Tathimini ya “goli la mkono” kwenye uchauguzi mkuu ujao!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,967
22,476
Wanajamvi,

Humu ndani, nimegunduwa jambo moja. Pale inapokuja kwenye ugombea urais, majina mengine yanayotajwa tofauti na lile la mgombea wa CCM, kwa kiasi kikubwa, hawapewi nafasi haya kidogo! Sababu kubwa inayotumika, ni kwamba NEC itatangaza mgombea wake iwe iweje!

Lissu aliulizwa swali kama watashiriki uchaguzi mkuu chini ya mazingira yaliyopo. Akasema hawawezi kuacha kushiriki uchaguzi. Pamoja na wasiwasi ambao wananchi wengi walionao kuhusu uhuru wa tume ya uchaguzi na malalamiko ya “goli la mkono”

Hili likanifanya nijiulize kama walishawahi kulifanyia tathmini “goli la mkono”. Goli ambalo Nape alivunjika mkono akiwa kwenye kampeni na jitihada za kupiga goli hilo “la mkono”, na kuna tetesi kuwa hatoshiriki tena kwenye mchezo huo! Lakini hilo haliondoi ukweli kuwa bado kuna ambao ndani ya ccm watakaoucheza mchezo huo!

Je upinzani mmejipanga vipi? Nina amini kabisa kama siyo Lowassa, kungekuwa na vurugu kubwa za wananchi waliiona kuwa wamedhulumiwa!

Ni ukweli kuwa uchaguzi huu ujao utatupiwa jicho sana! Je ukitokea mchezo mchafu, nini kitafanyika kukabiliana na hali hiyo? Inashangaza sana kuona kuwa kuna watanzania wanaongea kwa kujiamnini kabisa hadi unajiuliza maswali kama uchaguzi ni jambo la muhimu chini ya mazingira kama hayo! Pamoja na kwamba watanzania ni waoga, bado ninatoa ushauri kuwa ccm msithubutu tena kupiga goli la mkono, maana mtajuuta na kupata taabu sana!
cc Nape Nnauye britanicca
 
Makaratasi mengi ya kura yatachapishwa, kupita namba ya waliojitokeza kupiga kura

Watanzania watapata kipigo cha mbwa koko...Watanzania watapata taabu saana
 
Hivi yale maandamano ya mange mliingia barabarani au mliogopa kupata taabu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hili ni tusi kwa wapenda manadiliko wa kweli. Nafahamu kabisa kuwa mnategemea sana uoga wa Watanzania. Lakini hamjui kuwa imeshatokea mara nyingi tu kuwa viongozi hao wa upinzani waliamuwa kuwatuliza! Kwa taarifa yako, Lowassa siyo wa kwanza. Nadhani hamjui moto atakaouwasha Tundu Lissu ndiyo maana mnaamini itakuwa business as usual. Nawapeni tu tahadhari.
 
Ccm inajiona kuwa wao ni wapenda amani lakini ni wachochezi wa fujo na wavunjivu wa haki za binadamu, ni wachokozi wanaoleta vita halafu wanasingizia vyama mbadala!
Wabaya sana.
 
Ali Hassan Mwinyi alisema, "watanzania/ Tanzania ni kichwa cha mwenda wazimu".
Kauli hii aliitoa wakati huo Timuya Taifa ya soka inapokea mkong'oto.

Bila ya Tume huru na Katiba mpya itakayoondoa kutohojiwa kwa matokeo ya kura za urais mahakamani na kuondoa kinga ya kutokuburuzwa mahakamani kwa Rais. Mgombea wa CCM ataendelea kutangazwa mshindi hata pale kura zisipotosha kumpatia nafasi ya urais. Mfano hai ni ule uchafu wa kumsimika Shein, mgombea wa CCM baada ya kupigwa chini kupitia kisanduku cha kura na goli la mkono la Nape lilimsukumiza mtu aliye-beep tu.

Karibuni nilimsikia Waziri mpya wa sheria akijisifu kwamba amesaidia kutengeneza katiba za mataifa matano. Kuna usanii utaanzishwa karibuni kama ile pipi ya Kikwete ya "Katiba mpya/ tume ya Warioba".

Wapinzani bado hawajaamua kudai tume huru ya uchaguzi, wacha tu CCM iendelee kufanya ujinga wa kuwafanya watanzania wajinga.
Well said mkuu! Nilishangazwa sana hata mimi kuhusu upinzani kutokudai tume huru na kushiriki uchaguzi! Labda wana plan B
 
Ali Hassan Mwinyi alisema, "watanzania/ Tanzania ni kichwa cha mwenda wazimu".
Kauli hii aliitoa wakati huo Timuya Taifa ya soka inapokea mkong'oto.

Bila ya Tume huru na Katiba mpya itakayoondoa kutohojiwa kwa matokeo ya kura za urais mahakamani na kuondoa kinga ya kutokuburuzwa mahakamani kwa Rais. Mgombea wa CCM ataendelea kutangazwa mshindi hata pale kura zisipotosha kumpatia nafasi ya urais. Mfano hai ni ule uchafu wa kumsimika Shein, mgombea wa CCM baada ya kupigwa chini kupitia kisanduku cha kura na goli la mkono la Nape lilimsukumiza mtu aliye-beep tu.

Karibuni nilimsikia Waziri mpya wa sheria akijisifu kwamba amesaidia kutengeneza katiba za mataifa matano. Kuna usanii utaanzishwa karibuni kama ile pipi ya Kikwete ya "Katiba mpya/ tume ya Warioba".

Wapinzani bado hawajaamua kudai tume huru ya uchaguzi, wacha tu CCM iendelee kufanya ujinga wa kuwafanya watanzania wajinga.
Hiyo sentenso ya kwanza imenikumbusha kauli ya The Boss kuhusu watanzania kumshukuru rais baada ya lile tukio la kupatwa kwa jua!🤦🏾‍♂️
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom