza mtaani kuandamana.

Ni rahisi kuwalaumu Watanzania kuwa ni watu wa maneno zaidi kuliko vitendo. Japo hilo lina ukweli kwa kiasi flani — na lilipaswa kuzingatiwa wakati wa maandalizi ya maandamano hayo — lakini ukweli unabaki kuwa Magufuli alikuwa keshajiandaa “kunywa damu za waandamanaji.”

Sasa haihitaji uelewa japo mdogo wa tasnia ya mikakati kubaini kwamba kama unafahamu fika kwamba adui yako ametega mabomu njia flani, basi usipite njia hiyo.

Vita yoyote ile inahitaji mikakati. Na mikakati ya vita huwa flexible, kwa maana kwamba inaweza kubadilika muda wowote ule. Na mkakati hujumusha wapangaji wa mkakati husika na watekelezaji wa mkakati huo.

Katika suala la maandamano hayo, mhusika mkuu katika kupanga mikakati ya maandamano hayo alikuwa bloga wa Kitanzanian anayeishi nchini Marekani, Mange Kimambi.

Na watekelezaji wa mikakati ya maandamano hayo walikuwa Watanzania wote wanaoguswa na hali ilivyo huko nyumbani.

Na haijalishi jitihada kubwa kiasi gani zimetumika katika kuandaa mkakati, utekelezaji wake utategemea zaidi mazingira ya wakati husika. Na kubadili mwelekeo wa mkakati ni sehemu ya mafanikio ya mkakati husika.

Kwahiyo, uamuzi wa watu kutojitokeza mtaani kuandamana baada ya kuona kila dalili kuwa kuna mtu ana kiu ya damu zao ulikuwa uamuzi wa busara. Ulipaswa kuwa sehemu ya mikakati ya maandamano hayo.

Kwenye mikakati ya operesheni za kishushushu, kwa mfano, miongoni mwa masuala yanayoangaliwa wakati wa kuandaa operesheni ni “if things go wrong.” Yaani iwapo mambo yatakwenda kinyume na matarajio. Na hapo mkakati unazaa “mpango mbadala” (Plan B).

Muda huu ambapo baadhi ya watu wanaweza kuwa wamehitimisha kuwa wazo la maandamano halikufanikiwa, tungeweza kuwa tuna vilio vikubwa iwapo baadhi ya wenzetu wangeweka kando busara na kujiingiza mtaani na hatimaye kujeruhiwa au kuuwawa.

Haipaswi kulaumiana kuwa “watu wamemwangusha Mange” kwa sababu kimsingi maandamano hayo yalikuwa kwa ajili ya kila Mtanzania anayeitakia mema nchi yetu. Having said that, Mange anastahili pongezi nyingi kwa jitihada kubwa alizofanya kuja na wazo hilo na kulihamasisha kwa nguvu kubwa kabisa.

Kama kuna mapungufu katika mikakati ya maandalizi ya maandamano hayo basi ilikuwa huku ughaibuni. Nadhani kilichochangia kujitokeza kwa watu wachache ni kukosekana “uongozi” katika nchi husika.

Kwamba, watu walitarajiwa wajisukume wenyewe kwenda palipo na ubalozi wa Tanzania katika nchi husika. Kijiografia, mtu anayeishi Uskochi, kwa mfano, pengine ingemlazimu alale London ili aweze kushiriki maandamano hayo saa tatu asubuhi. Kwahiyo, laiti kungekuwa na “uongozi” basi labda ingekubaliwa kuwa badala ya waandamanaji wote kukutana London, ziwepo sehemu nyingine kwa Uskochi, Wales na Eire ya Kaskazini.

Nimeandika kwenye kichwa cha habari kuwa dhamira ya maandamano hayo imefanikiwa. Naam, imefanikiwa kwa sababu kuu mbili. Kwanza, ujumbe umemfikia Magufuli bila hata kuandamana. Na ikumbukwe kuwa ile nguvu kubwa iliyotumika kudhibiti maandamano hayo inamaanisha mabilioni ya shilingi yametumika katika kipindi hiki ambapo serikali ya kidikteta inakabiliwa na hali ngumu mno kifedha.

