TARIME: Watu wawili wafariki baada ya kuangukiwa na kifusi katika machimbo madogo ya dhahabu

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Watu wawili wamefariki dunia kwa kufukiwa na kifusi cha udongo wakati wakichimba madini ya dhahabu katika machimbo madogo yaliyoko mtaa wa Buguti Kata ya Turwa wilayani Tarime.

Akizungumza Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe amesema tukio hilo limetokea Jumapili Agosti 5 na kuwataja waliofariki kuwa ni Bisaku Chacha (19) na Charles Mairo (18).

Amesema marehemu waliingia kwenye shimo lililokuwa limeachwa kwa siku nyingi wakitafuta mawe ya dhahabu matokeo yake waliangukiwa na mawe hayo.

Mzazi wa Charles, Mairo Wembe amesema hakuziamini taarifa za mwanae kufariki dunia, baada ya kurejea nyumbani ndio aliamini.
 
Back
Top Bottom