Tanzania ya Magufuli ilikuwa ya kimafia

NTIGAHELA

JF-Expert Member
Jan 1, 2014
362
254
KISIASA, Mafia State humaanisha nchi kuwa na serikali jambazi. Ama inatenda uhalifu moja kwa moja kupitia vyombo vyake au inaendesha makundi hatari ya uhalifu.

Jana, Rais Samia alieleza kuhusu fedha za watuhumiwa wa kesi za uhujumu uchumi kufichwa China. Ni zile watu walilipishwa ili kununua uhuru wao kupitia makubaliano ya kufupisha mlolongo wa kesi na punguzo la adhabu, yaani plea bargain.

Baada ya Rais Samia, raia namba moja na Amiri Jeshi Mkuu, kutamka kwa ulimi wake kwamba fedha za plea bargain zilipigwa, sasa tupo kwenye wakati mzuri kuhitimisha kwamba nchi ilikuwa na serikali jambazi. Tanzania ilikuwa Mafia State.

Kesi za uhujumu uchumi ziligeuzwa chanzo cha mapato ya nchi. Watu walitishwa kukubali makosa vinginevyo wangeozea jela. Vile kesi hizo hazina dhamana. Basi, mtuhumiwa akatakiwa achague kutoa pesa au kuzoea maisha ya nyuma ya nondo.

Namfahamu mzee aliyefuatwa na kuambiwa kampuni yake iliacha deni la Yen za Japan 3,000 (Sh53,000). Deni hilo likapigwa faini kutoka Sh53,000 hadi kuwa Sh72 milioni. Akaambiwa alipe au akawe mgeni wa jela kwa kesi ya uhujumi uchumi.

Mzee hakuwa na pesa. Alishanyang'anywa kiwanda na nyumba mbili. Ikabidi aitishe michango ya ndugu. Walipoanza kulipa, walielekezwa kuingiza malipo kwenye akaunti binafsi.

Huo ukawa mwendo. Kampuni zilipewa mzigo wa faini za kodi, kisha fedha zikalipwa akaunti za watu binafsi.

Ilikuwa Mafia State. Polisi hadi JWTZ walitumika kudhulumu haki. Wenye maduka ya kubadili fedha walifilisiwa ndani ya saa chache. Walinyang'anywa fedha zao benki. Ofisi zao zikafungwa.

Ilikuwa serikali jambazi. Watu waliokuwa na fedha nyingi benki, walishangaa salio linasoma sifuri. Wafanyabiashara wengi wakaogopa kuweka pesa benki.

Serikali inayopora raia ni jambazi. Kwa bahati mbaya sana, Watanzania walisalitiwa. Walijua wana serikali, kumbe lilikuwa genge la wahalifu. Hawakuona aibu kuiba na kudhulumu.

Naijua story ya kiwanda cha uchapaji cha Business Printers Limited (BPL), kilivyoporwa, kisha kikawa kinachapa magazeti ya Cyprian Musiba bure. Hata kura za Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020, zilichapwa BPL kwa dhuluma. Wenye kiwanda wamefilisika hadi leo.

FB_IMG_1675277651192.jpg
 
KISIASA, Mafia State humaanisha nchi kuwa na serikali jambazi. Ama inatenda uhalifu moja kwa moja kupitia vyombo vyake au inaendesha makundi hatari ya uhalifu...
Watanzania nyinyi wengi wenu ni wapumbavu tu, siku za majuzi majuzi ilikuwa, serikali ya JPM haina pesa za kuendeshea nchi na miradi yake haitaenda, TRA wanapika data, nchi imefilisika, Hazina hakuna pesa!

Leo tena ambaye alikuwa akipika data za makusanyo, Hazina hakukuuwa na pesa, nchi ilielekea kufilisika eti ni mwizi wa matrion!

Zilitoka wapi tena za kuiba hizi ambazo awali mlimsema hakusanyi ni mpaka data?

Hivi mnajua mnachekesha
 
Watanzania nyinyi wengi wenu ni wapumbavu tu, siku za majuzi majuzi ilikuwa, serikali ya JPM haina pesa za kuendeshea nchi na miradi yake haitaenda, TRA wanapika data, nchi imefilisika, Hazina hakuna pesa...
Ficha ujinga wako, kuna kupora fedha za watu binafsi na kupora fedha za umma. Usichanganye hayo mambo. Data alikuwa anapika wala hilo halina mjadala. Yaani kama ndio uko hapa kumtetea dhalimu basi umepoteza pambano mapema sana.
 
Ficha ujinga wako, kuna kupora fedha za watu binafsi na kupora fedha za umma. Usichanganye hayo mambo. Data alikuwa anapika wala hilo halina mjadala. Yaani kama ndio uko hapa kumtetea dhalimu basi umepoteza pambano mapema sana.
unakipaji cha kichekesho, utafika mbali usikate tamaa!
 
Mimi nadhani Rais angepaswa kuhakikisha kuwa wananchi wake wanakuwa na maisha nafuu badala ya kuturudisha nyuma kila siku.

Naona kama vile Rais wetu hajui anapaswa kufanya nini katika hiyo ofisi yake maana anachokifanya sasa ni kupiga majungu tu.

Ni aibu sana kuwa na Rais ambaye hatimizi majukumu yake na anakalia kupiga majungu tena anampiga majungu marehemu.
 
JPM (R. I. P). Yani haupo nasi, ila una trend kuliko hata walio hai. Hakika ulikuwa shujaa wa Africa.Jina lako litatajwa katika vizazi vingi vijavyo.
Aldolf Hitler hayupo kitambo ila bado anatrend hadi leo
Margreth thatcher anatrend lakini sio kwa wema pia
Osama bin laden hali kadhalika
Umaarufu unaweza kuwa positive au negative, Jiwe atatrend sana but not in a good way
 
Zilitoka wapi tena za kuiba hizi ambazo awali mlimsema hakusanyi ni mpaka data?
Hivi hujasoma uzi ukaelewa? Mleta mada kasema yule shetani alikuwa anapora fedha za watu kwa kufanya uhalifu wa kuwabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi.

Hivyo akawa anawataka wachague kufia jela ama kulipa mabilioni.

Wakichagua mabilioni shetani yule anayakwapua kwa kuyaficha China kwenye akaunti binafsi. Sasa wizi siyo makusanyo halali ya serikali. Umeelewa????


Jiwe alikuwa mwizi sana
 
Back
Top Bottom