Pili, soma nukuu hii kutoka kwenye makala niliyoitafsiri kutoka gazeti la kimataifa la Africa Confidential [emoji117]Jarida Maarufu la Kimataifa Lachambua Ubabe wa Magufuli, Maandamano Na "Lamfagilia" Mange ~ Kulikoni Ughaibuni

Haitojalisha hata kama hakuna mtu atayejitokeza kuandamana Aprili 26. Kutoka umbali wa kilomita 26,000, Kimambi tayari ameweza kufanya zaidi ya kutikisa mkia wa chui kwa kutumia simu ya mkononi tu. Na laiti ikitokea asalimisha yeye mwenyewe, mara moja kukamatwa kwake kutakuwa tukio kubwa kabisa litakaloiweka Tanzania kwenye macho na masikio ya dunia nzima.

Naam, Mange amemudu “kumpelekesha” Magufuli na serikali yake nzima, sio kwa kutumia silaha, sio kwa kutumia vitisho, sio kwa kutumia kitu kingine chochote kile zaidi ya POSTS ZA INSTAGRAM. Yaani ni kama Mange ameua tembo kwa ubua. Kafanikiwa kumtetemesha Magufuli mpaka naambiwa huko Dodoma kwenye maadhimisho ya kashindwa kusalimia kwenye gari la wazi.

Sijasikia tathmini ya Mange kuhusu maandamano hayo lakini I hope hatoishia kudhani kuwa Watanzania wamemwangusha kwa vile hawakuingia mitaani kama ilivyokusudiwa.

Kadhalika natumaini hatokata tamaa hasa ikizingatiwa kuwa kwa sie wenye uelewa wa masuala haya, dhamira yake ya maandamano imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Kamwe katika historia ya Tanzania hakujawahi kutokea mtu mmoja kuwa na nguvu alizonazo Mange muda huu kiasi kwamba “anamwendesha Magufuli kwa rimoti.” Kuna msemo mmoja kwamba “it is the first to act who controls the game.” The first to act alikuwa Mange na idea ya maandamano.Na kwa hakika amemudu kui-control hiyo game mpaka mwisho.

Naam, maandamano hayakutokea yalivyokusudiwa lakini ujumbe umefika. Magufuli ana hofu kubwa zaidi ya alivyokuwa kabla ya jana.

Itakuwa kosa kubwa sana kuachana na jitihada hizi. Nyerere na wenzake walipoanza mapambano dhidi ya mkoloni hawakufanikiwa kwa siku moja. Hata mtoto akizaliwa haanzi kutembea siku hiyohiyo. Ingekuwa miujiza kama maandamano yangefanyika nchi nzima na Magufuli kuamua kujiuzulu kwa hiari yake.Hii kitu inahitaji jitihada endelevu.

Lakini pengine kubwa zaidi ni haja ya ushirikiano miongoni mwa watu wenye nia ya dhati ya kuung’oa udikteta wa Magufuli. Kila mtu akifanya kivyake, sio tu itamwia rahisi dikteta huyo kuzima jitihada husika bali pia uwezekano wa mafanikio utakuwa mdogo. Umoja ni nguvu.

Nihitimishe makala hii kwa kumpongeza Mange kwa mafanikio ya kihistoria katika suala hili.Ujumbe umefika, and that’s all that matters. Maandamano yalipaswa kuwa symbolic tu, na nina uhakika kuwa mamilioni ya Watanzania wameandamana kimoyomoyo. Changamoto kubwa sasa ni kuhakikisha kuwa kiu ya Watanzania kuung’oa udikteta haipotei.

Naam, watadhihaki kuwa maandamano hayajatokea lakini kile ambacho hawatosema ni kwamba “badala ya wananchi kuandamana, polisi na jeshi ndo walioandamana” tena sio bure bali kwa gharama kubwa kwa serikali iliyo taaban kifedha.
Screenshot_20180427-184430_Medium.jpg


Chanzo: “Tathmini: Dhamira Ya ‘Maandamano Ya Mange’ Imefanikiwa” @Chahali
 
Jana tuliandamana mioyoni mwetu nyumbani jamani.
 
