Tanzania na Huduma ya kwanza

Tanzania na Huduma ya kwanza

KILYA BIYE

Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
52
Reaction score
12
Ajali zinapotokea barabarani, nyumbani, shuleni, kazini au popote pale, mara nyingi wanaoanza kufika eneo la tukio wanakuwa hawana uelewa wa kutoa huduma ya kwanza na hivyo kuhatarisha maisha yao wenyewe au ya majeruhi.
Ikizingatiwa kuwa kuna hali ambayo majeruhi asipopata huduma ya kwanza haraka anapoteza maisha.

Swali langu kwa wana jamvi Hivi ni kwa nini hakuna elimu ya huduma ya kwanza kwa wananchi, au kuna mkakati upi wa kusaidia swala hili. (Mfano hata wewe unayesoma hapa ukipata ajali huko barabarani, (siombei upate ajali ni mfano) utahitaji kupewa msaada wa kwanza na watu watakaoanza kufika eneo la tukio, hivi kama hawajui lolote itakuwaje?
 
Ajali zinapotokea barabarani, nyumbani, shuleni, kazini au popote pale, mara nyingi wanaoanza kufika eneo la tukio wanakuwa hawana uelewa wa kutoa huduma ya kwanza na hivyo kuhatarisha maisha yao wenyewe au ya majeruhi.
Ikizingatiwa kuwa kuna hali ambayo majeruhi asipopata huduma ya kwanza haraka anapoteza maisha.

Swali langu kwa wana jamvi Hivi ni kwa nini hakuna elimu ya huduma ya kwanza kwa wananchi, au kuna mkakati upi wa kusaidia swala hili. (Mfano hata wewe unayesoma hapa ukipata ajali huko barabarani, (siombei upate ajali ni mfano) utahitaji kupewa msaada wa kwanza na watu watakaoanza kufika eneo la tukio, hivi kama hawajui lolote itakuwaje?

Dawa ya moto ni moto, hata wewe hapo ulipo ikitokea ajali hapo ulipo kumhusu mtu mwingine wewe unaujuzi gani na huduma ya kwanza???
 
Sasa wewe unajibu swali langu kwa swali,kama huna jibu si unyamaze,Mimi nimeona hili ni tatizo na nauliza wanajamvi ili tuone nini kifanyike,maana kuna elimu ya huduma ya kwanza ambayo kila mtu ni vizuri akaijua,mfano mtu amepoteza fahamu au amevunjika mkono na huduma ipo mbali.nini kifanyike watu wengine wanapoteza maisha kwa kukosa huduma ya kwanza.
 
WATOA HUDUMA YA KWANZA WAPO WENGI tu! ila wapo KWA AJILI YA SEMINA NA PESA NA SI KUTOA HUDUMA.Tena kama huku kwetu KUNA VIWANDA VIWILI VYA KUZALISHA WATOA HUDUMA YA KWANZA ambao husoma kozi hyo kwa MWAKA MZIMA mkuu!
 
Back
Top Bottom