Tanzania ya viwanda yageuka kuwa Tanzania ya vituo vya mafuta

Kulwa Jilala

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
3,510
7,755
Bila shaka sasa Tanzania mpya iliyokuwa inameremeta kwa ujenzi wa viwanda kila kona ya nchi, sasa imegeuka kuwa Tanzania ya ujenzi wa vituo vya mafuta kiholela na kila sehemu!

Sheria inataka ujenzi wa kituo cha mafuta uwe mita 500 kutoka kimoja hadi kingine lakini sheria hii haifuatwi tena. Kuanzia mwaka 2021 vituo vya mafuta vinaota kama uyoga kwenye nchi yetu. Swali la kujiuliza kimetokea nini?

Mkoa wa Pwani ulikuwa unaongoza kwa ujenzi wa viwanda vingi sana lakini sasa hivi wakifanya utafiti upya watakuta unaongoza kwa ujenzi holela wa vituo vya mafuta.
 
Tanzania tuna changamoto sana kwenye suala la kuamua innovative and sustainable development goals, ndio maana kila mtu akijenga nyumba anafikiria kutengeneza frame mbele ya nyumba, the same hata watu wenye pesa kadhaa siku hizi wanadhani ukiwa na millioni 200 the only thing to do ni kuweka vituo vya mafuta wakati the fact is in next 20 to 30 years, matumizi ya mafuta na fossils fuel yatapungua sana hasa kwenye kuendeshea mitambo na engine.

Pia ndio maana serikali bado inaweka tozo na kodi kwenye miamala ya simu na benki alafu mwisho wa mwezi waaanza kukimbizana na watu kuhusu kodi, endapo watu wengi wangekuwa wanalipia kwa njia za mitandao ingewasaidia wao kwenye kujua na pesa kiasi ngapi ambazo watu wana trade tena kwa taarifa sahihi kabisa.
 
Rushwa imetawala sana awamu hii.Ukiwa na pesa za kutosha unapata eneo lako zuri pale ukuta wa ikulu unajenga kituo chako cha mafuta na hakuna mtu atakusumbua.kwa sasa sheria hazifuatwi.
 
Back
Top Bottom