Tanzania bila CCM haiwezekani

Tanzania bila CCM haiwezekani

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,951
Wale wa ligi za mchangani nadhani bado hawajui ngoma nzito ya CCM.

CCM ni chama bora na imara barani Africa. Hakuna chama chochote Africa kinachoweza kufikia au kukaribia nguvu kubwa ya CCM.

Ndani ya damu yangu inatembea rangi ya kijani. Nimesha kula yamini kwamba CCM milele nitaienzi maana ndio uhai wa taifa letu.
Maisha ya wananchi wa TZ wanategemea uhai wa chama kikubwa Africa CCM.

Kuna hadithi ya samaki kwamba akiwa ndani ya maji anaweza akafanya madoido mengi apendayo kufanya. Huku aikwa hajui nje ya maji kuna maisha gani.

Wengi wamejaribu kuenda nje ya CCM wameona ugumu na hali ngumu. Nje ya CCM ni shida, hakuna heshima ni kurudi chini kabisa.

Tunawaona mawaziri wawili wakuu walichokifanya. Sasa hivi wanaaibika wamekuwa kams hawana akili nzuri. Ni jambo la hatari sana kumtukana mzazi wako. CCM ni mzazi wa wote TZ. bila CCM hakuna Tanzania.

Rais ametoa mda kwa wale waliofanya makosa watubu.
Mnakaribishwa sana kabla ya mlango haujafungwa.

Bila CCM , Tanzania haipo.
 
Cheo unachojipa huko, JPM amesema hakitambui na atapitia upya mfumo wa ajira wa chama. Sio mtu anaibuka na kujiita kamanda wa mitandao halafu anataka chama kimlipe
 
Inashangaza! Chama bora gani kinachopanga kufunga mabao ya mkono? Acha wapinzani wako wafanye kazi zao za siasa ili tukupime kweli kama wewe chama bora.
 
CCM ndio Tanzania
 
Tunaelewa CCM wametutoa pale wakatuleta hapa.. Kila siku mtoto anatambaa kwa sababu ya CCM,majizi na wazee wa vimemo wote wapo CCM.
 
ALL IN ALL WHAT IS THE OVERALL SITUATION OF OUR COUNTRY NOW? ALL DEVELOPED COUNTRIES THEIR PEOPLE ARE STRONG TO STAY STABLE AND CRITICIZE THE GOVERNMENT BUT AFRICAN COUNTRIES IS V/S.
"FEAR OF UNKNOWN IS THE SOURCE OF IGNORANCE POVERTY"
 
WENZENZU WALIOENDELE WANAONGOZWA NA SERA ZA KITAIFA SISI TUNAONGOZWA NA ILANI ZA VYAMA NA MAWAZO YA MTU MMOJA KAMA MUNG
 
umepanic nini hasa?
mkuu achana nae huyo amezaliwa jana na ndio maana anaona maisha bila ccm hayawezekani. kuna watu walisema Tanzania bila Nyrere haiwezekani, ni ujinga.CCM wapende wasipende iko siku itakufa tu hata wafanye nini.ilkufa dola ya warumi na nguvu zake zote itakuwa ccm ya Nchi masikini!
 
Hakuna chama chochote Africa kinachoweza kufikia au kukaribia nguvu kubwa ya CCM.
Nakubaliana wewe mia kwa mia! hakuna!Fanya uchaguzi wa aina yoyote ile kinaibuka mshindi iwe kwa mtutu wa bunduki,vifaru mitaaani, Mabozoka mgongoni na hata hilo likishindikana basi hutia mpira kwapani, hujitangazia ushindi wa kishindo. Lakini kutoa dola kwa vipande vya karatasi ni mwiko!
 
Tanganyika ilikuwepo tangu kuumbwa kwa ulimwengu,na watanganyika walikuwepo chini ya tawala zao za kitemi lakini hawakuyumba.
Wakaja Wajermani baadae Waingereza Tanganyika ipo wala haikuyumba.
1954 akaja mgeni mwingine anaitwa TANU tukampokea akafanya harakati zake zote mpaka tukapata uhuru na hatimae 1964, Tanganyika akaungana na Zanzibar akazaliwa Tanzania lakini hatukuyumba.
Mwaka 1977 TANU na ASP wakaungana akazaliwa CCM hatukuyumba.
Kati ya mwaka 1980 hadi 1985 Tanzania ilipitia kipindi kigumu kiuchumi kuliko wakati wowote ule, tukaambiwa tufunge mikanda tukafunga mikanda maduka hayana kitu sukari,chunvi,sabani dawa za meno nk mpaka upange mstari almaarufu kama bidhaa adimu watu wakafulia hadi majani ya mipapai,watanzania tukavumilia na nchi haikuyumba.
Mwaka 1993 Vyama vingi vikaanzishwa watabiri uchwala wakaonya tutayumba lakini wapi hatukuyumba ndio tukashuhudia kukua kwa demokrasia manyanyaso madogomadogo ya watawala yakatoweka kama moshi,kodi ya kichwa,kunyang'anywa mali kwa raia bila hiyari yao kama kuku,mbuzi,ng'ombe na michango isiyokuwa na kichwa wala miguu iliyopewa jina la kwenda kuimarisha chama ikatoweka, ingawa mali hiyo tuliyoichangia kama watanzania kama viwanja vya michezo kote mikoani vikaitwa vya CCM,ingawa majengo na vitega uchumi vyote vilivyopatikana kabla 1993 ni mali ya wananchi wote wa Tanzania, tukadhurumiwa lakini hatukuyumba.
Kama watanzania walipita katika mageuzi makubwa namna hiyo na uonevu mkubwa namna hiyo hawakuyumba,
Kwa nini leo tunaambiwa Tanzania bila CCM itayumba?
Mimi nasema nchi hata kama itaongozwa na NLD haitayumba hizo ni propaganda za wanasiasa ili waendelee kututafuna na sina shaka kutamka kuwa
TANZANIA BILA CCM INAWEZA KUSHUHUDIA MAENDELEO MAKUBWA KAMA NCHI ZA ASIA.
 
Back
Top Bottom