EDWIN BAJUNGU
New Member
- Jun 8, 2020
- 4
- 3
Amka Tanzania, amka kutoka katika usingizi bandia. Kaeni macho, kuweni chonjo, sasa semeni kuibiwa basi.
Wametuibia sana, wametunyonya sana, wameigeuza Tanzania shamba la bibi. Wametajirika kwa rasilimali zetu.
Ndiyo wametajirika kwa madini yetu, wanyama wetu, malighafi kutoka katika mashamba yetu, mifugo na samaki wetu. Sasa tunasema kuibiwa tena basi.
Madini tutachimba wenyewe, hatukubali tena ulaghai kuwa tuna teknolojia ndogo hatuwezi kuchimba madini wenyewe.
Ulaghai huo hauna nafasi tena kwani wachimbaji wetu wadogo wamefanikiwa kupata madini mengi na makubwa kuliko yaliyowahi kupatikana kupitia wawekezaji wageni.
Wachimbaji wadogo wamelipa kodi vizuri na serikali kupata mapato makubwa kuliko yaliyowahi kupatikana kutoka kwa wawekezaji wageni.
Tanzania ni nchi Tajiri sana, utajiri wetu lazima tuulinde. Lazima wananchi wetu wafaidi utajiri wa nchi yao Tanzania.
Ni muhimu kuulinda utajili wetu usiporwe na wanyonyaji, mafisadi, mabeberu na vibaraka wao.
Ndiyo maana tunamuhitaji Rais John Pombe Magufuli ili atuongoze kulinda na kudhibiti utajiri wetu usiporwe.
Wametuibia sana, wametunyonya sana, wameigeuza Tanzania shamba la bibi. Wametajirika kwa rasilimali zetu.
Ndiyo wametajirika kwa madini yetu, wanyama wetu, malighafi kutoka katika mashamba yetu, mifugo na samaki wetu. Sasa tunasema kuibiwa tena basi.
Madini tutachimba wenyewe, hatukubali tena ulaghai kuwa tuna teknolojia ndogo hatuwezi kuchimba madini wenyewe.
Ulaghai huo hauna nafasi tena kwani wachimbaji wetu wadogo wamefanikiwa kupata madini mengi na makubwa kuliko yaliyowahi kupatikana kupitia wawekezaji wageni.
Wachimbaji wadogo wamelipa kodi vizuri na serikali kupata mapato makubwa kuliko yaliyowahi kupatikana kutoka kwa wawekezaji wageni.
Tanzania ni nchi Tajiri sana, utajiri wetu lazima tuulinde. Lazima wananchi wetu wafaidi utajiri wa nchi yao Tanzania.
Ni muhimu kuulinda utajili wetu usiporwe na wanyonyaji, mafisadi, mabeberu na vibaraka wao.
Ndiyo maana tunamuhitaji Rais John Pombe Magufuli ili atuongoze kulinda na kudhibiti utajiri wetu usiporwe.