Jana tuliandamana mioyoni mwetu nyumbani jamani.
Sijui kama ujumbe ulikuwa unawakilishwa bila ya support ya watu na ikaonekana hiyo ni hali mutual kwa watanzania wote. Mtu anaweza kuwa hampendi rais akaamua kuandaa maandamano ya kuwasemea watu ambao wao hawakuonyesha kwa lolote kukubaliana na hilo. Mimi najua London kuna watz kibao siyo wale saba tulio waona, Sweden ndiyo usiseme sasa huko ulaya watu hawafiki 100 waliogopa nini ?. Tanzania yenye 55 mil inasemewa na watu waliyopo out of the country less than one class la primary school. Madai yao yalikuwa watandamana non stop mpaka aondoke madarakani sasa leo mbona kimya. Sidhani kama nakubaliana na dhana ya kusema aondoke madarakani , hata ningeunga mkono maandamano nisinge taka hilo. Mimi nataka mjadala mkubwa wa rasimu ya katiba ya Warioba urudi na siyo hayo ya uhuru wa kusema ambao tunao. Watu wanakufa au wanapigwa risasi nani ametuonyesha proof kuwa ni serikali inawapiga? Huu upinzani wenyewe wa kichokoraa hakuna la maana wanalofanya wanakula pesa za kodi kuliko wata serikali unamkabidhi nani gurudumu la maendeleo watu hawawezi kuendeshwa kinyumbu wakaandamana kwa kitu kisicho wadhuru direct. Siyo watanzania tafuteni pengine sisi tunataka katiba mpya ili haya mema anayofanya Rais yaweze kuwa sustainable na mabaya yake tujaribu kuyapunguza kwa kupunguza mamlaka makubwa aliyowekewa hata yeye Rais atakuelewa kuliko mapinduzi ya Mange. Maana kusema kafikisha ujumbe kwani lengo ni ujumbe kufika au Rais kujiuzulu au umesahau lengo kuu la maandamano.
 
Ndefu mno ndani imejaa takataka tu, zoezi lililo Shindwa linapambwa lionekane ushindi, ni mazuzu pekee watakubaliana na ujinga huu.
Mange mwenyewe anajuta, haamini mlichomtenda
Sema ulikwepa umande. Kama kuandika sentensi moja tu mgogoro (angalia ulivyopachika herufi kubwa katikati ya sentensi) utaweza kusoma makala? [emoji3]
 
Sijui kama ujumbe ulikuwa unawakilishwa bila ya support ya watu na ikaonekana hiyo ni hali mutual kwa watanzania wote. Mtu anaweza kuwa hampendi rais akaamua kuandaa maandamano ya kuwasemea watu ambao wao hawakuonyesha kwa lolote kukubaliana na hilo. Mimi najua London kuna watz kibao siyo wale saba tulio waona, Sweden ndiyo usiseme sasa huko ulaya watu hawafiki 100 waliogopa nini ?. Tanzania yenye 55 mil inasemewa na watu waliyopo out of the country less than one class la primary school. Madai yao yalikuwa watandamana non stop mpaka aondoke madarakani sasa leo mbona kimya. Sidhani kama nakubaliana na dhana ya kusema aondoke madarakani , hata ningeunga mkono maandamano nisinge taka hilo. Mimi nataka mjadala mkubwa wa rasimu ya katiba ya Warioba urudi na siyo hayo ya uhuru wa kusema ambao tunao. Watu wanakufa au wanapigwa risasi nani ametuonyesha proof kuwa ni serikali inawapiga? Huu upinzani wenyewe wa kichokoraa hakuna la maana wanalofanya wanakula pesa za kodi kuliko wata serikali unamkabidhi nani gurudumu la maendeleo watu hawawezi kuendeshwa kinyumbu wakaandamana kwa kitu kisicho wadhuru direct. Siyo watanzania tafuteni pengine sisi tunataka katiba mpya ili haya mema anayofanya Rais yaweze kuwa sustainable na mabaya yake tujaribu kuyapunguza kwa kupunguza mamlaka makubwa aliyowekewa hata yeye Rais atakuelewa kuliko mapinduzi ya Mange. Maana kusema kafikisha ujumbe kwani lengo ni ujumbe kufika au Rais kujiuzulu au umesahau lengo kuu la maandamano.
ulitaka kusema naona kama umejizungusha vilee
 
