Tanzania ni ya kwetu sote

Tanzania ni ya kwetu sote

Charliemic

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2019
Posts
604
Reaction score
979
Awali ya yote nipende kuwasalumu nyote! Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutuchagua na kutufanya tuitwe watanzania. Ni nchi ya kipekee duniani hivyo tuna kila sababu ya kutembea vifua mbele na kujivunia utanzania.

Baada ya kusema hayo niingie kwenye maada kwa kusema Tanzania ni nchi yetu sote kila mmoja pasipo kujali vyama vya siasa dini au kabila. Kila mmoja ana haki sawa hakuna mwenye haki zaidi ya wenzake!

Kila mmoja wetu ana wajibu wa kuijenga nchi yetu! Kwa namna moja au nyingine! Lakni katika kujenga huko haipaswi kulimuiza kundi fulani au tabaka fulani.

Hatupingani na kodi au mchango wowote kwa ajili ya maendeleo lakini tatizo ni kuwa serikali isitukamue kweli kweli! Haya makato kwa ajili ya solidarity fund ni makubwa mnoo

Serikali sikilizeni Julio chetu angalau mkayashusha. Ili sote tushiriki kuijenga nchi bila maumivu. Tusijifiche nyuma ya kivuli cha kodi! Ukweli ni kwamba hayo makato ni makubwa mnooo
 
Back
Top Bottom