Tangazo la kuitwa kwenye Usaili wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA)

Automata

JF-Expert Member
Mar 3, 2015
3,349
4,620
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) inapenda kuwataarifu waombaji kazi wote walioomba kazi zilizotangazwa mwezi Desemba, 2107 kuwa, usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 3 – 8 Februari, 2018 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo.

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-
i. Usaili wa Mchujo utafanyika tarehe 3 Februari, 2018 kama ilivyoainishwa kwenye tangazo hili, muda na sehemu usaili ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada;

ii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

iii. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpigakura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria;

iv. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji;

v. Wasailiwa watakaowasilisha“Testimonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (form iv and form vi results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI;

vi. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi;

vii. Kila Msailiwa azingatie tarehe na mahali alipopangiwa kufanyia usaili;

viii. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (TCU, NACTE na NECTA); na

ix. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji yaTangazo husika.

x. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi.


Kuona orodha ya majina ya walioitwa kwa ajili ya usaili pakua nyaraka ya hapo chini
 

Attachments

  • orodha ya majina ya walio itwa kwenye usaili wa mamlaka ya ngorongoro.pdf
    2.9 MB · Views: 743
Mambo ya awamu ya tano hiyo, ajira kila kona

Bado sasa TANAPA
 
duh kuna utitili baadhi ya kada... sema kuna rafiki yangu wamemtumia sms leo kuwa hakufanikiwa ajaribu wakati mwingine.... na nimecheki sijaona jina lake
 
Shortlist gani ya ovyo namna hii.Mfano kada ya procurement wameitwa watu 443 wakati wanaohitajika ni 2 tu kama sio kusumbua watu ni nini?
 
Shortlist gani ya ovyo namna hii.Mfano kada ya procurement wameitwa watu 443 wakati wanaohitajika ni 2 tu kama sio kusumbua watu ni nini?
Sasa mkiitwa mnalalamika msipoitwa lawamawangeitwa hao 50 mngesema umetuma umependeleo hivi lipi lifanyike kwa hili hakuna la kulaumu kumbuka kuna wengine hawajaitwa hivo ndo wamepatikana hao 443 wacha wakapambane kila mtu na bahati yake.
 
Sasa mkiitwa mnalalamika msipoitwa lawamawangeitwa hao 50 mngesema umetuma umependeleo hivi lipi lifanyike kwa hili hakuna la kulaumu kumbuka kuna wengine hawajaitwa hivo ndo wamepatikana hao 443 wacha wakapambane kila mtu na bahati yake.
Wangeita angulau watu 40 wenye sifa za juu kuliko wenzao ndio wafanyiwe usaili. Yaani angulau nafasi 1 ikashindaniwe na watu 20 wenye sifa za juu kuliko sasa ivi ambao kila nafasi 1 itashindaniwa na watu 221 na nyingine 222 .wapo watakaopata pesa za Ku afford gharama za nauli, malazi Pamoja na chakula kwa kukopa huku wengine kutoka katika maisha magumu watauza hata mashamba kupata fedha izo alafu kati yao 443 ni watu 2 tu ndio watakaopata iyo ajira. Bila Shaka wewe sio mtafuta ajira na hauna ndugu anayekabiliwa na changamoto hii ndio maana una support issue hii.

Lengo la Ku shortlist sio kufanya watu wengi wajaribu bahati zao Bali kupata wachache wenye qualification kuliko wenzao watakaokwenda kuchujwa kwenye usaili ili kupata watakaofikia vigezo vya kuajiriwa kwa mujibu wa taasisi husika.
Taasisi nyingi wamekua wavivu wa kushorist kwa kufuata vigezo vya qualifications Pamoja na uwiano mzuri Kati ya wanaitwa kwenye usaili na wanaohitajika kuajiriwa.

Naomba nikuache na swali. Unadhani baada ya kuchukua hao 2 inamaanisha 441 watakaoachwa wote hawana sifa?.
 
Sina nia mkuu ya kukejeli maana hata mimi niliomba ila sijaitwa japo naona nina vigezo vyote pia hali ndo ishakuwa hivi unafikiri nini kitatokea na bila shaka hata mkiwa 1000 ila lazima atapatikana 1 the best haina maana hawa 999 hawana sifa bali ni system tu ilivyo na unajua mtaani kulivyo kugumu.
Anyway hii system ni mbovu ila hakuna namna ndo ishakuwa sasa kila mtu anaeamini kupitia nguvu yake acha akatake risk na siku zote prodit oriented haiko applied kama hujakubali kuobey any risk itakayokuwa inaizunguka hiyo oppurtunity.
 
Sina nia mkuu ya kukejeli maana hata mimi niliomba ila sijaitwa japo naona nina vigezo vyote pia hali ndo ishakuwa hivi unafikiri nini kitatokea na bila shaka hata mkiwa 1000 ila lazima atapatikana 1 the best haina maana hawa 999 hawana sifa bali ni system tu ilivyo na unajua mtaani kulivyo kugumu.
Anyway hii system ni mbovu ila hakuna namna ndo ishakuwa sasa kila mtu anaeamini kupitia nguvu yake acha akatake risk na siku zote prodit oriented haiko applied kama hujakubali kuobey any risk itakayokuwa inaizunguka hiyo oppurtunity.
Unawatetea bure. Ni lazima pawe na uwiano mzuri Kati ya available vacancies na idadi ya shortlisted candidates.
 
Back
Top Bottom