Ndefu mno ndani imejaa takataka tu, zoezi lililo Shindwa linapambwa lionekane ushindi, ni mazuzu pekee watakubaliana na ujinga huu.
Mange mwenyewe anajuta, haamini mlichomtenda
Huyu Kulikoni Ughaibuni (anayejifanya alikuwa usalama wa Taifa) ni mtu wa kumpuuza tu. Hana tofauti na Ansbert Ngurumo. Wote wanajiona wajanjaa wakati hawana kitu.
 
If things go wrong.....improvise yourself.... Na hiki ndicho watanzania tulichokifanya baada ya kuona vikosi vimetanda kila kona.
 
Alitaka kuondoa uongozi halali uliowekwa kwa kura za wananchi..

Hilo halikutimia...

Watanzania wanajua namna sahihi za kutatua Changamoto zao...

Anayefikiri kushinda kwa kutumia violence...

Afikiri Mara mbili...

Hili ni Somo tosha kwa yeyote...
 
Serikali haijajibu hoja za wananchi, wananchi wamejibiwa kwa Vitisho, Watch Out.....

Bomu litalipuka soon

Ajira zimepotea na sukari kutoka 1800 hadi 2800

Serikali inachezea FAO la Kujitoa na Mafao ya wastaafu...

Wafanyakazi hawajaongezewa mishahara miaka 3

Uchumi umedorora..Shillini ni 2290 Tshs kwa Dola moja

A - Rais wa nchi ameacha Shughuli nyingi sana na kumfikiria Dr. Mange
B - Vyombo vyote vya Dola Vikahangaika na Dr. Mange
C - Vyombo ya Kimataifa vimejua hali halisi ya Tanzania
D - Serikali inapambana na wananchi, Je nani wanamuunga mkono huyo Jiwe?
E- Kwa nini aogope maandamano kama anafanya vitu vizuri kwa wananchi, Na wanampenda

Tupo Gizani: Maswali na hoja za wananchi bado kujibiwa

1 - 1.5 Trillioni ziko wapi?

2- Uhuru wa habari na demokrasia?

3 - Unafungia social media lakini hunyongi mafisadi (Eti kama china)

4 - Mafao ya Jamii - CCM na Serikali yake imetafuna

5- Sukari Jiwe akapandisha kutoka 1800 hadi 2800

6- Uchumi Jiwe ameua

7 - Ajira hakuna kabisa

Kejeli za vilaza wachache wa Lumumba, haziwezi kuzima hoja hizo hapo juu.

Vijana wa Lumumba wanalipwa special allowance ili kulinda mkate wa wachache, wanao tafuna keki ya taifa

-Wanajua fika kuwa hoja zao ni dhaifu Mbele ya Jukwaa hili la JF ---Ndio maana Bwana mkubwa analalamika Watanzania kuamini mitandao ya Jamii

Pili, Ni wazi kuwa Mikataba Feki walioingia CCM na Serikali yake ndio wanaibia nchi hii. Bado Wezi na Mabwanyenye wanaiba sana, kwa akili nyingi..Kwa sababu Mikataba bado ipo

CCM wakaingia mkataba na CHina na gesi ya Mtwara haina faida tena

Hivi waliingia mikataba mibaya ya kufilisi nchi si bado wako CCM

Au je, Mahakama ya Mafisadi imefunga wangapi? Vijana wa Lumumba, endelezeni njaa na kuwasaliti Watanzania.
 
