Tanzania's Sovereign Wealth Fund

Tanzania's Sovereign Wealth Fund

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,654
Reaction score
6,594
Wakati wa awamu ya Kikwete nakumbuka kuna wazo lilikuwa linafanyiwa kazi la kuanzishwa kwa Tanzania's Sovereign Wealth Fund ili mapato mbalimbali ya serikali, hasa kutoka kwenye sekta za mafuta na gesi yangewekezwa kwenye vitega uchumi mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Nchi nyingi, hasa zenye maliasili ya kutosha zimefungua na zinaendesha fund ya namna hii, mfano Qatar, UAE, China na Norway. Nadhani hata Ghadhafi alikuwa kwenye pilikapilika za kuanzisha kitu kama hiki kwa ajili ya Libya.

Kwa Tanzania hili wazo sijalisikia kwa muda, sijui lilifia wapi.
 
Hii kitu imewapaisha sana Norway! Tatizo la nchi yetu Mipango mingi utekelezaji 0.

Hii kitu ingetusaidia sana hata sasa kutokana na mapato ya madini. Sidhani kama tunawekeza kwenye vitu endelevu na vyenye ROI nzuri.

Mimi nadhani ningefaa sana kuisimamia hii, ni mzalendo, muadilifu, mchapa kazi. Ngoja niweke namba yangu ya simu hapa chini.
 
Hili wazo kila nikiuliza limefikia wapi nasikia kimya kizito.

Mwezi February mwaka huu 2025, Rais Trump alipoingia tu madarakani akasaini executive order ya mpango wa kuanzisha United States Sovereign Wealth Fund.

Kama wahusika wananisikia, naomba sana walirudie hili wazo na wawekwe watu waadilifu wa kulisimamia.

Mimi niko tayari kutoa mchango wangu katika hili wazo.
 
Hili wazo kila nikiuliza limefikia wapi nasikia kimya kizito.

Mwezi February mwaka huu 2025, Rais Trump alipoingia tu madarakani akasaini executive order ya mpango wa kuanzisha United States Sovereign Wealth Fund.

Kama wahusika wananisikia, naomba sana walirudie hili wazo na wawekwe watu waadilifu wa kulisimamia.

Mimi niko tayari kutoa mchango wangu katika hili wazo.

Ni wazo zuri sana endapo litatekelezwa
 
Huu uzi huwa haupati wachangiaji ila siri ya mafanikio ya kweli ya Tanzania imejificha katika wazo hili kama litatekelezwa kwa uadilifu na nidhamu ya hali ya juu.

Leo nimeona clip ya Prof. Muhongo akiibua tena wazo la Wealth Fund.
 
Back
Top Bottom