Tanzania masikini jeuri

Tanzania masikini jeuri

chameleon

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2013
Posts
555
Reaction score
170
Wana JF wenzangu naomba mniweke sawa pale ninapokwenda ovyo maana mimi mwenzenu elimu ya uchumi kwa maana ya darasa sina

Mara kadhaa nimemsikia raisi wetu Mhe JK akisema uchumi wetu unapanda na kwamba wale wasiovaa miwani ya mbao kama mimi mtanzania wanaona.

Yapo maswali mengi yanayonifanya nisione ukuaji huu wa uchumi kmf.

1 Elimu na ubora wa elimu umeshuka (ona matokeo na migomo)

2 Huduma za afya na matibabu zimeshuka (tizama dawa hakuna, wagonjwa wanalala chini na migomo ya madaktari)

3 Ajira hakuna wasomi wapo mitaani madiploma na degree wamefungia kabatini

4 Maisha vijijini ni magumu vijana wanakimbilia mjini kuuza matoi na bidhaa feki za Kichina au kucheza pool mchana kutwa

5 Miundombinu ya maji dhaifu watu wanalazimika kununua ndoo kwa Tsh 1000

6 Ahadi za wanasiasa zimeyeyuka. Kumbe zilikua za kutudanganya wenye miwani ya mbao

7 Naambiwa pamoja na yote deni la taifa watakalolipa wajukuu zangu linazidi TRILION 27

7 Orodha ni ndefu nisiwe mchoyo nawaachia wana JF

Najaribu kulinganisha na maisha ya kaya pale BABA mwenyenyumba anapokopa kwa ajili ya kula kuku na vimada (mafisadi) dukani kwa Mpemba (mpangaji) bila ridhaa ya mkewe.wakati kuta za nyumba
Zina nyufa kibao
ETI PONDA MALI KUFA KWAJA? MASIKINI MAMA NA WATOTO
 
Back
Top Bottom