Sema ulikwepa umande. Kama kuandika sentensi moja tu mgogoro (angalia ulivyopachika herufi kubwa katikati ya sentensi) utaweza kusoma makala? [emoji3]
Exactly! Hapa ndo ninaamini ule usemi kuwa Watanzania ni wavivu wa kusoma. Sasa makala ya kusoma under five minutes maximum mtu anaamua kuikacha ila ingekuwa stori za dhahania juu ya kisa cha mapenzi hata page 10 angesoma
 
Maandamano yaliyopangwa kufanyika jana April 26, 2018 hayakutokea. Hilo halina mjadala.Na wala si la kushangaza. Kwa nguvu kubwa iliyoonyeshwa na vyombo vya dola juzi, ilihitaji zaidi ya ujasiri kwa mtu kujitokeza mtaani kuandamana.

Ni rahisi kuwalaumu Watanzania kuwa ni watu wa maneno zaidi kuliko vitendo. Japo hilo lina ukweli kwa kiasi flani — na lilipaswa kuzingatiwa wakati wa maandalizi ya maandamano hayo — lakini ukweli unabaki kuwa Magufuli alikuwa keshajiandaa “kunywa damu za waandamanaji.”

Sasa haihitaji uelewa japo mdogo wa tasnia ya mikakati kubaini kwamba kama unafahamu fika kwamba adui yako ametega mabomu njia flani, basi usipite njia hiyo.

Vita yoyote ile inahitaji mikakati. Na mikakati ya vita huwa flexible, kwa maana kwamba inaweza kubadilika muda wowote ule. Na mkakati hujumusha wapangaji wa mkakati husika na watekelezaji wa mkakati huo.

Katika suala la maandamano hayo, mhusika mkuu katika kupanga mikakati ya maandamano hayo alikuwa bloga wa Kitanzanian anayeishi nchini Marekani, Mange Kimambi.

Na watekelezaji wa mikakati ya maandamano hayo walikuwa Watanzania wote wanaoguswa na hali ilivyo huko nyumbani.

Na haijalishi jitihada kubwa kiasi gani zimetumika katika kuandaa mkakati, utekelezaji wake utategemea zaidi mazingira ya wakati husika. Na kubadili mwelekeo wa mkakati ni sehemu ya mafanikio ya mkakati husika.

Kwahiyo, uamuzi wa watu kutojitokeza mtaani kuandamana baada ya kuona kila dalili kuwa kuna mtu ana kiu ya damu zao ulikuwa uamuzi wa busara. Ulipaswa kuwa sehemu ya mikakati ya maandamano hayo.

Kwenye mikakati ya operesheni za kishushushu, kwa mfano, miongoni mwa masuala yanayoangaliwa wakati wa kuandaa operesheni ni “if things go wrong.” Yaani iwapo mambo yatakwenda kinyume na matarajio. Na hapo mkakati unazaa “mpango mbadala” (Plan B).

Muda huu ambapo baadhi ya watu wanaweza kuwa wamehitimisha kuwa wazo la maandamano halikufanikiwa, tungeweza kuwa tuna vilio vikubwa iwapo baadhi ya wenzetu wangeweka kando busara na kujiingiza mtaani na hatimaye kujeruhiwa au kuuwawa.

Haipaswi kulaumiana kuwa “watu wamemwangusha Mange” kwa sababu kimsingi maandamano hayo yalikuwa kwa ajili ya kila Mtanzania anayeitakia mema nchi yetu. Having said that, Mange anastahili pongezi nyingi kwa jitihada kubwa alizofanya kuja na wazo hilo na kulihamasisha kwa nguvu kubwa kabisa.

Kama kuna mapungufu katika mikakati ya maandalizi ya maandamano hayo basi ilikuwa huku ughaibuni. Nadhani kilichochangia kujitokeza kwa watu wachache ni kukosekana “uongozi” katika nchi husika.

