Tanzania ni Jamii isiyojifunza wala kuelimika

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,064
Majanga ya kiasili yanatajwa ni miongoni mwa matukio ambayo ni vigumu sana kujikinga nayo kwa 100%, kwa sababu mengi hutokea katika scale kubwa na hivyo kuwanyima watu sehemu ya kukimbilia.

Hata hivyo, mataifa mbalimbali, yakipatwa na majanga hayo, hujitahidi kuyatumia majanga hayo kama msingi wa kujilinda dhidi ya mengine ya namna hiyo endapo yakitokea tena. Katila kufikia hilo, mambo mbalimbali hufanyika, kama vile:

1) Kuangalia maeneo mengine yaliyo prone kwa janga kama lililotokea.

2) Kutengeneza mifumo thabiti ya predictions na uokoaji kama endapo yakitokea tena eneo jingine.

Je, sisi Tanzania, majanga ya awali yamekuwa yanatufunza chochote?

Landslide iliwahi kutokea miaka ya nyuma huko Same. Watu walipoteza maisha na mali. Landslide kubwa na mbaya zaidi ilitokea huko Uganda, tulishuhudia na tukaenda kutoa pole kwa hawa majirani zetu.

Kwa upande wetu Tanzania, janga lile lile lililokuwa limetokea Same, limetokea Hanang, tena kwa scale kubwa zaidi. Watu wamepoteza maisha na mali, na uwezo wetu wa uokozi bado upo duni vilevile kama ilivyokuwa wakati ule, na mipango yetu ya makazi imeendelea kuwa holela vile vile kama ilivyokuwa siku hizo za nyuma.

Angalia miji kama Mwanza. Fikiria siku likitokea hata tetemeko dogo la ardhi, jinsi yale mawe makubwa yasiyo na mzizi yaliyo juu ya vilima, yatakapoporomoka kushuka chini.

Ifikirie pia Dodoma, mji mkuu uliobuniwa na wanasiasa bila ya kuwashirikisha wataalam. Dodoma ipo kwenye Rift Valley, hizi ni deep rooted structures ambazo zinalifanya eneo la Dodoma kuwa earthquake prone. Wanasiasa waliposhituliwa kuwa eneo ni hatari kwa matetemeko, CDA wakati huo ikatoa mwongozo kuwa majengo yote ya ghorofa Dodoma, yasizidi ghorofa 3. Leo maelekezo hayo yamepuuzwa au yamefutwa kimyakimya, na inaonekana unaweza kujenga jengo la urefu wowote. Tena jengo la Waziri mkuu lipo juu mlimani, juu ya mawe, labda wanataka likitokea tetemeko, yeye awafikie wahanga wengine kwa kutokea juu.

Watawala na wapanga mipango na miji yetu, sijui ni kwa kukosa maarifa, kukosa akili, au ni kwa uzembe au kwa kupuuza, hawajui kuwa maafa makubwa ya matetemeko ya ardhi, hasa epicenter inapokuwa nchi kavu, yanasababishwa na majengo marefu.

Hii nchi, kama watu wataendelea kupeana vyeo kwa kuangalia ni nani chawa wa Rais, ni nani chawa wa CCM, au ni nani kada mzuri wa CCM, hakika hakuna mahali popote au eneo lolote tutakalofanikiwa.

Poleni sana wafiwa na waathirika wote wa landslide ya Hanang. Lakini inasikitisha zaidi kwa sababu tuna mazingira yanayopalilia majanga mengi ya aina hiyo na aina nyingine kuendelea kutokea katika miaka ijayo.
 
Subiri usikilize kauli za kisiasa siasa!!!
Pale unapotarajia misingi ya kitafiti kuboresha emergency preparedness & emergency evacuation utaishia kusikia viapo, tambo na majigambo!
Ya Hanang' yataisha na tutasahau
Sehemu nyingine ikishika moto itasolviwa kama jambo jipya!
 
Viongozi wa Tanzania na Watanzania wenyewe, wemesha vuka kiwango cha ujinga na sasa wapo katika kiwango cha upumbavu.Na Mwl.Nyerere kasha wahi sema

"Upumbavu ni kama urefu na ufupi,huwezi muelimisha mpumbavu akaacha upumbavu wake"

Tukio hilo ni mbaya sana,kwa sababu limegusa maisha (roho),Mali na uharibifu wa miundombinu,lakini viongozi wamefanya kama sehemu ya kwenda kujionesha kwa ufahari wa magari na kupiga picha.

Shame on us na hopeless kabisa.
 
