Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 15,107
- 28,608
Wiki iliyopita nilitoa post mbili ambazo kwa namna fulani zina mkaribio mkubwa na habari iliyotoka hivi karibuni kwamba Prof. Mwandosya ameonyesha nia ya kugombea uraisi. Nilisisitiza sana kwamba mimi sina ushabiki na Chama chochote cha siasa nchini, hasa pale wengi walipodhani nilikuwa nikimfanyia kampeni Makamba.
Post hizo zilisema;
1. Ushauri wa Bure kwa Kikwete Kuhusu Makamba Kutaka Kuwa Rais
2. Je unadhani Salim Ahmed Salim au Mwandosya wangefanya vizuri zaidi ya Kikwete?
Katika post yangu namba 1 wengi walidhani niko kambi ya Makamba, hasa pale niliposema Tanzania imenajisiwa sana kiuongozi na kupoteza heshima ya Ofisi ya Raisi, Bunge na Baraza la Mawaziri. Nikasema kwamba "ikiwa Makamba ana uwezo wa kurekebisha hili kwa hivi sasa, wale tulio na uchungu wa nchi yetu tutasema hewala, acha Makamba aje, ili mradi umri wake unaruhusiwa kikatiba. Kwetu sisi si busara kusema acha nchi iendelee kuharibika hadi Makamba afikishe umri aliokuwa nao JK alipopitishwa kuwa mgombea wa uraisi. Huo utakuwa ni wendawazimu. Kuendelea kungoja katika hali tuliyo nayo ni ku-compound uozo wa tatizo la kiuongozi linalotukabili kwa sasa. Suala la msingi ni kama Makamba ndiye desparate remedial solution tunayohitaji, na kama watu wenye akili hatutajadili umri wake katika hili ".
Katika post No2 kuhusu kama Mwandosya angekuwa Raisi badala ya JK nilisema kwamba "Kwa mtu kama Mwandosya nadhani tungeshuhudia mawaziri wengi wakifungwa au kufukuzwa kazi, na Takukuru na ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu kupewa uhuru na meno zaidi. Pia ninaweza kusema kwa uhakika kwamba chini ya JK tumekuwa na urafiki na mataifa mengi ya nje, lakini ni urafiki ambao haujapelekea sisi kuheshimiwa kama taifa bali urafiki wa kimaslahi kwa hao wanaojifanya rafiki zetu. Chini ya Mwandosya naona kama heshima yetu kama taifa ingepanda sana, na urafiki ungeimarishwa katika misingi ya kuheshimiana na sio kutumiwa. Kwa hiyo binafsi naona Mwandosya angekuwa makini na mkali zaidi ya JK. Mawaziri wangemheshimu sana na kumwogopa".
Basi nikiwa Mtazania mwenye mapenzi na uendelevu wa nchi yangu, ninachowasihi Watanzania wote walio CCM, Chadema NCCR, TLP na kwingineko, kuacha ushabiki wa kisiasa na kutafakari sana juu ya muelekeo wa nchi yetu katika kipindi hiki. Tutafakari tamko la Mwandosya kwa makini, hasa kuhusiana na niliyoandika hapa juu na katika post nilizotaja. Tanzania ni kubwa sana zaidi ya vyama vya siasa, na inapita katika kipindi muhimu sana kuelekea uchumi ambao unaweza ukaifanya kinara wa maendeleo katika Afrika, na hilo litawezekana tu tukiwa na mtu makini kama Raisi ajaye, anayeweza kuheshimiwa sana na wananchi, mawaziri wake, na watendaji wa serikali, na vile vile viongozi wa mataifa ya nje.
Mbele yetu tuna nafasi ya kipindi cha miaka kumi cha kutembea kifua mbele kama Watanzania, au kujutia uamuzi tuliofanya kwa misingi ya ushabiki wa kisiasa, uliofanya tuamue mambo kutokana na misingi ya uchama, makundi, ukabila, udini, uzee au ujana kama watu wasio na akili timamu.
Post hizo zilisema;
1. Ushauri wa Bure kwa Kikwete Kuhusu Makamba Kutaka Kuwa Rais
2. Je unadhani Salim Ahmed Salim au Mwandosya wangefanya vizuri zaidi ya Kikwete?
Katika post yangu namba 1 wengi walidhani niko kambi ya Makamba, hasa pale niliposema Tanzania imenajisiwa sana kiuongozi na kupoteza heshima ya Ofisi ya Raisi, Bunge na Baraza la Mawaziri. Nikasema kwamba "ikiwa Makamba ana uwezo wa kurekebisha hili kwa hivi sasa, wale tulio na uchungu wa nchi yetu tutasema hewala, acha Makamba aje, ili mradi umri wake unaruhusiwa kikatiba. Kwetu sisi si busara kusema acha nchi iendelee kuharibika hadi Makamba afikishe umri aliokuwa nao JK alipopitishwa kuwa mgombea wa uraisi. Huo utakuwa ni wendawazimu. Kuendelea kungoja katika hali tuliyo nayo ni ku-compound uozo wa tatizo la kiuongozi linalotukabili kwa sasa. Suala la msingi ni kama Makamba ndiye desparate remedial solution tunayohitaji, na kama watu wenye akili hatutajadili umri wake katika hili ".
Katika post No2 kuhusu kama Mwandosya angekuwa Raisi badala ya JK nilisema kwamba "Kwa mtu kama Mwandosya nadhani tungeshuhudia mawaziri wengi wakifungwa au kufukuzwa kazi, na Takukuru na ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu kupewa uhuru na meno zaidi. Pia ninaweza kusema kwa uhakika kwamba chini ya JK tumekuwa na urafiki na mataifa mengi ya nje, lakini ni urafiki ambao haujapelekea sisi kuheshimiwa kama taifa bali urafiki wa kimaslahi kwa hao wanaojifanya rafiki zetu. Chini ya Mwandosya naona kama heshima yetu kama taifa ingepanda sana, na urafiki ungeimarishwa katika misingi ya kuheshimiana na sio kutumiwa. Kwa hiyo binafsi naona Mwandosya angekuwa makini na mkali zaidi ya JK. Mawaziri wangemheshimu sana na kumwogopa".
Basi nikiwa Mtazania mwenye mapenzi na uendelevu wa nchi yangu, ninachowasihi Watanzania wote walio CCM, Chadema NCCR, TLP na kwingineko, kuacha ushabiki wa kisiasa na kutafakari sana juu ya muelekeo wa nchi yetu katika kipindi hiki. Tutafakari tamko la Mwandosya kwa makini, hasa kuhusiana na niliyoandika hapa juu na katika post nilizotaja. Tanzania ni kubwa sana zaidi ya vyama vya siasa, na inapita katika kipindi muhimu sana kuelekea uchumi ambao unaweza ukaifanya kinara wa maendeleo katika Afrika, na hilo litawezekana tu tukiwa na mtu makini kama Raisi ajaye, anayeweza kuheshimiwa sana na wananchi, mawaziri wake, na watendaji wa serikali, na vile vile viongozi wa mataifa ya nje.
Mbele yetu tuna nafasi ya kipindi cha miaka kumi cha kutembea kifua mbele kama Watanzania, au kujutia uamuzi tuliofanya kwa misingi ya ushabiki wa kisiasa, uliofanya tuamue mambo kutokana na misingi ya uchama, makundi, ukabila, udini, uzee au ujana kama watu wasio na akili timamu.