Sijui kama na kwa majirani wengine ndivyo ilivyo, ila mie kwa hapa niaona niitumie Uganda Kama kielelezo maana mimi ni Mkazi wa Kagera Mkoa unapakana na Nchi ya Uganda. Nimeleta uzi huu kwa kuanagalia mazao mawili muhimu ya Kahawa na Samaki. Kahawa ya Kagera karibu asilimia 30 inavuka mpaka na kuelekea Uganda kwa njia ya ziwa na hata barabara. Jambo hili limekuwa la Muda mrefu. Hivi kwa nini watu wanapendelea kuuza kahawa Uganda? Jibu ni kuwa hivi sasa bei ya kilo moja ya kahawa isiyosagwa kwa Tanzania ni Tshs.1000/= wakati Mganda ananunua kwa Tshs1500/= tena kwa kuifuata mwenyewe. Wakulima wanajiuliza hivi Uganda wanapeleka kahawa soko la wapi ambako Tanzania hawajui? Inawashangaza watu kuona Uganda ili wafikie soko inabidi wapitie Tanzania au Kenya na kulipa ushuru kadha wa kadha, iweje wawe na bei ya juu kwa mkulima kuliko Tanzania ambayo hailipi ushuru kwa nchi yoyote?
Kwa upande wa samaki, hapo ndipo mgogoro kabisa, viwanda vya Tanzania vinanunua kilo ya samaki kwa bei ya Shilingi elfu 4000/= wakati kwa Uganda inaenda hadi Tshs 6000/= hivyo wavuvi wa Tanzania wanapata faida kwa kuuza samaki Uganda kuliko wanunuzi wa ndani? Kwa njia hii Uganda inasafirisha samaki kwa Wingi kuliko Tanzania wakati Tanzania inamiliki sehemu kubwa ya ziwa Victoria kuliko Uganda.
Najua wapo watakaosema wanaouza Uganda Kahawa na Samaki si wazalendo, hawajui kuwa kodi ya mazao hayo ndizo barabara, sawa, lakini naomba wewe ujibadirishe kwa muda tu uwe mukulima au mvuvi, upate suruba zote wanazopata baada ya hapo uje na jibu. Ni nani mhujumu wa uchumi wa Tanzania?
Jamani watu hawako tayari kupunjwa kwa makato rukuki yasiyokuwa na tija kwao. Ukweli ni kuwa ushuru unaopatikana kutokana na mazao hayo ni mdogo kuliko thamani ya Kahawa na Samaki zinazovuka mipaka.
Sina uzoefu na mipaka mingine lakini nadhani kote ni hivyo hivyo, jamani nani ataisadia Tanzania?
Kwa upande wa samaki, hapo ndipo mgogoro kabisa, viwanda vya Tanzania vinanunua kilo ya samaki kwa bei ya Shilingi elfu 4000/= wakati kwa Uganda inaenda hadi Tshs 6000/= hivyo wavuvi wa Tanzania wanapata faida kwa kuuza samaki Uganda kuliko wanunuzi wa ndani? Kwa njia hii Uganda inasafirisha samaki kwa Wingi kuliko Tanzania wakati Tanzania inamiliki sehemu kubwa ya ziwa Victoria kuliko Uganda.
Najua wapo watakaosema wanaouza Uganda Kahawa na Samaki si wazalendo, hawajui kuwa kodi ya mazao hayo ndizo barabara, sawa, lakini naomba wewe ujibadirishe kwa muda tu uwe mukulima au mvuvi, upate suruba zote wanazopata baada ya hapo uje na jibu. Ni nani mhujumu wa uchumi wa Tanzania?
Jamani watu hawako tayari kupunjwa kwa makato rukuki yasiyokuwa na tija kwao. Ukweli ni kuwa ushuru unaopatikana kutokana na mazao hayo ni mdogo kuliko thamani ya Kahawa na Samaki zinazovuka mipaka.
Sina uzoefu na mipaka mingine lakini nadhani kote ni hivyo hivyo, jamani nani ataisadia Tanzania?