Tatafakari juu ya Tamko la Prof. Mwandosya

Tatafakari juu ya Tamko la Prof. Mwandosya

Umeongea point tupu,hakuna mtu safi kwenye huo ukoo wa panya! Yote manyani tu.

Huu ndio ushabiki wa kiasiasa tunaoukabili nchini na ambao hautatufikisha popote na unanisikitisha sana. Mtu anamchukia mwanasiasa fulani kwa kuwa tu hayuko kwenye chama anachoshabikia. Mtu hayuko tayari kupembenua zuri au baya analosema mtu huyu, iwe Bungeni au jukwaani, kwa sababu tu ni wa chama kingine asichoshabikia.

Na upande wa pili ni kwamba mtu anampenda tu mwanasiasa fulani, hata aongee au kufanya utumbo au ujinga wa namna
gani, yeye ataunga mkono na kushangilia kwa kuwa tu ni mtu wa chama anachoshabikia.

Mara nyingine nashindwa kuelewa, nani hasa ni mwendawazimu zaidi; yule anayeongea na kufanya uwendawazimu, au yule anayeshabikia uwendawazimu wa mwendawazimu.
 
Unaweza kutueleza huyo wandosya kafanya nini hapa Tz,toka aanze utumishi wake kafanya nini au kasimamia jambo gani likapata ufanisi mkubwa? Acheni porojo bwana!

Mkuu, una mtazamo uliopotoka sana kuhusu uraisi. Uraisi sio tuzo au medani wanayopewa watu waliotufanyia mambo mazuri hapa nchini.

Hata hivyo labda turudi nyuma kwa kutumia kigezo chako "katufanyia nini". Pale Mwinyi alipoteuliwa kuwa mgombea uraisi alikuwa amewafanyia nini Watanzania? Au hata Mkapa, na Kikwete, walikuwa wamewafanyia nini Watanzania kilichofanya wastahili kupewa nafasi ya kugombea Uraisi? Labda wewe unajua, mie sijui, na wala sikuona wwote hawa walichowafanyia Watanzania hadi kiwafanye wastahili uraisi. Lakini naelewa kwamba huenda walionwa kuwa na sifa za kuwa maraisi wetu, na sifa hizo hazikutia ndani kile walichokuwa wamewafanyia Watanzania.

Huenda kati ya Mkapa na Mrema, kwa kutumia kigezo chako Mrema alistahili kuwa raisi kuliko Mkapa - lakini swali la msingi ni kama Mrema alikuwa na sifa za uraisi zaidi ya Mkapa.

Hivyo basi, Magufuli anaweza akawa amesaidia sana kusimamia ujenzi wa barabara nchini na akastahili pongezi na wote tukasema Magufuli ametoa mchango mkubwa kwa Watanzania - sasa je tutamchagua Magufuli kuwa raisi kwa sababu alisimamia vizuri ujenzi wa barabara zetu? Toka lini kusimamia barabara inakuwa sifa ya kuwa raisi mzuri?

Katika mfano wa Tanzania kuwa kama wasafiri wa ndege niliotaja hapo juu; ukiuliza Mwandosya katufanyia nini ni sawa na mtu kusema mhudumu wa ndege aliyetudumia vizuri sana ndie anastahili kuchukua jukumu la kuwa pilot katika safari yetu.

Tutakuwa tumepotoka sana ikiwa tutadhani sifa ya kuwa raisi wa Tanzania ni kutokana na yale uliyowafanyia Watanzania. Wapo wengi waliowafanyia Watanzania mambo makubwa, tunawapongeza na huenda wanastahili medani. Lakini haina maana wana sifa ya kuwa maraisi wa Tanzania. Sifa za mtu kuwa raisi wa Tanzania ni kutia nani kuwa decisive, patriotic, assertive, visionary, wisdom, intelligence, exposure, diligence, leadership capability, kuheshimika na watu wa ndani na nje, kuheshimiwa na baraza la mawaziri na taasisi za serikali, nk. Nitakuwekea post juu ya hili ili ufanye tathmini.
 
Kama JK ameweza kuwa raisi basi hakuna anayeshindwa .

Kuwa raisi linaweza likawa jambo rahisi, na mtu yeyote akaweza. Lakini sasa, kupata raisi mwenye uwezo (capable president) ndio jambo la msingi hapa.

Sidhani kama Watanzania tumefikia hatua ya kuwa taifa la watu waliokata tamaa kiasi hiki.
 
Sina tatizo na Mwandosya. Wasiwasi wangu ni afya yake. Alishakaa India miezi kadhaa akipata matibabu na amekuwa akirudi India mara kwa mara kuhusu afya yake.
 
Sina tatizo na Mwandosya. Wasiwasi wangu ni afya yake. Alishakaa India miezi kadhaa akipata matibabu na amekuwa akirudi India mara kwa mara kuhusu afya yake.

Ikiwa yeye amesema amekwisha pona, na wewe na mie sio madaktari na wala hatujampima tukathibitisha kwamba afya yake bado sio nzuri, naona sio fair kukata shauri kwamba tuna wasiwasi na afya yake. Na kama ni kweli afya yake ilidhurika kutokana na mkono wa mtu, basi tutakuwa tunawapa ushindi wa chee hao waliomdhuru, maana tutakuwa tunatimiza lengo lao.
 
CCM haitatoa Rais itatoa wagombea wengi sana.

Unajua Mathias, kuna jambo hapa huwa linanisumbua sana. Ni wazi kwamba wengi wa watu walio "intellectuals" wamechoshwa na CCM, na wasingependa hata kufikiria CCM itatoa raisi ajaye. Lakini tatizo sasa ni kwamba, kwa aina ya wapiga kura tulio nao Tanzania, the best candidate ataketoka chama cha upinzani ana uwezo wa kushinda?

Binafsi siamini Kikwete alimshinda Slaa kwa sababu Kikwete ni kiongozi bora zaidi ya Slaa. Lilikuwa ni suala la aina ya wapiga kura tulio nao.

Mara nyingine nafikiri vyama vya upinzani wanapaswa kuwa pragmatic katika hili, wakitambua kwamba hata kama wana mteule bora sana wa kugombea uraisi bado anaweza kushindwa na mgombea wa CCM kutokana na mwamko mdogo wa kisiasa wa wapiga kura wa Ki-Tanzania.

Wapinzani wasing'ang'anie win-lose situation, wakiratarajia tu kushinda uraisi na CCM kushindwa. Wapinzani wanapaswa ufikiria pia win-win situation, ambapo hata kama wao wameshindwa basi angalau yule aliyeshinda kule CCM ni yule ambaye atakuwa raisi kupitia CCM lakini kwa manufaa ya watanzania wote, wa CCM na wasio wa CCM. Hivyo zaidi ya kushughulika na mgombea wao, vyama vya upinzani vinapaswa kujitahidi ku-influence apatikane mgombea wa CCM anayekubalika na upinzani, atakaefanya jazi kwa kuviheshimu vyama vya upnzani, japo yuko CCM.

La sivyo siku moja upinzani watakuta wameshindwa na mtu kama Mwigulu Nchemba, ambaye ninakuhakikishia akiwa raisi ataua vyama vyote vya upinzani nchini!
 
Back
Top Bottom