Kwamba, watu walitarajiwa wajisukume wenyewe kwenda palipo na ubalozi wa Tanzania katika nchi husika. Kijiografia, mtu anayeishi Uskochi, kwa mfano, pengine ingemlazimu alale London ili aweze kushiriki maandamano hayo saa tatu asubuhi. Kwahiyo, laiti kungekuwa na “uongozi” basi labda ingekubaliwa kuwa badala ya waandamanaji wote kukutana London, ziwepo sehemu nyingine kwa Uskochi, Wales na Eire ya Kaskazini.

Nimeandika kwenye kichwa cha habari kuwa dhamira ya maandamano hayo imefanikiwa. Naam, imefanikiwa kwa sababu kuu mbili. Kwanza, ujumbe umemfikia Magufuli bila hata kuandamana. Na ikumbukwe kuwa ile nguvu kubwa iliyotumika kudhibiti maandamano hayo inamaanisha mabilioni ya shilingi yametumika katika kipindi hiki ambapo serikali ya kidikteta inakabiliwa na hali ngumu mno kifedha.

Pili, soma nukuu hii kutoka kwenye makala niliyoitafsiri kutoka gazeti la kimataifa la Africa Confidential [emoji117]Jarida Maarufu la Kimataifa Lachambua Ubabe wa Magufuli, Maandamano Na "Lamfagilia" Mange ~ Kulikoni Ughaibuni

Haitojalisha hata kama hakuna mtu atayejitokeza kuandamana Aprili 26. Kutoka umbali wa kilomita 26,000, Kimambi tayari ameweza kufanya zaidi ya kutikisa mkia wa chui kwa kutumia simu ya mkononi tu. Na laiti ikitokea asalimisha yeye mwenyewe, mara moja kukamatwa kwake kutakuwa tukio kubwa kabisa litakaloiweka Tanzania kwenye macho na masikio ya dunia nzima.

Naam, Mange amemudu “kumpelekesha” Magufuli na serikali yake nzima, sio kwa kutumia silaha, sio kwa kutumia vitisho, sio kwa kutumia kitu kingine chochote kile zaidi ya POSTS ZA INSTAGRAM. Yaani ni kama Mange ameua tembo kwa ubua. Kafanikiwa kumtetemesha Magufuli mpaka naambiwa huko Dodoma kwenye maadhimisho ya kashindwa kusalimia kwenye gari la wazi.

Sijasikia tathmini ya Mange kuhusu maandamano hayo lakini I hope hatoishia kudhani kuwa Watanzania wamemwangusha kwa vile hawakuingia mitaani kama ilivyokusudiwa.

Kadhalika natumaini hatokata tamaa hasa ikizingatiwa kuwa kwa sie wenye uelewa wa masuala haya, dhamira yake ya maandamano imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Kamwe katika historia ya Tanzania hakujawahi kutokea mtu mmoja kuwa na nguvu alizonazo Mange muda huu kiasi kwamba “anamwendesha Magufuli kwa rimoti.” Kuna msemo mmoja kwamba “it is the first to act who controls the game.” The first to act alikuwa Mange na idea ya maandamano.Na kwa hakika amemudu kui-control hiyo game mpaka mwisho.

Naam, maandamano hayakutokea yalivyokusudiwa lakini ujumbe umefika. Magufuli ana hofu kubwa zaidi ya alivyokuwa kabla ya jana.

Itakuwa kosa kubwa sana kuachana na jitihada hizi. Nyerere na wenzake walipoanza mapambano dhidi ya mkoloni hawakufanikiwa kwa siku moja. Hata mtoto akizaliwa haanzi kutembea siku hiyohiyo. Ingekuwa miujiza kama maandamano yangefanyika nchi nzima na Magufuli kuamua kujiuzulu kwa hiari yake.Hii kitu inahitaji jitihada endelevu.

Lakini pengine kubwa zaidi ni haja ya ushirikiano miongoni mwa watu wenye nia ya dhati ya kuung’oa udikteta wa Magufuli. Kila mtu akifanya kivyake, sio tu itamwia rahisi dikteta huyo kuzima jitihada husika bali pia uwezekano wa mafanikio utakuwa mdogo. Umoja ni nguvu.

