Tanzania ishakuwa nchi ya viwanda

Tanzania ishakuwa nchi ya viwanda

AMAN32

Senior Member
Joined
Feb 6, 2013
Posts
110
Reaction score
55


Habari zenu wanajamii, kuna baadhi ya watu hubeza juhudi za serikali ya awamu ya tano ambayo no ya viwanda,lakini kimsingi tumepiga hatua sana tazama hiyo machine iliyotengenezwa na watanzania,wale wanaoendelea kubeza shauri zao ila sisi tunasonga mbele
Note: mods msibadilishe content ya thread yangu
 
watu walishatengeneza na mafriji ya mafutaa ya taa na bado haikuitwa ya viwanda.... ila sijaelewa kuwa ya viwanda hata vya kizamani au kisasa maanake ...duh!
 
watu walishatengeneza na mafriji ya mafutaa ya taa na bado haikuitwa ya viwanda.... ila sijaelewa kuwa ya viwanda hata vya kizamani au kisasa maanake ...duh!
Mbona hatujawahi kuona hayo mafriji ya mafuta ya taa.msipende kubeza boo
 
Huo ni mradi wa kimasikini, matumizi ya hicho kifaa ni kwenye sehemu zenye shida ya maji, hivyo siyo sustainable project, hauwezi kuuza hizo mashine kwenye miji iliyoendelea au nchi zilizoendelea au shida ya maji ikiisha hiyo mashine itabaki museum. Ni ubunifu lakini ubunifu wa kusuluisha matatizo ya kimasikini. Ubunifu unapaswa kulenga vitu vinanyoweza kupenya mpaka kwenye soko la kimataifa na kutumiwa na watu wote masikini na matajiri.
 
Huo ni mradi wa kimaskini, matumizi ya hicho kifaa ni kwenye sehemu zenye shida ya maji, hivyo siyo sustainable project, hauwezi kuuza hizo mashine kwenye miji iliyoendelea au nchi zilizoendelea au shida ya maji ikiisha hiyo mashine itabaki museum. Ni ubunifu lakini ubunifu wa kusuluisha matatizo ya kimasikini. Ubunifu unapaswa kulenga vitu vinanyoweza kupenya mpaka kwenye soko la kimataifa
Sasa huwezi kwenda kimataifa kama pia hujafanya kitaifa
 
Juu sijui wangine wakoje vile wataka waone mafanikio ya viwanda baada ya 2 years ya manifesto ya Magufuli. Huyu Rais wenyu Kenya wanamlilia hamjui hilo. But acha wale wabaguzi wa kikabila Kenya.
 
Juu sijui wangine wakoje vile wataka waone mafanikio ya viwanda baada ya 2 years ya manifesto ya Magufuli. Huyu Rais wenyu Kenya wanamlilia hamjui hilo. But acha wale wabaguzi wa kikabila Kenya.
Wamchukue sasa kama wanamlilia maana hata sisi tunamlilia wao
 
Huo ubunifu wa mtu unuhusisha vipi na serikali ya awamu ya tano?Sifia serikali ya awamu ya tano kwa kuwakamua wafanyabiashara ila katu usiisifie ukiona ubunifu wa mtu!Lini serikali hii iliwakusanya watu na kuwapa ubunifu?
 
Hii teknolojia iboreshwe, itasaidia sana nyumba za kupanga maana kuchangisha bili za maji vyumba kumi ni mtihani kwelikweli.
 
Huo ubunifu wa mtu unuhusisha vipi na serikali ya awamu ya tano?Sifia serikali ya awamu ya tano kwa kuwakamua wafanyabiashara ila katu usiisifie ukiona ubunifu wa mtu!Lini serikali hii iliwakusanya watu na kuwapa ubunifu?
Ile motisha serikali inayotoa kwa wananchi kuwa Tanzania ya viwanda ndio inawasukuma pia kufanya na kubuni zaidi
 
Chota maji na kamziki pembeni! Hahaha, safi sana, hongera zao..
 
Back
Top Bottom