Subiri usikilize kauli za kisiasa siasa!!!
Pale unapotarajia misingi ya kitafiti kuboresha emergency preparedness & emergency evacuation utaishia kusikia viapo, tambo na majigambo!
Ya Hanang' yataisha na tutasahau
Sehemu nyingine ikishika moto itasolviwa kama jambo jipya!
Na mbaya zaidi serikali hii hii,huchukua mpaka pesa za wahanga bila aibu wala chembe ya huruma rejea ya mkoa wa Kagera.
 
Huwa najiuliza, mipango miji wanapogawa viwanja juu ya milima au mabondeni kama ilivyo Mwanza, Dar es salaam, Kibondo Same na Arusha, huwa wanatumia vigezo gani vinavyohakikisha usalama wakati wa mafuriko, milipuko ya volcano au landslides?

Mwanza ni moja ya eneo lenye miamba hatarishi ambayo siku moja itaporomoka na kupeleka watu kuzimu, lakini watu wameruhusiwa kujenga kama kwamba ni salama, Likitokea janga kama la Hanang tutamlaumu Mungu? 🧐
 
Viongozi wa Tanzania na Watanzania wenyewe, wemesha vuka kiwango cha ujinga na sasa wapo katika kiwango cha upumbavu.Na Mwl.Nyerere kasha wahi sema

"Upumbavu ni kama urefu na ufupi,huwezi muelimisha mpumbavu akaacha upumbavu wake"

Tukio hilo ni mbaya sana,kwa sababu limegusa maisha (roho),Mali na uharibifu wa miundombinu,lakini viongozi wamefanya kama sehemu ya kwenda kujionesha kwa ufahari wa magari na kupiga picha.

Shame on us na hopeless kabisa.
Tuna viongozi wajinga sana nchi hii.

Kuna wakati mmoja nilishuhudia kwa macho yangu:

Kuna mabasi mawili yalibeba wanakwaya akina mama toka Kenya. Maeneo yale ya karibia na maeneo yale ya Mkata basi moja lilitumbukia bondeni. Jingine likaja kupaki barabarani, na abiria wa basi hili la pili wakawa wanawaokoa majuruhi kwa kuwahamisha toka lile basi lilitumbukia bondeni na kuwaweka kwenye basi jingine. Polisi nao wakawa tayari wamefika. Kuna lorry lilikuwa limetoka Tanga, likaja likaligonga lile basi liliokuwa barabarani, na kuwapitia waokoaji wale wote. Ajali ilikuwa mbaya sana.

Kilichotokea, baada ya taarifa kufika mkoani, pale Kibaha. Mkuu wa mkoa akatoka na V8 lake bila ya madaktari. Ajali ilitokea saa 11 alfajiri, mimi nilifika eneo la tukio saa 2 asubuhi, majeruhi na marehemu walikuwa bado wapo chini wamelazwa bila ya msaada kwa maelezo kuwa madaktari wamekpsa usafiri. Lakini mkuu wa mkoa yupo pale na V8 lake. Kawahi kupiga picha na kuonesha kuwa amewahi haraka kugika eneo la tukio, badala ya yeye kama kiongozi mkuu wa mkoa kuhakikisha waokoaji wamefika eneo la tukip haraka, kakurupuka yeye kuwahi kupiga picha!!
 
Na mbaya zaidi serikali hii hii,huchukua mpaka pesa za wahanga bila aibu wala chembe ya huruma rejea ya mkoa wa Kagera.

Tukio lile la Serikali kuchukua pesa iliyochangwa na wahanga, lilikuwa la laana kubwa. Ni kama Serikali ilifurahia kwa sababu ililifanya janga kama chanzo cha mapato ya serikali.
 
Na mbaya zaidi serikali hii hii,huchukua mpaka pesa za wahanga bila aibu wala chembe ya huruma rejea ya mkoa wa Kagera.
Ila kusema kweli mtu yule alikuwa mwovu sana,alizifinya hela za rambirambi na misaada kisha akawatukana Wahaya kuwa wao ni nuksi kwani kila baya linawakuwata wao,ukimwi,ugonjwa wa minyauko ya migomba na kijiji kuitwa Katerero na mto kuitwa Katerangoma. Na akamalizia kuwa Serikali haitatoa hata senti kwa vile siyo ilileta tetemeko na wala yeye kwenye kampeni hajawaahidi kuwaletea tetemeko.
 
Mkuu upo sahihi, lakini tambua kuwa wahusika hawana Habari na wala hawajali lolote.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Muokoaji ndani ya suti kachomekea kabisa.

Uongozi ni mfano hawa wanatoa mfano gani?

Hawa walikuja kufanya maigizo tu .
1701684846573718-0.jpg
 
Back
Top Bottom