Nihitimishe makala hii kwa kumpongeza Mange kwa mafanikio ya kihistoria katika suala hili.Ujumbe umefika, and that’s all that matters. Maandamano yalipaswa kuwa symbolic tu, na nina uhakika kuwa mamilioni ya Watanzania wameandamana kimoyomoyo. Changamoto kubwa sasa ni kuhakikisha kuwa kiu ya Watanzania kuung’oa udikteta haipotei.

Naam, watadhihaki kuwa maandamano hayajatokea lakini kile ambacho hawatosema ni kwamba “badala ya wananchi kuandamana, polisi na jeshi ndo walioandamana” tena sio bure bali kwa gharama kubwa kwa serikali iliyo taaban kifedha.
View attachment 758277

Chanzo: “Tathmini: Dhamira Ya ‘Maandamano Ya Mange’ Imefanikiwa” @Chahali
Ukikubal kushindwa napo n uungwana

Kiukwel kashindwa,na kadhalilika.Tena n bora angeendelea kutumika nyuma ya keyboard kulko kujiuma uma alkojiuma ktk mahojiano

Kiukwel n kuwa wanaomtumia hawakufanya tathmin ya mwitikio wa watz ktk kuandamana.
So in short propaganda zilikuwa hazjazaa matunda ya kutufarakanisha kiasi cha kutaka kuipindua like arab spring in egypt, and the likes.
Screenshot_20180427-215317.jpg
 
Akili kubwa hii. Hongera kwa uchambuzi uliotulia.

Serikali haijajibu hoja za wananchi, wananchi wamejibiwa kwa Vitisho, Watch Out.....

Bomu litalipuka soon

Ajira zimepotea na sukari kutoka 1800 hadi 2800

Serikali inachezea FAO la Kujitoa na Mafao ya wastaafu...

Wafanyakazi hawajaongezewa mishahara miaka 3

Uchumi umedorora..Shillini ni 2290 Tshs kwa Dola moja

A - Rais wa nchi ameacha Shughuli nyingi sana na kumfikiria Dr. Mange
B - Vyombo vyote vya Dola Vikahangaika na Dr. Mange
C - Vyombo ya Kimataifa vimejua hali halisi ya Tanzania
D - Serikali inapambana na wananchi, Je nani wanamuunga mkono huyo Jiwe?
E- Kwa nini aogope maandamano kama anafanya vitu vizuri kwa wananchi, Na wanampenda

Tupo Gizani: Maswali na hoja za wananchi bado kujibiwa

1 - 1.5 Trillioni ziko wapi?

2- Uhuru wa habari na demokrasia?

3 - Unafungia social media lakini hunyongi mafisadi (Eti kama china)

4 - Mafao ya Jamii - CCM na Serikali yake imetafuna

5- Sukari Jiwe akapandisha kutoka 1800 hadi 2800

6- Uchumi Jiwe ameua

7 - Ajira hakuna kabisa

Kejeli za vilaza wachache wa Lumumba, haziwezi kuzima hoja hizo hapo juu.

Vijana wa Lumumba wanalipwa special allowance ili kulinda mkate wa wachache, wanao tafuna keki ya taifa

-Wanajua fika kuwa hoja zao ni dhaifu Mbele ya Jukwaa hili la JF ---Ndio maana Bwana mkubwa analalamika Watanzania kuamini mitandao ya Jamii

Pili, Ni wazi kuwa Mikataba Feki walioingia CCM na Serikali yake ndio wanaibia nchi hii. Bado Wezi na Mabwanyenye wanaiba sana, kwa akili nyingi..Kwa sababu Mikataba bado ipo

CCM wakaingia mkataba na CHina na gesi ya Mtwara haina faida tena

Hivi waliingia mikataba mibaya ya kufilisi nchi si bado wako CCM

Au je, Mahakama ya Mafisadi imefunga wangapi? Vijana wa Lumumba, endelezeni njaa na kuwasaliti Watanzania.
 
Back
Top Bottom