Tanzanite One Mining kuachisha kazi wafanyakazi 600

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,931
31,176
Heshima kwenu wanajamvi,

Habari mbaya kwa machalii & wanaApollo wa miji ya Arusha na Kilimanjaro.Nimepenyezewa taarifa za uhakika kwamba kampuni ya uchimaji wa madini ya vito (Tanzanite) itapunguza wafanyakazi 600 wakati wowote kuanzia sasa ili kukabiliana na hali mbaya ya fedha uliyoikumba kampuni hiyo tangu ilipochukuliwa na wafanyabiashara wazawa Hussein Gonga na Faisal Shahbhai raia wa Tanzania mwenye asili ya kiasia (Hindi).

Hali ya uzalishaji imezidi kuwa mbaya hasa baada ya wataalam wengi kuondoka baada ya kushindwa kufanyakazi chini ya uongozi mpya uliojaa ubabaishaji na ukosefu wa ujuzi wa kutosha wa kuedesha migodi mikubwa.Huduma nyingi hasa chakula,usafiri na nk zimekuwa zikisuasua kwa muda mrefu.Madeni makubwa ya wazabuni mbali mbali limekuwa tatizo kubwa na kusababisha kuzorota kwa uzaishaji wa madni hao hadimu duniani yanayopatikana Tanzania tu.

Mara kadhaa nimekuwa nikileta mabadiko yanayohusiana na kudorora kwa uzalishaji wa mgodi huo uliokuwa ukiingizia serekali mapato makubwa.

Waziri wa madni kipindi milki ya mgodi ilipohamishiwa kwa wazawa wababaishaji Mheshimiwa Simbachawene alionywa juu ya uwezo na ujuzi wa wamiliki wapya lakini hakutilia maanani kwasababu ambazo anazijua mwenyewe.
 
Sawa umefurahi au umesikitika dadavua kiduchu.

Mimi nimefurahi...walikua wanasumbua sana tukikutana nao maeneo ya kujidai.
Kuna wale niligombana nao pale Midway hotel-hope hawatapoma.
 
Tulimwambia ridhiwani hana ujuzi wa kuendesha hii kampuni wao wakakomaa wakaamini wahindi watawasaidia. Waliona jenerali Mboma alikuwa na mgodi wakadhani ni kama kuvua dagaa ziwani.
 
Tulimwambia ridhiwani hana ujuzi wa kuendesha hii kampuni wao wakakomaa wakaamini wahindi watawasaidia. Waliona jenerali Mboma alikuwa na mgodi wakadhani ni kama kuvua dagaa ziwani.

Ahahahahaaaaaaa...Riz 1,...hivi Mwalusamba bado yupo na hizi deal.
 
Najua wanasifa za kijinga kuna rafiki yangu namwonea huruma sana kwasababu ana watoto wadogo watatu wa kwanza ndio yuko form 1 wa pili std 1 watatu anatambaa.Ebu niambie na jamaa nina hakika hana ujuzi wowote zaidi ya kunywa beer na kufukuzia wanawake.


Ngongo hawa wajinga wana masifa ya kipuuzi sana mkuu.
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Habari mbaya kwa machalii & wanaApollo wa miji ya Arusha na Kilimanjaro.Nimepenyezewa taarifa za uhakika kwamba kampuni ya uchimaji wa madini ya vito (Tanzanite) itapunguza wafanyakazi 600 wakati wowote kuanzia sasa ili kukabiliana na hali mbaya ya fedha uliyoikumba kampuni hiyo tangu ilipochukuliwa na wafanyabiashara wazawa Hussein Gonga na Faisal Shahbhai raia wa Tanzania mwenye asili ya kiasia (Hindi).

Hali ya uzalishaji imezidi kuwa mbaya hasa baada ya wataalam wengi kuondoka baada ya kushindwa kufanyakazi chini ya uongozi mpya uliojaa ubabaishaji na ukosefu wa ujuzi wa kutosha wa kuedesha migodi mikubwa.Huduma nyingi hasa chakula,usafiri na nk zimekuwa zikisuasua kwa muda mrefu.Madeni makubwa ya wazabuni mbali mbali limekuwa tatizo kubwa na kusababisha kuzorota kwa uzaishaji wa madni hao hadimu duniani yanayopatikana Tanzania tu.

Mara kadhaa nimekuwa nikileta mabadiko yanayohusiana na kudorora kwa uzalishaji wa mgodi huo uliokuwa ukiingizia serekali mapato makubwa.

Waziri wa madni kipindi milki ya mgodi ilipohamishiwa kwa wazawa wababaishaji Mheshimiwa Simbachawene alionywa juu ya uwezo na ujuzi wa wamiliki wapya lakini hakutilia maanani kwasababu ambazo anazijua mwenyewe.

Tunaenda kushuhudia ongezeko la vibaka Moshi na Arusha............!!!!!!!
 
Duh akili mkichwa sasa
Wakizubaa mtaani itawaghalimu waongeze maarifa ili kukidhi mahitaji ya familia zao.


OVER
 
Duh kweli hali si hali vijana wengi wameingia kitaa siku hizi wana heshima kweli kweli.
 
Tanzanite One bado hakijaeleweka vijana wengi wamekuwa wazururaji na omba omba.
 
Huu mkataba waHawa wawekezaji mpya usitishwe Mara moja ... Watafutwe wawekezaji wa ukweli wenye kuweza kuendesha huu mgodi wataoweza kulipa kodi vizuri na kutengeneza ajira nyingi kwa vijana.... Shida ya huu mgodi wakubwa wengi ndio wamejifichia Hapo kwa mgongo wa wekezaji uchwara wakibongo wanaouendesha kwa sasa..
 
Tulimwambia ridhiwani hana ujuzi wa kuendesha hii kampuni wao wakakomaa wakaamini wahindi watawasaidia. Waliona jenerali Mboma alikuwa na mgodi wakadhani ni kama kuvua dagaa ziwani.

Mengi ana migodi ana walipa watu 3000 kama vibarua ,na mamenaja wake ndio haohao wahindi wa bonite
 
Back
Top Bottom