Tanzania Daima lamshambulia Zitto?


maneno yaliotumika tu mkuu
 
Hiyo picha haina shida yoyote.Mbona gazeti ninalo na imeandikwa MARAFIKI WA KWELI.Kuna ubaya gani? Mbona sisi huku mtaani CCM na CDM tunaazimana chumvi? Mleta mada analeta uchochezi wa kipumbavu usiyo na maana yoyote.

upo arumeru mkuu? visu, mapnga mshayatupa?
 
Picha na vicheko sidhani kama ni hoja. Manake kama walivyotangulia kusema wengine siasa si uadui wala vita, ila binafsi nimepata taabu kidogo na hayo maneno yaliyoandikwa kama kweli ndivyo ilivyo kusema "marafiki wa kufa na kufaana" nashindwa kuelewa mwandishi ana maana gani.......
 
statizo sio kwa mtoa mada ila liko kwa mwandishi wa gazeti alitaka kutoa picha gani kwa watu hasa kipindi hiki cha siasa za kuviziana?Zitto si tishio tu kwa ccm bali hata kwa baadh ya viongoz wa cdm,watu wanahangaika kuzima nyota yake kila siku.sisi tunajua hakuna ubaya wwt kuwa marafiki hatuna siasa za chuki.Jk atamaliza muda wake then ataiaji km raia sasa uadui wa nn?mwandishi ana ajenda yake
 
Ninaipenda CDM,ninawaamini viongozi wake lkn namna wanavyomkabili mbunge wangu Zitto wananikera!!Why Tanzania Daima and Mwanahalisi always???Not Jambo leo,habari leo or Uhuru???Urafiki wa watu wawili ukifanywa kuwa habari lazima kuwe na hidden agenda(nzuri/mbaya).
 
Mimi sioni tatizo, gazeti kwa kuwa linamilikiwa na mbowe, wapiga picha ni lazima walikuwa wanawatafuta wanachama wa chadema waliokuwepo, hata uhuru wangefanya hivyoooooo..... sio kila wakati kuwa na negative kwa kila jambo
 
No, kuna kitu hapa hakipo sawa. Si zambi kukutana na na Rais lakini kuna mipaka yake. Hasa ukiwa ni mwanasiasa. David na Ed (both Milband and Balls ) huwa wanakutana kila mara ila sijawahi ona wamepiga picha pamoja (labda washamba na sio wastaarabu). Kuna mpipaka yake kwenye siasa.

Picha ya Zitto na kikwete ina ujumbe ufuatao nao ni kwamba Zitto anamkubari sana Raisi ila watendaji wake ndiyo anaona wana matatizo. Swali kama unaona hivyo na wewe unaipenda nchi kwa nini usiende kumumsaidia?

Najua CDM wanajua kuwa tatizo la nchi hii chanzo ni kikwete na zitto anasema hapana kwa mawazo, maneno na matendo.

Zitto kwa ufupi tu akaokoe jahazi la Raisi ampendaye!
 

:A S-baby:Ukweli mtupu!!
 
Huyu lazima atakuwa Tuntemeke maandishi yake yamekaa ki ukuda ukuda tu kutaka kuchonganisha watu.
 
Picha ile imeongea mengi kuliko yote mtakayo-post humu. Rais wetu alikuwa anamkumbusha Zitto kufuta lile bango lake la sahihi 76 za kumwondoa WM Pinda kwa kuwa wale mawaziri fisadi "wote" wameondolewa. La kujiuliza ni vipi Zitto aalikwe kwenye sherehe ambayo imekaa kifamilia na ki-CCM namna ile?
 
Jamani ninalo gazeti hapa na mh; rais kashika glass ya juice mkono wakushoto mkno wa kulia wamekumbatiana na mh; zito wanacheka ni mambo ya kawaida kwenye "cocktail" !!

Tutafute vitu vya kujenga hapa kwenye uwanja wetu, sio majungu na mambo yasiyo kuwa na ukweli ama fikra binafsi na finyu.
 
picha haina tabu hata kidogo labda kama tutaijaza maneno yetu
 
kuna ubaya gani kiongozi kama mbunge kukutana na rais, nyie chadema acheni siasa za kijanjaweed
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…